Wednesday, 27 May 2020

Moto wa matumaini,Ujasiri na uvumilivu vitakuvusha....



Habari za wakati huu rafiki na ndugu yangu, ikiwa Leo ni siku nyingine siku ambayo itakupa ushindi mkubwa, haijarishi kuna vipingamizi gani lakini kwa kutoogopa na kuvikabiri Nina hakika utakuwa mshindi sana kwani ukiogopa changamoto zinakuzoea na kukuona dhaifu hivyo Kila siku zitakuandama,karibu tuwe sote mpaka mwisho......

Rafiki kitu kikubwa unachopaswa kukifahamu ni kwamba;
"ALL ACHIEVEMENT, ALL EARNED RICHES,HAVE THEIR BEGINNING IN AN IDEA''

Magorofa na vitu vyote vizuri unavyovitamani vilianza kama wazo kwa mtu, na hata wewe hapo ulipo ni matokeo ya mawazo uliyowahi kufanya huko nyuma, hivyo kama mawazo hayo yanakuletea matatizo Leo basi Jaribu kuwaza tofauti ili kesho yako iwe kesho yenye matumaini makubwa. Wiki iliyopita tuliangalia hatua sita za kufuata ili uweze kufikia utajiri, kama hukuziandika ziandike na anza kuzifanyia kazi. Kutoka kwenye kitabu cha THINK AND GROW RICH Leo tutaangalia mambo matatu makubwa unayotakiwa kuyaishi ili kufika safari ngumu na yenye vikwazo vingi ya mafanikio.

"KNOW WHAT YOU WANT AND THE DETERMINATION TO STAND BY THAT DESIRE UNTIL YOU REALIZED IT"

Safari yoyote ya mafanikio inataka ufahamu hitaji lako, nini hasa unataka kweli, kisha kuwa na shauku ya dhati ya kupata unachotaka, wengi wanahitaji mafanikio lakini wanakosa shauku ya kuipata fedha, lakini hata wenye vitu hivi vyote viwili bado utahitaji vitu vitatu kufikia ndoto zako.

MOTO WA MATUMAINI
Leo tulio wengi tunafahamu umuhimu wa fedha lakini hatuna ujasiri wa kusimama na kusema tumejitoa, kuweka kazi kweli na kuhakikisha tunaupata utajiri na kupafanya dunia kuwa sehemu bora kuishi kwetu na kwa wanao tuzunguka.

UJASIRI
Watu wengi wamezoea kufanya vitu vya kawaida na wanafikiri Kila mtu anapaswa kufanya kama wao, hivyo ukikosa ujasiri wa kusimama kweli lazima wakutoe kwenye ramani ya kule unakotaka kufika.

UVUMILIVU
Safari ya mafanikio siyo lelemama na ndio maana ni wachache ndio wamefanikiwa, wewe kazi yako ni kuweka bidii na muda mrefu huku ukikabiliana na changamoto, lakini usitarajie matokeo ya haraka, furahia unapoweka bidii zaidi na unaposhindwa badili njia lakini usikate tamaa kwa safari yako.

Hayo ndio mambo matatu unayopaswa kuyafahamu, kwenye kitabu hiki ipo Hadithi ya mtu mmoja ambaye alifahamu uwepo wa madini kwenye eneo lake, lakini baada ya kuchimba kwa muda mrefu bila kupata madini aliamuwa kupauza kwa mtu mwingine na yule aliyepanunua alipoendelea kuchimba baada ya yule mtu wa kwanza kushindwa baada ya Futi tatu tu akayakuta madini mengi sana, Hivi ndivyo tunavyoyaishi maisha yetu, tunapambana lakini tunapokuwa tumebakiza safari kidogo kufikia kule tunakotaka kufika tunakata tamaa na kuacha na kuanza kitu kingine na mambo yanakuwa yale yale.

Kipo ulichoondoka nacho rafiki yangu, weka kazi kweli, Ujasiri ndio nguzo yako na uvumilivu utakupa unachotaka kwani maisha siyo magumu ila kuna watu ni dhaifu kuliko maisha. Asante sana ndugu.

Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944

Bonyeza hapa chini;

https://kinyagakelvin.blogspot.com

Utapata mafunzo mengi yatakayokusaidia kwenye maisha yako.


No comments:

Post a Comment