Sunday, 31 May 2020
Nzi na nyuki wote wanajituma.........
Rafiki yangu hongera kwa kuweza kuifikia jumapili hii ya Leo, siku ambayo unapaswa kujipima ulipanga kufanya nini kwenye wiki hii, umefikia wapi na Je mpango wako wa mwezi umekamilika kama ulivyopanga? Je unajipangia yapi ambayo mwisho wa mwezi wa Juni utajipima tena? Kama unafanya hivyo hongera ila kama Kila siku unaishi bila ya kujipima na kujifanyia tathimini hata bidii kwenye kile unachofanya ni kazi bure na hapa chini utafahamu kama wewe ni nyuki au nzi.......
Miaka kadhaa iliyopita nilimsikiliza mwandishi mmoja akielezea utofauti wa maisha ya nzi na nyuki,bilashaka ulishawahi kuona Sega la Asari,unaweza kuona jinsi nyuki anavyopata matokeo baada ya jitiada za muda mrefu na mwisho wa siku tunapata Asari tamu kweli.
Upande wa pili tunamwangalia Nzi, ukiona anavyoruka kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine unaona naye anajishughulisha lakini hata kama siyo kwetu bado matokeo anayozalisha nzi ni kwa manufaa yake na viumbe wengine labda wanao mla lakini hakuna cha maana kutoka kwa nzi.
Maisha ya wadudu hawa ni Sawa na maisha yetu, kama Kila siku unaishi bora kumekucha na hakuna mipango yeyote uliyojiwekea na Kila baada ya muda unajipima kuyaendea basi maisha yako ni Sawa na Nzi na hakuna chochote unachozalisha labda faida ni kwa boss wako pekee ambaye anakufanya uwe busy kwa malipo kidogo ya kukufanya uendelee tu kuishi, tafakari na chukuwa hatua.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944/0712161251
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment