Sunday, 31 May 2020

Nzi na nyuki wote wanajituma.........



Rafiki yangu hongera kwa kuweza kuifikia jumapili hii ya Leo, siku ambayo unapaswa kujipima ulipanga kufanya nini kwenye wiki hii, umefikia wapi na Je mpango wako wa mwezi umekamilika kama ulivyopanga? Je unajipangia yapi ambayo mwisho wa mwezi wa Juni utajipima tena? Kama unafanya hivyo hongera ila kama Kila siku unaishi bila ya kujipima na kujifanyia tathimini hata bidii kwenye kile unachofanya ni kazi bure na hapa chini utafahamu kama wewe ni nyuki au nzi.......

Miaka kadhaa iliyopita nilimsikiliza mwandishi mmoja akielezea utofauti wa maisha ya nzi na nyuki,bilashaka ulishawahi kuona Sega la Asari,unaweza kuona jinsi nyuki anavyopata matokeo baada ya jitiada za muda mrefu na mwisho wa siku tunapata Asari tamu kweli.

Upande wa pili tunamwangalia Nzi, ukiona anavyoruka kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine unaona naye anajishughulisha lakini hata kama siyo kwetu bado matokeo anayozalisha nzi ni kwa manufaa yake na viumbe wengine labda wanao mla lakini hakuna cha maana kutoka kwa nzi.

Maisha ya wadudu hawa ni Sawa na maisha yetu, kama Kila siku unaishi bora kumekucha na hakuna mipango yeyote uliyojiwekea na Kila baada ya muda unajipima kuyaendea basi maisha yako ni Sawa na Nzi na hakuna chochote unachozalisha labda faida ni kwa boss wako pekee ambaye anakufanya uwe busy kwa malipo kidogo ya kukufanya uendelee tu kuishi, tafakari na chukuwa hatua.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

Saturday, 30 May 2020

Haijarishi unapitia nini hupaswi kuacha kutekeleza mambo haya manne.....



Habari za wakati huu rafiki yangu ninachoamini ni kwamba kadri siku zinavyosogea ndivyo tunavyokikaribia kifo, huna haja ya kuogopa kwani kufa ni hakika ila siku zote ogopa kutokuishi, maana unaweza kuwa hai lakini huishi bali unaigiza kuishi, muda ni mchache sana Fanya yaliyo sahihi.......

Rafiki yangu huwa kuna siku unakuwa na nguvu sana na hamasa ya juu ya kutekeleza majukumu yako, lakini wakati mwingine unakuta unajihisi uchovu, unahisi kukata tamaa, pamoja na vyovyote vile unavyojisikia wanafalsafa wanatushauri mambo haya manne hatupaswi kuacha kufanya kwasababu yoyote ile.

COURAGE,TEMPERANCE,JUSTICE AND WISDOM

COURAGE (UJASIRI)
Rafiki huwa tunakosa ujasiri kwasababu ya mambo ya nje, pengine ni shida imekuandama ukakosa ujasiri wa kusimamia ukweli, usilazimike kufanya chochote kile kwasababu yeyote ile, kuwa jasiri siku zote, tenda wema na kataa ouvu hata kama utakuumiza, jiambie siku zote kwamba haijarishi napitia yapi nitaendelea kuwa jasiri.

TEMPERANCE(HALI YA JOTO)
Ni kawaida kwetu sisi binadamu pale tunapopitia magumu au kuwa na shida fulani tunakuwa na hali ya unyonge, tunakuwa baridi kwasababu tumepata matokeo ambayo hatukuyatarajia,lakini hilo halina utatuzi kwetu, haijarishi Jana ulishindwa, amka Leo na jiambie ninakwenda kupambana tena, usikubali siku moja ikaharibu siku zingine nyingi, uliferi darasani ondoa unyonge na pambana.

JUSTICE (HAKI)
Kuwa mtu wa haki siku zote za maisha yako, usiwatendee wengine kile ambacho usingependa kutendewa, hakuna mazingira yoyote yatakayokufanya usiwe mtu wa haki, ili litakufanya uwe na nguvu siku zote, Mara nyingi usipotenda haki utakuwa umechaguwa upande usio sahihi.

WISDOM(HEKIMA)
Hiki ni kitu kigumu sana kukitekeleza, lakini kwa kujifunza Kila siku kwenye maisha yetu na kubadilika hakika tunaweza fikia kiwango cha juu sana cha hekima,Kila mtu anatamani sana kuwa na hekima ila niwachache sana wana hekima, kuwa msikilizaji zaidi, usihukumu wengine na kuwa mwepesi kusamehe usiwe mtu wa chuki na visasi.

Basi rafiki ujasiri,kuendelea kupambana bila kuchoka,kuwa mtu wa haki na hekima ni vitu unavyopaswa kuvifanya siku zote kwenye maisha yako haijarishi unayapitia yapi na hakika utaufikia utosholevu wa juu sana kwani vitu hivi ni kama mbegu ambayo wewe mpandaji ndio utavuna matunda kwenye mbegu hizo nenda kayaishi haya.

Kinyagakelvin162@gmail.com

My Email;
https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251
Asante.



Friday, 29 May 2020

Misimamo yako isiyoyumba inavyokuyumbisha......



Katika kitu ambacho ni Zawadi kubwa ambayo unaweza kuitumia vizuri na kufika mbali basi ni upweke,kuna wakati unaweza on a dunia imekutenga, marafiki, shida zimekuandama na huoni mbele, huu ndio wakati mzuri sana ambao uliukosa pale ulipokuwa umezungukwa na kelele za marafiki fake ambao sasa wamekukimbia na hapo unakuwa na utulivu ambao ni nguvu ya kukusogeza unakotaka kufika, pengine ni rafiki zako waliojuwa mipango yako ndio walikufelisha na sasa hawapo, acha kulalamika tumia upweke kufika kule unakotaka kufika...........

Rafiki yangu pengine neno MSIMAMO ni neno ambalo Kila mtu anatamani kuonekana analiishi kwenye maisha yake, lakini nimekutana na wengi ambao misimamo imewafikisha pabaya, msimamo ni kitu kizuri lakini lazima uwe makini na misimamo uliyonayo, Miaka ya nyuma kidogo nilijiwekea misimamo mingi sana, sitaki kuonewa na Niko tayari kufa kuliko mtu kunionea, nitadai haki yangu mpaka niipate na mengine mengi, rafiki yangu mmoja akaniuliza iko wapi ile misimamo yako? Leo hakuna ongezeko lolote kwenye mishahara yetu lakini hujawahi funguwa mdomo kwenye hilo kulikoni?

Kwanza kabisa niseme Happy birthday kocha Aman, Jana ilikuwa kumbukizi ya kuzaliwa kwako na leo kama kawaida yako huwa ukiandika makala inayohusu siku yako ya kuzaliwa huwa unapinduwa fikra za wengi sana, kama mtu alikuwa anafikiria kwenda magharibi unampeleka mashariki, asante kaka Raymond kumfanya atuandikie makala kwenye siku yake ya kuzaliwa na makala ile imefanya niandike misimamo wakati mwingine inatuyumbisha.

Hebu fikiria kama kocha angeendelea kuweka kuweka msimamo wa kutotibu ni wangapi ambao wangekosa huduma yake? Hiyo yote ni matokeo ya kutokuwa na misimamo isiyo yumba, baada ya kutathimini makala ile nimeondoa misimamo mingi ambayo nilikuwa nayo na naanza kujiona nimetoka kifungoni.

Mwaka 2024 Tarehe 01 mwezi wa sita ni tarehe ambayo nilikuwa na msimamo nayo kwenye kazi ninayofanya, baada ya kusoma makala ya kocha nimeboresha wazo langu kwa kuregeza msimamo Wangu, Kwa ufupi tangu 2018 nimekuwa nikipunguza utegemezi Wangu kwenye mshahara kwa asilimia 10 na ikifika tarehe hiyo kwa msimamo wangu natakiwa kuwa nina utegemea mshahara kwa chini ya asilimia 50 na asilimia hiyo 50 kuiwekeza.Sasa ninaongeza kiwango cha kuto utegemea mshahara kufikia 20 kila mwaka ili ikifika tarehe hiyo niwe siutegemei mshahara wangu moja kwa moja kama sasa ila Sitoondoka kwenye Ajira kama nilivyopanga ila nitawekeza zaidi kwenye utowaji elimu bora kwa wanafunzi na nataka kuionyesha jamii kuwa mwalimu siyo dhambi na na wala siyo tiketi ya kuwa masikini bali kutumia fikra zetu vizuri kusaidia wengine, maana niliamini huwezi endelea kuwa mwalimu na kuwa na utajiri, nataka niondoe dhana hiyo kwa kubaki kwenye kada ya ualimu na lazima niwe na utajiri ili kujenga walimu wenye wito wengi na siyo walimu wengi wanao ingia kwenye kada hii ili kupunguza stress na kutoa elimu ya hovyo kwa jamii, nitahakikisha naanzisha harakati za kubadili mfumo wa utoaji elimu ili kuleta manufaa kwa jamii inayotuzunguka.

Uhuru wangu wa kwanza nitaupata kwa kutodai nyongeza ya mshahara tena kwenye maisha yangu na sitolalamika tena kwamba mshahara ni kidogo kama nilivyokuwa nafanya huko nyuma bali ninakwenda kutumia kiasi hiki kidogo kutengeneza utajiri huku nikifahamu siku yeyote kiasi hiki pia kinaweza kisiwepo na hata nikifukuzwa kazi leo nitaendelea kufundisha mpaka mwisho wa maisha yangu ya hapa duniani.

Kinyagakelvin162@gmail.com
Blog;
https://kinyagakelvin.blogsport.com

0763766944.

Thursday, 28 May 2020

"Wengi wape" kanuni iliyokuferisha bila wewe kufahamu....



Umepitia changamoto nyingi sana huko nyuma na nyingi umeshazisahau, amini hata hizi zinazokupa hofu sasa zitapita,usiogope pambana nazo na utakuwa salama,nakusalimu kwa jina la baba na naomba tuwe sote....

Rafiki Leo tuangalie kauli hii maarufu ya "WENGI WAPE" hii inatuambia kwamba maamuzi ya wengi huwa ni sahihi na kile wanachoamuwa wengi basi huwa hakipaswi kupingwa, ukiangalia kwa haraka haraka unakubaliana na usemi huu, na umeishi ukiamini hili na ndio maana umekutana na changamoto nyingi sana.

Kwanza nataka utambuwe kwamba hakuna hata mtu mmoja hapa duniani ambaye mnafafanana naye kwa Kila kitu hata kama ni pacha wako wa kufanana kabisa lazima kuna maeneo mnatofautiana, lakini jamii inataka tufanane, itakufananisha na wengine, kwa kukuambia usifanye hivi kwasababu haiwezekani, alifanya fulani na fulani na walishindwa, hii inatupa picha kwamba wengi tunaishi kwa kutumia vipimo vya wengine.

Nimeona hata makazini kuna maamuzi mengi yanafanywa na wengi wanakuwa na mtazamo fulani wa pamoja na mambo yanafuatwa kwa kutokana na wingi wao lakini baadaye Kila mtu anashangaa maamuzi haya yalipitaje mbona ni ya hovyo? Ni kwa kanuni ya wengi wape.


Sasa Leo tuangalie kwenye fedha Msemo huo kwanini umetuangusha sana.kutoka kitabu cha ELIMU YA MSINGI KUHUSU FEDHA mwandishi ameuliza swali moja linasema hivi;KWANINI ELIMU YA DARASANI NI KIKWAZO KWENYE FEDHA? ameeleza sababu kama saba hivi, lakini Mimi nakwenda kujadili na wewe sababu tatu, ukitaka kuzijuwa sababu zote nunua kitabu ukisome mwenyewe kina mambo mengi ambayo hatutaweza kuyachambuwa yote. Zifuatazo ni sababu tatu kwenye swali hilo hapo juu.

1.Mategemeo na msukumo kutoka kwenye jamii.
Jamii zetu zina mtazamo kwamba mwajiriwa ana kipato cha uhakika na kama mko ndugu wawili mmoja ni mwajiriwa na mwingine ni mfanyabiashara basi jamii itamtegemea zaidi mwajiriwa kuliko mfanyabiashara mdogo, wakati Mara nyingi huyu mfanyabiashara ana kipato kikubwa kuliko mwajiriwa,na hili huwa linaanzia kwenye familia, utegemezi kwa waajiriwa ni mkubwa zaidi na kwasababu mwajiriwa hajawahi Fanya biashara basi atakubaliana nao na kubeba majukumu yote bila hata ya kulalamika kumbe ndugu yake anatumia nafasi hiyo kujinyanyua.

2.Maisha ya maigizo
Kati ya kitu kinachotuangusha waajiriwa na wasomi ni kujiweka kwenye hadhi fulani ambazo siyo asilia, wengi watakuambia kwa degree yako utaanzishaje biashara ya genge? Ya kuuza vitafunwa, biashara ya juice?ndio maana utakuta wasomi wengi Kila siku wanazunguka na bahasha kutafuta ajira lakini kuna kazi nyingi za kuwaingizia kipato hawataki kufanya.Kama umeajiliwa basi uko tayari kuigiza maisha ambayo siyo viwango vyako ili kuwaridhisha wengine, utapandaje daladala si ukope ununue gari? Basi unasema mbona Kila mtu ananishauri hili unafanya.

3.Ujuaji mwingi na kutokuwa tayari kujifunza.
Wasomi huwa tunajidanganya kwamba tumeshasoma na tunajuwa Kila kitu na hivyo hatuko tayari kujishusha na kujifunza, pengine unakuta kijana katoka chuo kikuu, kafika ofisini kawakuta wenye uzoefu zaidi yao na ukizingatia elimu zetu ni nadharia zaidi, akifika ofisini kwakuwa waliopo wana elimu ndogo hataki kujishusha, nenda kampe wazo la biashara ndogo ndogo ya kumuingizia kipato utamuona atakavyokushangaa, kwa kudhani elimu walizo nazo zinawatosha ndio maana Kila siku wanaishi maisha ya kulalamika, ila kwa kujifunza Kila siku na kuchukuwa hatua bilashaka tungekuwa na jamii bora sana.

Rafiki yangu mtazamo wa wengi wape utakuchelewesha sana, jiulize swali ni kwanini 20% pekee ya watu duniani ndio matajiri na 80% wana maisha ya mahangaiko na ufukara? Kama ingekuwa wengi wape kwanini wasingekuwa wamefanikiwa 80% na 20% ndio masikini na vipato vya kati? Njia ya kwenda peponi ni nyembamba na ngumu ila ya kwenda kwenye moto wa Jehanamu ni pana na isiyo na vipingamizi, hivyo amua Leo wapi unataka kupita? Asante sana.

Bonyeza hapa chini

https://kinyagakelvin.blogspot.com

Kupata mafunzo yaliyopita zaidi ya 25.
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944

Wednesday, 27 May 2020

Moto wa matumaini,Ujasiri na uvumilivu vitakuvusha....



Habari za wakati huu rafiki na ndugu yangu, ikiwa Leo ni siku nyingine siku ambayo itakupa ushindi mkubwa, haijarishi kuna vipingamizi gani lakini kwa kutoogopa na kuvikabiri Nina hakika utakuwa mshindi sana kwani ukiogopa changamoto zinakuzoea na kukuona dhaifu hivyo Kila siku zitakuandama,karibu tuwe sote mpaka mwisho......

Rafiki kitu kikubwa unachopaswa kukifahamu ni kwamba;
"ALL ACHIEVEMENT, ALL EARNED RICHES,HAVE THEIR BEGINNING IN AN IDEA''

Magorofa na vitu vyote vizuri unavyovitamani vilianza kama wazo kwa mtu, na hata wewe hapo ulipo ni matokeo ya mawazo uliyowahi kufanya huko nyuma, hivyo kama mawazo hayo yanakuletea matatizo Leo basi Jaribu kuwaza tofauti ili kesho yako iwe kesho yenye matumaini makubwa. Wiki iliyopita tuliangalia hatua sita za kufuata ili uweze kufikia utajiri, kama hukuziandika ziandike na anza kuzifanyia kazi. Kutoka kwenye kitabu cha THINK AND GROW RICH Leo tutaangalia mambo matatu makubwa unayotakiwa kuyaishi ili kufika safari ngumu na yenye vikwazo vingi ya mafanikio.

"KNOW WHAT YOU WANT AND THE DETERMINATION TO STAND BY THAT DESIRE UNTIL YOU REALIZED IT"

Safari yoyote ya mafanikio inataka ufahamu hitaji lako, nini hasa unataka kweli, kisha kuwa na shauku ya dhati ya kupata unachotaka, wengi wanahitaji mafanikio lakini wanakosa shauku ya kuipata fedha, lakini hata wenye vitu hivi vyote viwili bado utahitaji vitu vitatu kufikia ndoto zako.

MOTO WA MATUMAINI
Leo tulio wengi tunafahamu umuhimu wa fedha lakini hatuna ujasiri wa kusimama na kusema tumejitoa, kuweka kazi kweli na kuhakikisha tunaupata utajiri na kupafanya dunia kuwa sehemu bora kuishi kwetu na kwa wanao tuzunguka.

UJASIRI
Watu wengi wamezoea kufanya vitu vya kawaida na wanafikiri Kila mtu anapaswa kufanya kama wao, hivyo ukikosa ujasiri wa kusimama kweli lazima wakutoe kwenye ramani ya kule unakotaka kufika.

UVUMILIVU
Safari ya mafanikio siyo lelemama na ndio maana ni wachache ndio wamefanikiwa, wewe kazi yako ni kuweka bidii na muda mrefu huku ukikabiliana na changamoto, lakini usitarajie matokeo ya haraka, furahia unapoweka bidii zaidi na unaposhindwa badili njia lakini usikate tamaa kwa safari yako.

Hayo ndio mambo matatu unayopaswa kuyafahamu, kwenye kitabu hiki ipo Hadithi ya mtu mmoja ambaye alifahamu uwepo wa madini kwenye eneo lake, lakini baada ya kuchimba kwa muda mrefu bila kupata madini aliamuwa kupauza kwa mtu mwingine na yule aliyepanunua alipoendelea kuchimba baada ya yule mtu wa kwanza kushindwa baada ya Futi tatu tu akayakuta madini mengi sana, Hivi ndivyo tunavyoyaishi maisha yetu, tunapambana lakini tunapokuwa tumebakiza safari kidogo kufikia kule tunakotaka kufika tunakata tamaa na kuacha na kuanza kitu kingine na mambo yanakuwa yale yale.

Kipo ulichoondoka nacho rafiki yangu, weka kazi kweli, Ujasiri ndio nguzo yako na uvumilivu utakupa unachotaka kwani maisha siyo magumu ila kuna watu ni dhaifu kuliko maisha. Asante sana ndugu.

Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944

Bonyeza hapa chini;

https://kinyagakelvin.blogspot.com

Utapata mafunzo mengi yatakayokusaidia kwenye maisha yako.


Tuesday, 26 May 2020

Matatizo yako kifedha yanasababishwa na changamoto hizi mbili......



Rafiki hongera sana kwa kuwa na ujasiri wa kuendelea na mipango yako mizuri pamoja na changamoto unazopitia, hiyo ndio maana ya ushindi, kuendelea kufanya bila kuchoka na hapo unakuwa shujaaa halisi.

Kutoka kwenye kitabu cha THE RICHEST MAN IN THE BABYLON alikuwepo mtu mmoja aliyeitwa Arkad, mtu huyu alikuwa na utajiri mkubwa sana, siku moja rafiki yake wa utotoni alimtembelea na kumuuliza alifanyaje mpaka akaupata utajiri huo? Wakati anakumbuka hakutoka kwenye familia ya kitajiri labda pengine anaweza kuwa ni Mali za kurithi?ndipo Arkadi anamjibu kama mpaka Leo unatengeneza fedha kwa ajili ya chakula na mahitaji madogo madogo pekee basi una matatizo haya mawili, hivyo nataka kushare na wewe matatizo hayo mawili hapa chini.

1.UMESHINDWA KUJIFUNZA SHERIA ZA FEDHA
Pamoja na umuhimu wote wa fedha kwenye maisha yetu lakini elimu hii haifundishwi mashuleni na hapa ndio kunafanya idadi ndogo sana kuzijuwa sheria hizo.

2.UZIFUATI SHERIA HIZO
Wapo wengi wanafahamu sheria chache za fedha lakini kwa makusudi kabisa wanazivunja, watu wanafahamu kabisa kwamba hawatakiwi kutumia zaidi ya kipato chao lakini wanaamua kutumia zaidi na kuishi hivyo kwa maisha yao yote.

Hayo ndiyo matatizo mawali ambayo pengine na wewe rafiki yangu unayo, sasa pengine unajiuliza utapata wapi elimu hiyo wakati mashuleni hawatufundishi?

Kwenye kitabu hiki kupitia maongezi ya tajiri Arkadi na rafiki yake, Arkadi anatuambia aliajiriwa kama mwandishi na alikuwa akiandikia watu,siku moja alikuja Tajiri mmoja ambaye alimtaka Arkadi amwandikie sheria ya Tisa ambayo ilikuwa ndefu na Arkadi alishindwa kuikamilisha kwa wakati aliotaka Tajiri yule aliyeitwa Algamashi, Mtu yule alikasilishwa lakini Arkadi hakuogopa ndipo akamwambia kufika kesho itakuwa imekamilika ila nataka unifundishe ni kwa namna gani naweza kuwa tajiri kama wewe? Ndipo mzee tajiri anamwambia kamilisha kazi niliyokupa nitakufundisha hata na hivyo nimeshakuwa mzee na sasa nitafurahi vijana wakijifunza kwa wazee, anasema maisha ya ujana ni Sawa na Mwanga wa kimondo lakini Busara za wazee ni Sawa na nyota.

Rafiki tutaendelea na simulizi hii wakati ujao lakini nina imani yapo uliyoondoka nayo, Je mtaani kwako hakuna wazee kama Algamashi ukawatafuta wakakuambia ni kwa namna gani sheria za fedha walizo ziishi zimewafanya wakafika hapo? Au tunawaacha wafe na utajiri wao vichwani mwao bila kutuachia?

Asante sana rafiki na uwe na siku njema.

Kinyagakelvin162@gmail.com
Bonyeza kiungo;
https://kinyagakelvin.blogspot.com

Hapo utajifunza masomo yaliyopita kama uliyapoteza.
0763766944

Monday, 25 May 2020

Kwanini wewe siyo tajiri?.......



Habari za wakati huu rafiki, kuweza kukutana na maandishi haya kunaonyesha kwamba u buheri wa afya na kwa hilo sote kwa pamoja tunayosababu kumshukuru mungu wetu.

Rafiki yangu ulishawahi fikiria siku moja Mtoto wako atakapopata ujasiri akakuuliza KWANINI WEWE BABA/MAMA SIYO TAJIRI? utamjibu nini? Ulishawahi fikiria swali hilo?

Basi kwenye kitabu cha RICH DAD,POOR DAD zipo hadithi kadhaa zinazoonyesha namna watoto wanavyoweza kutuuliza maswali hayo na kwenye kitabu hicho ipo siku moja  Robert alimuuliza baba yake kwanini wewe siyo tajiri?ndipo baba yake akampa jibu la kwamba yeye siyo tajiri kwasababu alichaguwa kuwa mwalimu na walimu hawapendi kuwa matajiri wanapenda kufundisha na hivyo kama anataka kuwa tajiri amuulize baba wa rafiki yake Mike atamfundisha kwani ana mipango mizuri ya kifedha. Hapa kwenye kisa hiki mwandishi anataka kutufundisha kwamba waajiriwa wengi hatupendi kujifunza kuwa matajiri na hivyo tunaridhika na kazi zetu,malipo ya mwisho wa mwezi yasiyotosha na kurudi tena kufanya kazi na kulipa madeni yetu,lakini kama tukitaka kupata elimu ya fedha darasani kwenye mfumo wa elimu masomo hayo hayafundishwi.

Adithi ya pili inatuelezea kisa ambacho mama mmoja anaadithia kuhusu Mtoto wake ambaye siku moja alikuja kutoka shule na kumuuliza swali hili;

"Why should I put time into studying subjects I will never use in real life?"
Akimaanisha kwamba ni kwanini aweke muda wake kwenye masomo,kujifunza mambo ambayo hatakuja kuyatumia kwenye maisha yake?

Ndio mama yake bila kufikiri akamjibu kwa kujiamini kwamba;
"If you don't get good grades, you won't get into college and if you don't graduate from college, you won't get a good job,And if you don't have a good job,how do you plan to get rich?
Akiwa na maana kwamba, kama hatopata maksi za juu hatoweza kwenda chuo na asipomaliza chuo hatopata kazi nzuri, sasa bila kazi nzuri atawezaje kuwa tajiri?

Hizi ndizo ngonjera zilizozoeleka huko mitaani kwetu lakini baada ya mama huyo kujibu hivyo ndipo Mtoto wake anamjibu kwa swali? JE MATAJIRI WOTE TUNAOWAFAHAMU WAMEPATA UTAJIRI KWASABABU YA ELIMU ZAO?

Hapo mama akawa mpole na kujisemea kwamba ni kweli tumekuwa tukijibu majibu tuliyozoea na kuambiwa na Wazazi wetu na hayo tunawaamishia watoto wetu wakati yameshapitwa na wakati.

Bilashaka lipo ulilo ondoka nalo rafiki yangu, nikutakie siku njema na wakati mzuri wa kutafakari maisha yako. Asante

Kinyagakelvin162@gmail.com
Blog yangu;
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944

Sunday, 24 May 2020

Vitu vyote duniani vina kasoro ila siyo vibaya.....



Hebu mfikirie mtu anayependa kile anachofanya kwa moyo wake wote, akili na nguvu zake,halafu, mtu anayewapa watu nafasi ya kukosea na mwepesi wa kusamehe na anasema ukweli kwa Kila kitu hata kama utamuumiza na yeye pia, ona mtu huyu alivyo na maisha ya furaha na Amani moyoni mwake, chagua kuishi hivi Leo na siku zote kama unataka......

Leo tutaangalia mtazamo wa kuona vitu kwa UBAYA, pengine wapo watu waliokuumiza sana,wezi na wengine wengi waliokutendea ubaya wa Kila namna, kuna mtu anaweza kukushawishi kwamba watu hao siyo wabaya ukamuelewa? Lakini leo nataka kukuambia mtazamo wowote ulio nao kwenye watu au vitu hakuna ubaya wowote bali kuna kasoro.

Unapoona vitu au watu kwa mtazamo wa kasoro unajipa nafasi ya kutokuwa na chuki na chochote na hasira na yeyote yule kwani hata wewe unakasoro zako, kwani hata mtu anayeonewa ni kwa sababu ya upofu wake ambao ni kasoro ndio maana wengine wanaona kwa niaba yake na pale atakapogundua kasoro yake hatokubali kuonewa na yeyote.

Hebu fikiria mwizi kavunja na kakuibia Mali zako, ukiwaza kwa ubaya unaweza kuona chuki dhidi ya mwizi huyo ukikutawala na bahati mbaya usimuone na siku nyingine ukaibiwa tena kwani hata mwizi huyo anaona kasoro zako na ndio maana anakuibia Kila siku lakini pale unapoona kasoro zilizopo zaidi kwako unawasaidia hata wanaokutendea ubaya.

Ukichukulia mfano wa mwizi hapo juu, kwa mtazamo wa kasoro zilizopo upande wako unaanza kuona pengine ni geti lako linashida,pengine unahitaji kuweka ulinzi kwenye eneo lako au uzembe wowote ambao utakufanya uchukuwe hatua. Je umetapeliwa? On a kasoro zako na lekebisha, acha kukimbilia kulaumu wengine kabla ya kuona kasoro zako,wengine wanapokukosea wanakuonyesha kwamba kuna vitu vina kasoro na unapaswa kurekebisha.

Pengine kwa hayo machache utakubaliana na Mimi kwamba hakuna kitu chochote kibaya bali kuna kasoro na jifunze kuona wema kwenye Kila ubaya, Asante najumapili njema.

https://kinyagakelvin.blogspot.com
Email yangu;
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944

Friday, 22 May 2020

Tatizo halipo kwa anayekulipa na kiasi unachopokea.......


Hongera rafiki kwa siku hii ya Jumamosi ya tarehe 23/05/2020 hakuna siku nyingine itakayo kuja ikafanana na siku kama hii kwa Kila kitu, lakini bado sisi binadamu tulio wengi tunazichukulia siku kama vile ni kitu ambacho tunacho muda wote na milele, basi kwa Mimi rafiki yako kukumbusha hilo sitegemei kama unakwenda kuipoteza siku ya Leo kwa kufanya yale uliyozoea kufanya.

Rafiki yangu Jana niliandika makala yenye kichwa cha habari kinachosomeka SONGOMBINGO ZA BAJETI,kwenye makala ile nilieleza changamoto baadhi ambazo wengi tunakutana nazo na kujikuta tunaingia kwenye madeni, na kwa kunukuu makala kutoka kwa kocha toka kwenye kitabu cha THE WAR OF ART na kusema kutofahamu nini cha kuanza nacho kati ya HARAKA na MUHIMU na kuorodhesha matumizi muhimu ni yapi baadhi ya rafiki zangu walionyesha kutoridhika na Maelezo yale kwa msingi wa maswali mawili ambayo nitayatolea ufafanuzi hapa chini.

1.Unafanyaje pale matumizi muhimu yanapokuwa makubwa kuliko kipato chako?
Baada ya kumnukuu mwanafalsafa Seneca kwamba matumizi muhimu ni machache ila anasa ndio gharama na nyingi yupo mmoja hakukubaliana na hilo kwa kusema Je kusomesha, kujenga nyumba,chakula, mavazi hayo ni Anasa? Nilimuomba awe mtulivu na Leo nakwenda kumjibu.

Rafiki kitu ambacho kinawagharimu wengi ni kuishi maisha ambayo hawalingani nayo, naweza ita maisha ya Jirani zao, utakuta mtu anapoelezea matatizo ya kifedha aliyo nayo na madeni aliyo nayo kwasababu ya matumizi muhimu aliyonayo unaweza kumuonea huruma na kukubaliana naye, tatizo ni kwamba wengi tunaangalia tulipoangukia na siyo tulipojikwaa, kosa ambalo wengi tunalifanya ni kuyapa mambo umuhimu kwa kufuata mkumbo, mfano wengi wanaingia kwenye madeni kwa kisingizio cha kulipia wototo ada, lakini swali ni je kipato chako kinaruhusu wewe kupeleka watoto wako kwenye shule unazowapeleka? Au kwasababu umeona watoto wa Jirani wanasoma shule nzuri na wewe hutaki kuonekana wa chini unawapeleka? Hivi ndivyo tunavyoendesha maisha yetu kwenye Kila kitu,lazima mwanzo ukubali kuishi chini ya kipato chako na kisha ufanye jitiada za kukiongeza bila ya kukaa na kusubiria mwajiri wako, Fanya biashara na jishughulishe.

2.Swali la pili nililoulizwa ni JE UNAVYOSISITIZA MARA NYINGI NA KUTUONYESHA MADENI NI KITU KIBAYA MBONA KUNA WENGI WANAFANIKIWA KUPITIA MIKOPO?
Nadhani swali hili kwa wanakisima cha maarifa wanaelewa vizuri na huko mbele tunavyoendelea kuchambuwa vitabu utajifunza kwa kina kupitia kitabu cha elimu ya msingi kuhusu fedha, lakini kwa Leo nikupe siri moja ambayo unapaswa kuijua unapokopa, kabla hujakopa jiulize maswali mawili NANI ATALIPA? na swali la pili NITATOA WAPI? unakuta mtu anakopa kwasababu kipato hakitoshi na wakati huo huo atapaswa kulipa kupitia kipato hicho hicho, Kwanini wengine wanakopa na kufanikiwa? Jibu ni kwasababu wanakopa wao lakini hawalipi wao, mfano mfanyabiashara anaweza kukopa kwasababu tayari anawateja lakini hana mtaji, hivyo anapokopa anafahamu mteja wake ndiye atakayelipa deni hilo, Je kivipi? Pengine nimekopa milioni mbili ili niongeze mtaji kwenye biashara yangu,milioni mbili ikazalisha milioni tatu, hata kama natakiwa nilipe liba laki tano bado nitabaki na faida ya laki tano. Hivyo hiyo ziada yote imetokana na wateja wake lakini siyo kwenye kipato chake cha awali.

Rafiki yangu tuendelee kuwa pamoja Nina hakika tutavuka pamoja, tamaa yangu ni kuiona Tanzania yetu inaondokana na ufukara huu kupitia mafanikio ya mtu mmoja mmoja, hivyo tambuwa hakuna aliyezaliwa kwa ajili yako hivyo kumlaumu boss wako au serikali ni kuchaguwa kushindwa.

Mwl.Kelvin Kinyaga
https://kinyagakelvin.blogspot.com
Email yangu ni;
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944

Songombingo za bajeti........



Hongera sana kwa kuweza tupia jicho lako kwenye ukurasa huu, wapo wengi wangetamani kupata nafasi hiyo lakini hawakuweza, kwa Maradhi,kwasababu muda wao wakuwa duniani umepita na Kila namna nyingine kadha wa kadha,hivyo bahati hiyo usiitumie kusoma na kufurahia nenda kayafanyie kazi.

Leo tuangalie bajeti na changamoto zake, serikali yoyote huwa na kipindi ambacho kupitia bunge lake wanakaa na kupanga bajeti, hii inatupa picha kwamba bajeti ni kitu muhimu sana. Pamoja na umuhimu huo bado utakubaliana na Mimi bajeti ina changamoto zake, changamoto ya kwanza ni wakati gani mzuri wa kupanga bajeti?

Kosa kubwa ambalo wengi tunalifanya ni kupanga bajeti baada ya kuwa tumeshapokea fedha.

Tarehe 18/05/20 nilisoma makala bora sana kutoka kwa kocha ikieleza ni kipi cha kuanza nacho kati ya haraka na muhimu? Je nikikuuliza wewe kama unapaswa kuweka kipaombele kati ya haraka na muhimu utachaguwa kipi?

Sasa Mara nyingi tunapopanga bajeti baada ya kuwa tumeshapokea fedha huwa hatuweki uzito kwenye muhimu na tunaweka uzito kwenye haraka na pale muhimu vinapokuwa vimefikia muda wake huwa haviwezi kusubiri na hapo ndio wengi tunaingia kwenye mtego wa mikopo na madeni.

Nini cha kufanya?
Panga bajeti yako kabla hujapokea fedha unazotarajia au kipato chako, hapa utaona ni vipi muhimu unapaswa kuviwekea bajeti na achana na vingine vyote ambavyo utaviona vinahitaji haraka wakati umepokea fedha, maana wengi hawatumii bajeti kwenye maisha yao na wanaopanga bajeti pindi wakipata fedha wanatumia kwa vitu vingine vya haraka na vile muhimu vinawarudisha kwenye madeni.

Je matumizi muhimu ni yapi?
Hela ya chakula ni muhimu, ada za watoto,kodi ya nyumba, bili za Umeme, Maji,fedha ya dharula,fedha kwa ajili ya matibabu, lakini utakuta wengi kwasababu vitu hivi havihitaji fedha yako kwa Mara moja wengi wanajisaulisha na kusubiria mpaka muda utakapofika ndio waaenze kupambana nayo, lakini utakuta mavazi, michango ya sherehe ni vitu ambavyo wepesi kutoa, rafiki kanuni itakayokufanya ufanikiwe haijawahi kubadilika TUMIA KIASI KIDOGO KULIKO UNACHOPATA na hili litawezekana kupitia bajeti na ukishaweka bajeti yako kataa vishawishi vyovyote vile vitakavyojitokeza na kukulazimisha utumie nje ya bajeti yako.

Rafiki hiyo ni sehemu ndogo sana lakini ilishanitesa sana huko nyuma na kwasababu sipendi ukosee kama Mimi ndio ujifunze,  nakuletea makala hii ufanyie kazi ili tuvuke pamoja na kufurahia Zawadi ya maisha ambayo mungu katupatia bure kabisa, asante sana na nikutakie siku njema.

Mwl.Kelvin Kinyaga;
https://kinyagakelvin.blogspot.com
Email yangu
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944.

Thursday, 21 May 2020

Anza asubuhi yako na S.A.V.E.R.S.....



Rafiki bilashaka umeanza siku yako ukiwa na utulivu kabisa na unaomba mungu siku yako iendelee na utulivu huo, uko Sawa lakini upande mwingine jiandae na watu wasio na shukrani, wenye kukukwaza na kukuvuruga ili pale wanapojaribu kukuvuruga usipatwe na mshituko wowote na hali hiyo itakupa hekima ya hali ya juu kukabiliana nao kwa kujiambia sitajibizana nao wala kugombana nao, karibu tuendelee........

Rafiki na ndugu yangu, linapokuja swala la asubuhi Kila mmoja wetu ana utaratibu wake, wapo wanao amka na kuanza na kushika simu zao na kuperuzi mitandao ya kijamii, wapo wanao anza asubuhi zao kwa kusikiliza habari magazetini, wapo wanaonza asubuhi zao kwa kubishania michezo na Kila namna nyingi kadri ya mapenzi ya mtu, pengine kwa kuanza siku yako na utaratibu wako huoni kama kuna tatizo lolote na unaweza kushangaa kwanini ifike sehemu nishauriwe ni kwa namna gani niianze siku yangu,rafiki kwenye ulimwengu huu wa habari kuna Kila habari na ni wewe ndio mwamuzi wa kipi unapaswa kusikia na kipi huhitaji, lakini kile unacholisha akili yako ndicho utakachovuna,kama Kila siku unalisha habari hasi za kukatisha tamaa au za kuhuzunisha ndivyo utakavyoyaishi maisha yako, na habari nyingi za mitandao ya kijamii ni hasi kwa zaidi ya 90%.Habari zote muhimu unaweza kuzisikia bila hata kukimbilia kwenye mitandao ya kijamii, siku zetu ni mfano wa maisha yetu, tunapokuwa vijana tunakuwa na nguvu kubwa ya kazi lakini tukishafika uzeeni tunakuwa hatuna nguvu hizo, sasa unapoanza siku asubuhi unakuwa na nguvu kubwa sana na inapofika jioni nguvu hizo upunguwa hivyo ukianza na habari hasi unakuwa umepoteza nguvu zako kwa haraka sana, hivyo hapa chini tunakwenda kujifunza kanuni bora ya kupangilia asubuhi yako na ukajikuta hupotezi nguvu zako na unafanya mengi ambayo usingeweza kufanya kama ungechaguwa kuendelea kuanza siku na habari za mitandao.

S.E.V.E.R.S
Wiki iliyopita nilitumiwa kitabu na rafiki yangu Dr.Raymond Mgeni,kitabu hicho kinakwenda kwa jina la MIRACLE MORNING FOR WRITERS na kimeandikwa na Hal Elrod&Steve Scott,mwandishi kaonyesha anakiandika kwa ajili ya waandishi lakini nina amini yaliyomo humu yanamsaidia Kila binadamu mwenye kujuwa kusudi la maisha yake. Hatua ya kwanza tutakwenda kuzielezea harufi hizo moja baada ya nyingine na maana zake.

1.Herufi 'S'
Herufi hii inasimama kwa neno SILENCE, watu wengi wanaanza siku kwa kelele, mitandao ya kijamii,habari ni kelele. Unapoanza siku yako kwa ukimya, pengine ukatumia dk 5 kumshukuru mungu na dk 10 kutuliza akili yako,kuwa na utulivu mkubwa kiasi kwamba una uwezo wa kuyasikiliza mapigo yako ya moyo, wazungu wanaita Meditation, hii itakuondolea stress na itakupa utulivu mkubwa sana, watu wengi hukosa kabisa muda huu na ndio maana mambo yao muhimu wanayakumbuka wakiwa mariwatoni au bafuni kwani ndio sehemu pekee wanapokuwa peke yao. Hivyo rafiki Tenga muda wako asubuhi sana Kila siku kabla ya kufanya chochote na fanya tahajudi(meditation) yako.

2.Herufi 'A'
Herufi 'A' inawakilisha neno 'AFFIRMATION'.Neno hili linakutaka uwe na maneno ambayo utayasema na yanakupa nguvu ya kuendelea na kile unachohitaji, pengine umechoshwa na madeni na unataka kuachana nayo. Ukayaandaa maneno ambayo unayasoma. Mfano.Nimekuwa kwenye utumwa wa madeni kwa kipindi kirefu na nimechoshwa na utumwa huu, kuanzia Leo siwezi kukubali kuendelea na hali hii na nitahakikisha namaliza madeni yote, niko tayari kushindia uji lakini niondokane na utumwa huu. Baada ya kutamka maneno hayo Kila siku asubuhi sidhani kama utashindwa kuondokana na madeni. Hivyo unaweza kuweka maneno yoyote kwa kile unachohita na Nina amini utafanikiwa.

3.Herufi 'V'
Herufi 'V' inasimama kwa neno 'VISUALIZATION'. Hapa unatengeneza picha ambayo iko kwenye akili yako, pengine kwa mfano wa mtu mwenye madeni hapo juu, anaweka picha kwamba baada ya muda fulani atakuwa hana deni, ataanza kuwekeza akiba na atafunguwa malengo account na anaona amekuwa mfanyabiashara mkubwa, anamiliki nyumba na mengine mengi, kuwa na picha ya kile unachotamani kunakupa nguvu ya kuchukuwa hatua.

4.Herufi 'E'
Herufi 'E' inasimama kwa neno 'EXERCISES' rafiki mazoezi ni kitu muhimu sana kwenye maisha yetu, mwili wenye afya ni mwili wa mazoezi, tumia dakika si chini ya 10 kufanya mazoezi ya viungo, kimbia, luka kamba na hili litaupa mwili nguvu ya kupambana na Afya ya mwili na hilo ndio mwanzo wa mafanikio mengine, kwani afya kwanza mengine ziada.

5.Herufi 'R'
Herufi hii inasimama kwa neno 'READING',tengeneza utamaduni wa kusoma, ukiweza kusoma kurasa 10 kwa siku na hili litakufanya ulishe akiri yako, kwani mwili wenye chakula usio na chakula kwenye akili yake ni mwili usiokuwa na macho, kwenye vitabu kuna utajiri mkubwa sana.

6.Herufi 'S'.
Inasimama kwa neno 'SCRIBING'ambalo lina maana Sawa na neno 'WRITTING',rafiki kuandika ni muhimu sana, unaweza kuandika ratiba ya majukumu yako ambayo unakwenda kuyatekeleza kwenye siku yako, ikiwezekana andika na wale utakaopaswa kuwasiliana nao kwenye siku unayoiendea, andika matumizi unayotarajia kufanya kwenye siku yako.

Rafiki kwa kuanza na mtililiko wa neno S.E.V.E.R.S Kwenye siku yako utakuwa mtu mwenye hamasa sana kwenye siku unayoiendea na asubuhi yako itakuwa tulivu sana, ukiamka masaa mawili au moja kabla ya kwenda kwenye shughuli zako na kutekeleza haya hakika utakuwa umeanza kwa ushindi mkubwa, nenda kayaishi haya kwenye siku yako na utanishukuru, mwanzo hautakuwa rahisi hivyo pambana mpaka ufanikiwe kwenye hili.

Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944

Wednesday, 20 May 2020

Dhana mbili unazopaswa kuzijuwa kuhusu fedha....



Asubuhi huwa na nguvu pale unapoamka na kumshukuru mungu kwa uhai,kwa watu wazuri wanaokuzunguka,familia yako,mume au mke wako, watato kama umejariwa na vile vyote vinavyokupa nguvu ya kusonga mbele, lakini kuianza siku yako kwa kukumbuka watesi, adui zako au wale wote wanaokuchukia ni kuamua kukaa mbali na furaha na kuishi maisha ya chukizo.

Rafiki Leo tutaangalia dhana mbili zilizobakia kati ya tatu ambazo unapaswa kuzifahamu, kutoka kwenye kitabu cha Dr Makirita Aman cha ELIMU YA MSINGI KUHUSU FEDHA nilieleza dhana moja ambayo ni FEDHA,ukirejea makala yangu ya tarehe 09/05/2020 nilieleza kwamba fedha ni zao la Thamani, na haya makalatasi tunayoamini ndio fedha ni njia tu ya kubadilishana thamani, Leo tuangalie dhana mbili zilizobakia kuhusu fedha unazopaswa kuzifahamu.

1.Utajiri ni nini?
Yapo maneno mengi kwenye fedha tunayatumia bila kufahamu maana yake ni nini? Ukisikia neno tajiri bilashaka unafikiri mtu mwenye magari ya kifahari, nyumba nzuri na aina ya umiliki wa vitu vingi vya thamani, hebu tuone maana halisi ya neno Tajiri. UTAJIRI ni hali ya kuwa na kiasi cha kutosha,kupitiliza hata uhitaji ambao mtu anao. Hivyo basi unaweza kuwa na Utajiri kwenye eneo fulani lakini sehemu ambayo bado una uhitaji bado hujawa na utajiri, hivyo nyumba,magari na ufahari mwingine ni sehemu ndogo ya utajiri na ndio maana watu wengi wanapambana kupata utajiri na wakiupata wanagundua bado kuna vingi wanahitaji na kama furaha wanaweka hapo basi siku zote wanakuwa wamejinyima furaha.

2.Uhuru wa kifedha ni nini?
Unaweza kuwa na fedha na ukawa na utajiri lakini usiwe huru kifedha,hebu tuone maana halisi ya UHURU WA FEDHA ni pale ambapo mtu anakuwa hana tena hofu kuhusu fedha.mtu kwenye hatua hii ana uhakika wa kuendelea kuishi atakavyo mladi havunji sheria na maadili, hata kama hafanyi kazi moja kwa moja, hapa mtu anakuwa amefanya uwekezaji ambao hahitaji tena kulazimika kufanya kazi moja kwa moja ndio fedha iingie.

Kwa kufahamu dhana hizi tatu kifedha utakuwa umejuwa uko wapi kwenye uelewa kwenye fedha mpaka sasa na utajisukuma mpaka siku moja ufikie Uhuru kifedha. Basi tuangalie maswali matatu ambayo nimewahi kukutana nayo pale nilipojaribu kuelezea dhana hizi tatu za fedha.

A.Umesema fedha ni mbadilishano wa thamani je wanaocheza bahati nasibu na kushinda fedha nyingi wanakuwa wametoa thamani gani?
Hapa rafiki tunaweza kuona swali hili zuri linasibitisha kwamba kweli fedha ni mbadilishano wa thamani, hebu angalia watu hawa baada ya miaka kadhaa wanarudi kwenye maisha yao ya ufukala,tena unaweza kuta ni wa kutupwa Mara dufu, unawakumbuka washindi wa BSS?wengi wako wapi? Unafikiri ni kwamba hawakuwa na vipaji? Kama umepata fedha nyingi tofauti na thamani uliyotoa basi muda si mrefu utarudi ulikotoka.

2.Umesema utajiri ni kuwa na kiasi cha kutosha na kupitiliza hata uhitaji ambao mtu anao, je inawezekanaje mtu akafikia hatua akakosa uhitaji? Hapa ndio maana dhana hii huwa inawachanganya wengi, kwanza tufahamu mahitaji muhimu ni rahisi sana kuwa nayo ila gharama nyingi ni anasa za duniani, lakini kwanini tunapaswa kuutafuta utajiri bila kukoma? Wapo wengi sana wenye uhitaji, masikini, waremavu na wengine wengi wanaweza nufaika na utajiri, tunaangaika na vingi kwa ajili ya wengine na si kwa ajili yetu pekee, Doctor hakusomea udaktari ili aje kujitibu bali kutibu wengine.

3.Hiyo dhana ya Uhuru kifedha mbona ni ngumu, inawezekanaje mtu apate fedha bila ya kufanya kazi? Kwenye kitabu hiki ukikipata na kukisoma kimeeleza kwa kina kuna watu wanamiliki hisa nyingi kwenye makampuni, kuna mtu niliwahi msoma anamiliki nyumba za kupangisha zaidi ya 10000 je huyu anakuwa ameshafikia hatua kwamba alishafanya kazi huko nyuma lakini sasa fedha inamfanyia kazi yeye. Hii ni hali ambayo ukiifikia unakuwa na utosherevu mkubwa sana.

Rafiki siku zote pigana ukijuwa ni wapi unataka kufika na baada ya kuzifahamu dhana hizi tatu Nina imani akili yako imefunguka sana, kwa maswali zaidi kuhusu dhana hizi tatu tuwasiliane kupitia.

https://kinyagakelvin.blogspot.com
Email yangu; Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944.

Tuesday, 19 May 2020

Hatua sita za kufuata ili kujipatia uhuru kwenye fedha......



Bila shaka neno asante ndio neno linalopaswa kuwa la kwanza kutamkwa kwenye Kila asubuhi yako, kwani kuishi na kuiona siku ni bahati tu na upendeleo mkubwa hivyo kupoteza muda ni kauli inayotumiwa na watu waliozoea kuchezea shilingi kwenye tundu la chooni, sina shaka na unayesoma hapa kwamba unafahamu umuhimu wa muda na kamwe hupotezi kwa mabishano,masengenyo wala kufanya yale yote yasikuwa na tija au kukuongezea hekima, kwani kwa kufanya hivyo ni kuchagua kupoteza kabla hata hujapata.

Rafiki Leo tutajifunza hatua sita unazopaswa kuzifuata ili kufikia Uhuru kifedha.....,hatua hizi tunazipata kutoka kwenye kitabu cha THINK AND GROW RICH karibu tuwe sote mpaka mwisho wa makala hii na hutabaki kama ulivyo.

1.Unahitaji kiasi gani cha fedha?
Rafiki utakubaliana na Mimi kwamba akili zetu zinajisukuma kwa kadri ambavyo tunazishughulisha,wengi tumezoea kutafuta fedha kwa ajili ya matumizi muhimu ya Kila siku na tukipata zaidi ya hapo tunazitumia vibaya na kisha kurudi kwenye maisha yetu tuliyozoea, hivyo kwenye kitabu hiki tunashauriwa kujiwekea kiwango ambacho tunaweza kujisukuma na kukipata lakini kisiwe kikubwa cha kutukatisha tamaa,tatizo siyo kuweka kiwango kikubwa na kushindwa kukifikia bali tatizo ni kujiwekea kiwango kidogo na kukifikia, mwandishi mmoja amewahi kusema.

2.Je ni kitu gani upo tayari kulipa ili uweze kufikia kiwango hicho?
Hakuna kitu ambacho utakipata bila ya gharama, lazima uwe tayari kugharamia ili uweze kupata unachotaka, pengine muda mwingi unajihusisha na kuangalia Tv,pengine ni kupumzika ndio kitu unapenda,pengine kukaa bila kufuatilia maisha ya wengine, pengine maisha ya kujinyima hukuzoea, haya yote ni baadhi ya gharama ambazo lazima uwe tayari kuzilipa, mwandishi mmoja amewahi kusema ukitaka kufanikiwa lazima uwe tayari kukataa vitu unavyopenda na kuchaguwa vitu usivyovipenda vinavyokufanya uwe bora.

3.Amua na Panga tarehe ambayo unataka uwe umeshakifikia kiwango hicho.
Kocha Wangu anapenda kusema chochote kisicho na muda wa kukitekeleza basi hakiwezi kutekelezeka, hivyo huwezi weka kiwango unachotaka kukifikia halafu usiweke ni lini unatakiwa kuwa umeshakikamilisha.

4.Tengeneza mpango wa kukifikia.
Lazima uwe na mkakati wa kukifikia, pengine nitaanzisha biashara ya chakula, au kuuza vitafunwa au nitatoa kwenye mshahara Wangu, kwa wiki nitatakiwa niwe nimepata 10000 na kwa mwezi 40000 na kwa mwaka ni 480,000. Bila kuwa na mpango kamili hiyo inabaki kuwa ndoto kupata kiasi hicho.

5.Kuwa na Maelezo mafupi yanayotaja kiasi cha fedha unachohitaji.
Mfano. 480,000 iwe imepatikana mpaka kufikia tarehe 01/01/2021 kutokana na biashara ya vitafunwa ninayofanya na Kila wiki lazima iwe imepatikana Tsh 10000 na kwa mwezi 40,000. Hivyo siku zote utakuwa unapambana kufika hapo.

6.Yasome yote uliyoandika hapo juu Kila siku Mara mbili.
Basi hatua ya mwisho ni kuhakikisha Kila siku asubuhi unasoma kile ulichokiahidi mwenyewe na unataka kukifikia, pia jioni kabla hujalala unapitia tena na kujipima kama unaendea kupata au la!,hivyo Jua liwake mvua inyeshe hutokubali kujipa sababu kwanini hujapata kiasi hicho.

Hivyo rafiki ndivyo mwanzo wako wa kufika unakotaka kufika unavyoanza kufanyiwa kazi, lakini ukijiambia unahitaji fedha nyingi bila kujuwa unazipataje na lini ikifika uwe umezipata na mkakati upi unao wa kufikia lengo lako unakuwa umechaguwa kushindwa, na pindi utakapokifikia kiwango hicho unajipongeza na kupanga kiwango cha juu zaidi na kufuata hatua hizo sita.

Asante sana rafiki na nikutakie siku njema na kazi njema pia.

https://kinyagakelvin.blogspot.com
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944.
#Tuvuke pamoja


Monday, 18 May 2020

Bidii ya kazi pekee haitoshi kukupa uhuru wa kifedha......



Rafiki yangu hongera kwa majukumu na hatua unazochukuwa Kila siku kwani bila kupiga hatua au kuchukuwa maamuzi yoyote tofauti na mazoea na kutarajia mabadiliko ni kujidanganya, kwani huwezi Fanya kitu kile kile ulichozoea kufanya na kwa namna ile ile na kukaa usubirie mabadiliko, huko ni kujidanganya,ni Sawa na kwenda chini ya muembe na kutarajia kuokota maparachichi, Kila siku jiulize LEO NIMEFANYA NINI CHA ZIADA TOFAUTI NA JANA?.........

Rafiki Leo tuangalie dhana ya FANYA KAZI KWA BIDII, kama siku zote ninavyosema mafanikio yoyote hupatikana kwa muunganiko wa vitu vingi, bidii kwenye kile unachofanya peke yake haitoshi kukupatia mafanikio.

Hebu tuangalie adithi kutoka kwenye kitabu cha THE RICHEST MAN IN THE BABYLON,hapa tunakutana na marafiki wawili Bansier na Kobbi,Kobbi anamkuta Bansier amekaa akitafakari kwa kina,anamuomba amuazime Shekeli mbili na Bansier anamjibu kama angekuwa na hizo shekeli mbili basi asingethubutu kumpa yeyote kwani na yeye anaziitaji, Basi Kobbi anamuambia Bansier kama hana fedha kwanini asiendelee na kazi ya kutengeneza magari yaliyopo ili apate fedha? (Bansier alikuwa fundi magari) na hapa Bansier anamjibu Kobbi kwamba alishafanya sana kazi na kupata hela nyingi huko nyuma lakini mwisho wa siku anajikuta hana kitu na amerudi kwenye maisha ya awali na kwa Hili Kobbi anakubaliana na Bansier kwani amekuwa akifanya kazi kwa bidii na anapata fedha lakini baada ya muda anarudi kule kule, baada ya kufikiri kwa kina wanakumbuka yupo tajiri mmoja mkubwa sana anaitwa Arkad ni bora waende wakamuulize ni wapi wanakosea ili waweze kurekebisha.

Hapa tunajifunza somo kubwa sana kwamba unaweza ukaweka bidii kwenye kazi na ukapata fedha lakini kwasababu huna elimu ya fedha hujuwi fedha inatakiwa iwekezwe wapi ili ikufanyie kazi, kwani kama Kila siku unaifanyia kazi je ni kwa vipi unatakiwa uiwekeze ukiipata ili ikufanyie kazi na usirudi kwenye hatua za mwanzo, Je ni wangapi wanaendesha maduka yao kwa zaidi ya miaka 20 na yapo vile vile hayakui? Wangapi wameweka bidii kwenye kazi na bado hawajapata kile wanachotaka?

Basi rafiki yangu tuendelee kuwa pamoja kwenye chambuzi za vitabu hivi yapo mengi ya kukufumbuwa macho, asante na siku njema.

https://kinyagakelvin.blogspot.com
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944
#Tuvuke pamoja


Sunday, 17 May 2020

Kama wewe mwenyewe umeshajiambia huwezi kupata basi hakuna atakayekupatia.........



Rafiki yangu habari za wakati huu, Nina imani hujambo na unafurahia maisha pamoja na yale yote unayopitia, karibu tushirikishane machache ili tuwe na msingi imara kwenye maisha yetu....

Rafiki kwenye maisha yetu kuna vitu ambavyo vipo ndani ya uwezo wetu,vitu ambavyo tunaweza vikabili na kuvibadili vile tunavyotaka sisi, lakini vipo ambavyo hatuna uwezo wa kuvizuia au visiweze kutukuwepo au kuwepo, mfano hata kama hutaki mvua inyeshe huna uwezo wa kuizuia kutonyesha kwasababu huna uwezo nalo, habari njema ni kwamba kwenye fedha na utajiri ni wewe mwenyewe ndio unayejiwekea ukomo, na zipo kauli mbili ambazo zinatumiwa na watu ndio zinazoamua hatima zetu.

SIWEZI KUPATA/NITAPATAJE
Rafiki kama nilivyokushirikisha kutoka kwenye moja ya vitabu vinne ambavyo uchambuzi Wangu unaegemea zaidi ni kitabu cha RICH DAD,POOR DAD kwa utafiti aliofanya mwandishi unaonyesha kwamba masikini au watu wasio na kipato cha kutosheleza ni wepesi sana kutumia neno SIWEZI KUPATA,utasikia akisema siwezi kupata kiasi hicho kwani ni kikubwa sana, siwezi kuendesha gari,siwezi kuweka akiba, lakini watu waliofanikiwa hawatumii kauli hiyo kwani ni kauli inayoonyesha kukata tamaa na kutoushughulisha ubongo kufikiri, lakini wao hutumia kauli ya NITAPATAJE watu wengi walioshindwa neno nitapataje hulitumia pale wanapotaka matumizi ya anasa kwa fedha ambazo hawana, pengine hapo ndio hutumia neno nitapataje? Na kwa haraka ukimbilia kukopa na pindi akipata fedha hulipa deni na kukopa tena, lakini kama unataka kufanikiwa usijiambie SIWEZI KUPATA UTAJIRI Bali anza kufikiri NITAPATAJE UTAJIRI? hapo unaifanya akili ianze kufikiri kwa mapana na kuwaza ni nini ifanye kukupatia unachotaka, rafiki unaweza kuona hizi ni kauli ndogo zisizo na maana lakini nikuambie tu kwamba jikague kwenye kauli hizi na badilika Mara moja kwani huwezi fikia mafanikio ya juu kwa kuwa mwepesi kusema siwezi kwa mambo yanayowezekana.

Makala hii imeandikwa na Mwl.Kelvin Kinyaga
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944
Kinyagakelvin162@gmail.com


Saturday, 9 May 2020

Njia unaifahamu lakini hauko tayari kwenda...........



Rafiki yangu hongera kwa siku nyingine, shukrani nyingi sana kwa mwenyezi mungu kuendelea kutupa sababu ya kuishi, bilashaka yapo tunayopaswa kukamilisha ndio maana tunaendelea kuwa hai,karibu rafiki tuweze kushirikishana machache ili tuweze kupunguzia mateso yaliyo msingi wa maisha yetu.

1.UBONGO
Rafiki yangu pengine ulishawahi kujiuliza au kutaka watu wote wafanye yaliyo sahihi pekee wasikosee kwa lolote,hata wewe ulishawahi kutamani usikosee kwa lolote, uachane na Tabia mbaya usiyoipenda kwako mwenyewe hasa linapokuja swala la fedha, pengine ni kukopa na madeni yamekuchosha lakini huwezi toka na kuachana na madeni na unaendelea kukopa pamoja na matatizo unayopitia, ulishajiuliza ni kwanini? Basi zipo sababu nyingi lakini hebu tuangalie sababu mbili zinazotutesa wengi.

A.Kwasababu hutaki kuonekana umeshindwa; hapa unaweza usinielewe ni kwa vipi? Mara nyingi tunapojaribu vitu vipya tunaanza na kushindwa, pengine unafahamu kabisa njia ya kuongeza kipato ni biashara lakini kwakuwa biashara siyo kitu rahisi hivyo kwa kuangalia wanaoshindwa na wewe hutaki kujaribu, pengine umekuwa una mazoea ya kukutana na rafiki zako Kila mwisho wa wiki kwa ajiri ya starehe na sasa unahitaji kuachana na mwenendo huo ili ufanikiwe unaona kwamba watu watakuona umeishiwa ndio maana upo tayari kuridhisha wengine ila si kwa manufaa yako, sisi binadamu ni wepesi kutengeneza tabia lakini wagumu kuzivunja hata kama zinatuumiza.
B.Sababu ya pili ni kukosa kusudi;neno hili kusudi siyo mara yako ya kwanza kulisikia lakini chochote ambacho ipo kusudi ya kufanya lazima utakifanya, hebu angalia ni wangapi wapo tayari kufa kwasababu ya njaa? Hivyo sababu lipo kusudi la kwamba wanataka kuishi lazima wajitoe kupata chakula. Kwenye kitabu cha MAN'S SERCH FOR MEANING cha Viktor Frankly anasema zipo hatua za kufuata ili kutengeneza kusudi,Lazima uwe tayari kufanya njia za kibunifu kwani unapotaka kufanya kitu lazima ufahamu kuna kupingwa,kukataliwa, kukosolewa na kukatishwa tamaa hivyo kama huna ubunifu huwezi kuendelea, Lazima kuwe na kitu unachokijali sana,pengine ni familia yako, la mwisho lazima ukubali kuteseka kwani mateso ndio msingi wa maisha ya kusudi, hivyo huwezi pata unachotaka kirahisi. Chukulia mfano wa mtu anayejifunza kuendesha baiskeri, Je anaweza chukuwa baisker kwa mara ya kwanza na kuendesha bila kupitia kikwazo chochote? haijarishi utafahamu njia zote za kuendesha baiskeri lazima utakapoanza kujifunza utajaribu na kushindwa na kuanguka, utachekwa lakini utapambana mpaka uweze hivyo usiogope kujaribu vitu vipya kwasababu ya kushindwa, kataa mazoea na usihofu unapojaribu na kushindwa, ng'ang'ana mpaka upate unachotaka.

2.VITABU VINNE
A.THINK AND GROW RICH-Kimeandikwa na Napoleon Hill mwaka 1935,mwandishi ametumia zaidi ya miaka 25 na kugundua kwamba mafanikio yoyote yanaanza na wazo, malengo ya kulitimiza wazo hilo,kisha uvumilivu na shauku vitafanya ufikie kile unachohitaji,mwandishi anamtumia mtu mmoja ambaye anaitwa Edwin, hakuwa na chochote ila alikuwa na shauku ya kufanya kazi na mtu maarufu (Thomas Edison)mtu aliyegundua taa za Umeme, pamoja na kuwa hakuwa na chochote lakini shauku yake ilipelekea kuajiriwa na Thomas na mwisho wa siku kufanya nae kazi, Je wewe unayo shauku ya kitu gani? Je shauku yako imeambatana na uvumilivu gani?usifute wazo lako Bali badili mbinu za kulifikia wazo lako, tutendelea kukichambuwa kitabu hiki na utajifunza mengi.

B.THE RICHEST MAN IN BABYLON;Kitabu kimeandikwa na George S Clason; kitabu kiliandikwa mwaka 1920,wote tunafahamu historia ya mji wa babeli, mwandishi anasema kanuni za fedha ziliazia babeli na Leo duniani kote tunazitumia, kitabu hiki kimesomwa na matajiri wengi duniani na kupitia kitabu hiki watu wameweza kufikia mafanikio ya juu sana,mwandishi anaanza kwa kusema maendeleo ya mtu mmoja mmoja ndio yanaleta maendeleo ya taifa zima, wengi tunaamini taifa ndio linaendelea kisha watu wake ndio wanaendelea lakini hili siyo kweli, hebu tujiulize kupitia matajiri unao wafahamu wewe ni Kodi kiasi gani serikali inakusanya? Na kulipa wafanyakazi wake serikalini? Je matajiri hawa wameajiri watu wangapi? Je Kila mtu angefahamu mbinu za kuupata utajiri na kuzifuata taifa letu lingekuwa wapi? Mwandishi anasema hivi,"OUR ACTS CAN BE NO WISER THAN OUR THOUGHTS.OUR THIKING CAN BE NO WISER THAN OUR UNDERSTANDING" akiwa na maana kwamba matendo yetu hayawezi kuwa mazuri zaidi ya mawazo yetu. Mawazo yetu hayawezi kuwa mazuri zaidi ya uelewa wetu. Hapa tunaweza kuona namna muunganiko wa mawazo, matendo na uelewa unavyohitajika ili tuweze kufikia ndoto zetu.

C.RICH DAD,POOR DAD;Kimeandikwa na Robert Kiyosaki, kitabu hiki kinatupa elimu namna maisha halisia yalivyotofauti na yale tunayojifunza shuleni, mwandishi anatupa ufafanuzi kupitia baba zake wawili, ambapo baba zake hao wote wawili wanampa funzo la maisha, baba zake hawa wawili walifanana kwenye Kila kitu isipokuwa upande wa fedha, baba tajiri ambaye alisoma na kuishia darasa la nane na baba masikini alisoma na kufika ngazi ya juu ya elimu yaani PHD au shahada ya uzamivu, baba huyu msomi ndio alikuwa baba yake Mzazi na baba wa rafiki yake aliyeishia darasa la nane alikuwa tajiri, baba msomi aliamini fedha ndio chanzo cha matatizo wakati baba tajiri aliamini kutokuwa na fedha ndio chanzo cha matatizo, mmoja aliamini ukienda shule unapata kazi nzuri na baba tajiri aliamini ukienda shule ili uje kumiliki kampuni yako, Mmoja anaamini kuwa na watoto ndio sababu ya kuwa tajiri,wakati mwingine aliamini kuwa na watoto ndio sababu ya kutokuwa na utajiri, hivyo pamoja na sababu hizi kuwa kwenye kitabu hiki lakini hizi ndizo sababu zilizopo mtaani kwetu, wangapi wanajilaumu kutofanikiwa kwasababu ya kuwasomesha watoto? Sehemu inayofuata tutajifunza masomo sita aliyojifunza Robert kutoka kwa baba Tajiri.

D.ELIMU YA MSINGI KUHUSU FEDHA;Kilichaondikwa na Dr.Amani Makirita, kitabu hiki kimeanza na kutoa maana ya fedha, wengi tunahangaika kupata fedha lakini hatufahamu maana yake, ni Sawa na kutafuta mtu usiyemfahamu, lakini Leo kupitia kitabu hiki mwandishi anataka kufahamu maana ya fedha, Fedha ni Njia ya Kubadilishana Thamani, hivyo fahamu kwamba unalipwa kulingana na thamani unayotoa, kama thamani yako ni 500 utalipwa 500,huwezi kupokea zaidi ya unachotoa.

Rafiki nitakwenda nikigusia maeneo baadhi ya vitabu hivi lakini ukitaka kupata kwa kina yaliyopo kwenye vitabu hivi nunua na uvisome mwenyewe.

3.KOCHA
Kutoka kwenye tafakari ambazo nazipata Kila siku kutoka kwa kocha ipo moja inasomeka hivi, Ukitaka kuwa juu ya wengine basi kuwa chini yao, kauli hii inatufundisha unyenyekevu, kama unataka kuwa na nguvu dhidi ya wengine basi jifunze kuwanyenyekea, na ili kufahamu hili namna linavyofanya kazi angalia Bahari inavyojinyenyekeza kwa mito, bahari ipo chini na mito ipo juu, lakini mito yote hupeleka Maji yake baharini na baadaye bahari inakuwa na nguvu kuliko mito, hivyo kama unataka chochote basi kuwa mnyenyekevu.

4.POROJO(Je hatua wanazozichukuwa serikali yetu ni sahihi dhidi ya gonjwa hili?)
Wiki hii nilipokea meseji kutoka kwa rafiki yangu akinitaka nieleze nimelichukuliaje swala la Corona na hatua Serikali yetu inazozichukuwa? Rafiki hizi ndizo porojo zinazoendelea mtaani kwa sasa, sikuwa na jibu zaidi ya hili,Serikali ipo sahihi au haipo sahihi hili si muhimu sana bali Mimi mwinyewe hatua ninazozichukuwa dhidi ya Corona ni sahihi au siyo sahihi?watu wengi tunafahamu kama maamuzi ya wengine ni sahihi au siyo sahihi ila hatufahamu maamuzi yetu kama ni sahihi au siyo sahihi, hivyo achana kubishana na wengine bishana na wewe mwenyewe.

Rafiki makala hii imeletwa kwako na Mwl Kelvin Kinyaga, funguwa kiungo hiki https://kinyagakelvin.blogspot.com na utapata makala nyingi za mafunzo, pia unaweza wasiliana nami kupitia;
Email yangu: Kinyagakelvin162@gmail.com au number za simu 0763766944
Kwa pamoja tutafika,Asante sana tutakutana wiki ijayo.


Saturday, 2 May 2020

Ubongo(Akili)+Vitabu vinne+Kocha+Menta+Porojo vitakuvusha........



Habari za wakati huu mwanamafanikio mwenzangu, bilashaka unaendelea kuishi bila hofu kwasababu unafahamu hofu haina msaada wowote, lakini pia unajitaidi na vile vilivyo ndani ya uwezo wako ili kujikinga na janga linalotukabiri, karibu kwenye ukurasa huu tujifunze baadhi ya vitu ambavyo Nina amini ukivisoma na kuvifanyia kazi utayafikia mafanikio yoyote unayoyahitaji, karibu tuwe zote mpaka mwisho.......

AKILI
Rafiki unahitaji muunganiko wa vitu vingi ili uweze kufanikiwa, hakuna kitu kimoja ambacho mtu yeyote atakushauri ukifuate na ukafanikiwa, lakini haimaanishi basi Kila kitu utakachoambiwa ndio sahihi hivyo unahitaji akili timamu ya kuchuja yale unayoona na kuyasikia kuhusu mafanikio, kitu unachopaswa kufahamu ni kwamba akili haipatikani shuleni na hakuna shule ambayo inafundisha akili hivyo usihusianishe mafanikio uliyopata shule au kutofanya vizuri darasani ndio sababu ya kutofanikiwa, wapo watu wengi waliogundua vitu vikubwa bila ya kwenda shule, Abraham Lincoln, Harry Truman,George Bernard shaw mtu aliyeshinda tuzo ya Nobel aliacha shule akiwa na miaka 16,John Major aliyekuwa waziri Mkuu wa uingereza na wengine wengi wenye majina makubwa na wamefanya mengi wakati elimu zao ni za kawaida sana hivyo usitumie kigezo cha kutokwenda shule au kufanya vibaya kwenye masomo yako kama sababu ya kushindwa, shule ina mchango wake lakini siyo sababu ya kutofanikiwa, hivyo akili ni moja ya nyenzo muhimu kuwa nayo.

VITABU VINNE
Rafiki kama kweli unahitaji kufanikiwa ipo tabia ambayo lazima uwe nayo, tabia hiyo ni ya kusoma vitabu, kwenye vitabu kuna Kila mafanikio na utajiri unao hitaji, unaweza kuanza kuuliza mbona kuna vitabu vingi sana je nianze na vipi?,rafiki ni kweli kuna utitili wa vitabu vingi sana na usipokuwa makini unaweza usifahamu unataka nini kwenye vitabu, lakini vipo vitabu vinne ambavyo kocha wangu alinishauri ni lazima nivisome kama kweli nataka kufanikiwa, nimesoma vitabu vingi sana lakini vitabu hivi vinne Nina kuambia visome na ukivimaliza rudia Mara nyingi uwezavyo huku ukifanyia kazi yale unayo jifunza, vitabu hivyo ni THINK AND GROW RICH- humu utaona namna fikra zako zinavyochangia wewe kufanikiwa au kushindwa na kwanini kushindwa au kufanikiwa sababu ni wewe na siyo mtu yeyote yule,Kitabu cha pili ni THE RICHEST MAN IN A BABYLON-Hapa utapata historia ya mji wa babeli na mtu tajiri aliyesababisha babeli iwe na nguvu duniani wakati ni eneo lililokuwa jangwa, kuna matajiri wengi wamekuzunguka je ulishawauliza walifanya nini wakafika hapo? Basi kitabu hiki kitakupa Kila kitu kwenye safari yako ya matumaini, Kitabu cha tatu ni RICH DAD-POOR DAD-Hapa utakutana na baba wawili mmoja msomi sana lakini masikini na mwingine ana elimu ya kawaida lakini ni tajiri na kipi kilisababishwa na hayo yote na nini utajifunza kwa wababa hao, vitabu vyote hivyo juu vimeandikwa kwa kingereza, kama kingereza kwako ni tatizo karibu ujiunge na kisima cha maarifa utapata uchambuzi mzuri sana kwa lugha ya kiswahili, kitabu cha nne na cha mwisho ni kitabu kilichoandikwa na Mtanzania kinaitwa ELIMU YA MSINGI KUHUSU FEDHA-Kitabu hiki kimefanyiwa utafiti kwa kutumia nchi yetu ya Tanzania na kina Kila msingi muhimu wa fedha na kimeandikwa kwa mifano ya nchi yetu, wapi uweke fedha yako ili ikufanyie kazi na makosa yote unayofanya kwenye fedha, ukivisoma vitabu hivyo vinne na usifanikiwe baada ya kufuata yaliyopo humo nina neno nzuri la kukuambia, huna akili Timamu, rudia Mara tatu kujiambia sina akili timamu.

KOCHA
Rafiki nikisema kocha si maanishi uwe mchezaji wa mpira wa miguu ndio uwe na kocha, kocha ni mtu ambaye changamoto zako ni fursa kwake, mfano wewe una changamoto inayokusumbuwa unamshirikisha halafu bila kusita anakuambia ufanye nini ujikwamue na changamoto uliyo nayo, Lakini kuna mtu unamkosa kwenye maisha yako na mtu huyo siyo adui Bali rafiki atakayekuambia unakosea na kukukalipia unavyofanya kinyume na kile unachopaswa kufanya ili ufanikiwe, siyo rahisi kupata rafiki huyu ila ukimpata utakubaliana kwamba ni kiungo cha kukupeleka kwenye ndoto zako. Ukihitaji mtu wa namna hii tuwasiliane.

MENTA
Pamoja na kwamba tayari una Kocha, mtu ambaye atakusimamia kwa ujumla kwenye Kila kitu bado utahitaji mtu aliyebobea kwenye kile unachotaka kukifanya, pengine unataka kubobea kwenye kilimo basi tafuta menta wako kwenye kilimo ambaye ana uzoefu kwenye kilimo, biashara, sheria,fundi na mengine mengi, sifa ya menta mzuri lazima akue kwenye kile anachofanya siyo kukifanya kwa muda mrefu bali Kila siku anapiga hatua za juu kwenye kile anachofanya.

POROJO
Rafiki mwisho kabisa unachohitaji ni porojo za wengine, naweza nisieleweke kutumia neno porojo lakini usinielewe vibaya, baada ya kufuata yote yaliyopo hapo juu basi kuna mengine mengi utayasikia kwa watu wanao kuzunguka, huwezi,unajisumbua bure, unajitesa bila sababu, bahili na ushauri mwingi usio kuwa na tija lakini kwakuwa umeshafuata yale yote yaliyo hapo juu kwako utajuwa hayo unayoshauriwa ni porojo tu, sikuambii ukabishane na watu bali nakuambia ili ukikutana na mengine njee ya yote hapo juu au yanayokwenda kinyume uyapuuze na porojo zingine utazisikia na kuona ni msingi wa kile ulichojifunza na utakiongezea, kama hutofuata nilichokushauri Kila mtu atakuwa mshauri wako na utachanganyikiwa na hutofika popote.

HABARI NJEMA
1.Nitakuletea makala kutokana na akili nilizo nazo,vitabu hivyo vinne,kocha na porojo zilizopo ili ukae nazo mbali, Kila mwisho wa wiki utapata mkusanyiko wa mambo hayo.
2.Share na wengine andiko ili na jiandae kwa maandiko yanayofuata.
3.Endelea kutembelea blog yangu kwa kubonyeza kiungo hiki https://kinyagakelvin162.blogspot.com kuna makala nzuri kwa ajiri yako.

Makala hii imeandikwa na Kelvin Kinyaga, mwalimu na mwana kisima cha maarifa asiye na shaka yeyote ya kufanikiwa kwani ni muda tu ndio unasubiriwa. Wasiliana naye kwa No 0763766944 au email Kinyagakelvin162@gmail.com
Asante sana,hifadhi andiko hili na mtumie Kila anayekuomba ushauri, usinishukuru kwa andiko bali fanyia kazi yalipo kwenye andiko,nakupenda Daima.