Rafiki yangu na mwanamafanikio hongera sana kwa kuchaguliwa kuiona siku hii nzuri ambayo kimazoea unaweza kuona ni kawaida ila ni bahati ya pekee sana tumeipata na tunapaswa kuitumia ipasavyo kwenye yale ya kusudi kwetu karibu tujifunze pamoja.
SHUHUDA
Rafiki Leo wakati nawasha simu yangu nimekuatana na ujumbe wa meseji unasomeka hivi.
"(666)Pole na matatizo tunakuona ujafanikiwa jiunge na mtandao mkubwa wa matajiri duniani (666)bila kutoa kafara piga 0757838723 kama unahitaji"
Rafiki unaweza kuona namna ujumbe huo unavyofahamu tabia za walio shindwa na wamebaki kutamani kufanikiwa bila ya kufahamu wafanye nini, wengi wanatamani mafanikio lakini hawako tayari kutoa kafara, sielewi neno kafara unalitafsiri vipi lakini tambuwa huwezi kufanikiwa bila ya kutoa kafara nitakueleza chini kwanini ni lazima utoe kafara. Lakini kabla hatujaona umuhimu wa kafara kwenye mafanikio tuone dhana ya kafara na maana yake.
Rafiki kabla sijafahamu kafara ni nini niliamini kafara ni kutoa ndugu na jamaa uwapendao kwa mizimu ili mizimu ikupatie utajiri na pengine aliyetuma ujumbe huo alikuwa anaamini unafahamu hivyo ndio maana akasema bila kutoa kafara je wewe unaamini nini? Je unaweza kwepa kafara na ukafanikiwa?
Kwangu neno KAFARA ninalitafsiri kama hali ya kuamua kuachana na mambo unayoyapenda na yasiyo na tija kwako na kuamua kufuata mambo usiyo yapenda na wakati mwingine yenye kuumiza ila yanakufanya uwe bora na ufanikiwe, Je kwa dhana hiyo utakuwa umeanza kunielewa nini nataka nikuambie.
Rafiki yangu ni vigumu sana kufikia mafanikio ya juu kwa kuendelea kufanya kawaida,kuchelewa kuamka kufuatilia mpira na ushabiki wa kisiasa, kuangalia TV muda mwingi, kwenda kwenye starehe muda wote, kupenda mapumziko kuliko kazi, kufanya matumizi kuzidi kipato na kukopa bila mipango na kutokuwa na tabia ya kujifunza na ukafanikiwa, rafiki kuachana na tabia hizo na zingine kama hizo unaweza kuona ni rahisi lakini sivyo kama udhaniavyo na hapa ndipo KAFARA inahitajika ndugu yangu lazima uwe tayari kuachana na vitu vingi unavyovipenda vosivyo na tija kwako nakufuata vitu vyenye tija hata kama huvipendi, toa kafara hiyo na mafanikio unayoyataka utayafikia kwa haraka.
Ni hayo rafiki yangu nenda katoe kafara Leo, futa yote yasiyo na tija kwako na weka yenye tija, kataa mapumziko yasiyo na maana kwako weka kazi na jitoe kweli kwa kile unachohitaji na wakati mwingine utadharauliwa na kupingwa lakini simama imara utafika na hiyo ndio kafara halisi na achana na zile kafara za kijinga ulizoaminishwa mwanzo.
Asante na karibu tena kwenye ukurasa huu.
Ni Mimi Mwl.Kelvin Kinyaga
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944
No comments:
Post a Comment