Monday, 1 June 2020
Huyu ndiye mwalimu bora kuliko wote.......
Nakusalimu rafiki yangu, wanaweza kukuzurumu Kila kitu lakini siyo namna unavyoweza kufikiri, hivyo kama una ubongo hapo ulipo na afya basi huna sababu yeyote ya kuwa na hofu kwani kama aliyekuumba ameendelea kukupa vitu hivyo hakuna atakayekuny'ang'a bali ni jukumu lako kuvitumia ipasavyo.
Rafiki yangu kujifunza ni hitaji muhimu sana kwa binadamu na ndio maana kuna shule, wote tunafahamu jinsi ambavyo shuleni tunafundishwa,nadharia halafu tunafanya mtihani kisha tunapewa cheti halafu tunakwenda kazini.
Kuna namna zingine ambazo tunajifunza kwa makosa yetu wenyewe (ujinga) na kuna namna ambayo tunajifunza kupitia makosa ya wengine (uelevu).Pamoja na namna zote hizo za kujifunza yupo mwalimu bora sana ambaye tunapaswa kumfahamu ambaye unapaswa kumfahamu.
MAISHA
Huyu ndiye mwalimu sahihi sana, hebu jiulize maisha angekuwa anakusemesha au mnaweza kuongea naye si ungeweza kumgombeza sana pale mambo yako yanavyokwenda kinyume na matakwa yako? Wengine wangeweza kumshitaki maisha mahakamani kama angekuwa ni binadamu kwamba yamekuwa yakiwadhurumu na yanawapendelea wengine, lakini hilo haliwezekaniki.
Kwenye kitabu cha RICH DAD,POOR DAD tulianza kuona namna Robert na Mike walivyohitaji kuwa matajiri na wenye uwezo wa kutengeneza fedha, wanaamuwa kwenda kumuomba baba yake na Mike awafundishe jinsi ya kutengeneza fedha, wanapofika pale baba yake Mike anawakubalia lakini anawaambia hatowafundisha kwa namna wanavyofundishwa darasani, watakuwa wanakwenda kufanya kazi Kila jumamosi kwenye kampuni yake na atawalipa fedha kidogo kisha atawafundisha, walikubali na wakawa wanafanya kazi ya usafi na kupanga file za ofisi, siku zilizidi kwenda lakini baba yake na Mike hakuwafundisha, kitendo hicho kilimkasirisha sana Robert kwamba baba yake Mike ni mnyonyaji amekuwa hawajali kabisa wafanyakazi wake na kuwalipa kidogo, lakini alikubaliana nao kuwafundisha ila amekuwa hafanyi hivyo bali kuwatumikisha.
Baadaye baba yake Mike anakutana na Robert pamoja na Mike na Robert anaeleza kwamba anaomba waongezewe mshahara na atimize ahadi yake ya kuwafundisha kama sivyo anaacha kazi, ndipo baba yake Mike anamjibu mbona nimekuwa nawafundisha? Na je maana ya kufudisha ni kuwa nadharia kama mnavyofundishwa shuleni? Hivyo sivyo maisha yatakavyowafundisha, maisha hayana muda wa kuongea na nyie na kuwabembeleza yenyewe yanawasukuma tu,na hiyo ndio elimu halisia.
"Now I know I can choose a profession for the work I want to perform and not because of job security, benefit or how much I get paid"
Hili ni somo ambalo lipo kwenye kitabu hiki, tunafanya kazi ili tujuwe namna ya kazi hiyo inavyoendeshwa,siyo kwa ajiri ya usalama au kiasi gani unalipwa ila uzoefu utakaoupata na namna gani unakwenda kuutumia kwenye maisha yako.
Je wewe umeajiriwa kwenye biashara ya mtu? Unajifunza nini ili uende ukakitumie kwenye biashara yako baadaye ndio muhimu hapo na siyo unalipwa nini, wewe ni mwajiriwa kama mwalimu? Unajifunza namna zipi za kusimamia na kuendesha shule ili uje kufunguwa shule yako ndio muhimu na siyo unalipwa nini, bilashaka umeondoka na kitu hapa, asante na uwe na siku njema.
Kinyagakelvin162@gmail.com
My blog;
https://kinyagakelvin.blogspot.com
Hapo utajifunza masomo mengi zaidi.
0763766944/0712161251
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment