Sunday, 28 June 2020
Tatizo alipo kwenye unachokipokea bali unachokinunua.
Habari za wakati huu rafiki yangu, bilashaka u mzima na buheri wa afya, umeianza wiki hii kwa nguvu na umeshapanga ni nini unakwenda kukamilisha kwenye siku hii, haijalishi nini kitakwenda kutokea ila hutojipa sababu kwanini usifanye bali kwenda kutekeleza yote uliyopanga.
Kama ilivyo utaratibu wetu siku hii ya Leo ya Jumatatu kwa wiki kadhaa sasa tunachambuwa kitabu cha Rich dad poor dad,tangu tumeanza kujifunza tumeona nini tunatakiwa kufahamu kupitia baba hawa wawili, maana hatujifunzi kwa kuwaangalia matajiri wanafanya nini pekee bali kutofanya kile ambacho masikini wanafanya.
Leo tuangalie dhana ya kununua inavyotutenganisha na utajiri, ni kawaida kwetu kuona tunakuwa masikini kwasababu kipato tulichonacho ni kidogo na pale tunapoongezewa kipato iwe kwa kuweka bidii au kulipwa na waajiri wetu bado gharama za maisha zinaongezeka na kuwa kubwa, sasa hapa ndipo pale wanaoshinda bahati nasibu au kuachiwa urithi wa fedha nyingi na utajiri huwa hawaelewi nini kinasababisha fedha zao au utajiri wao kupotea.
Moja ya tofauti kubwa kati ya masikini na tajiri ni kwenye manunuzi, masikini ananunua Mali zisizo zalisha(liabilities) wakati matajiri hununua Mali zinazo zalisha (Assets), Leo ukienda kuongea na mtu mwenye mawazo ya kitajiri utamsikia akiwaza kununua vitu vitakavyomuingizia kipato, biashara au kuwekeza fedha kwenye sehemu ambayo na yeye atanufaika, lakini masikini muda wote huwaza kununua anasa na kufanya starehe, vitu vinavyo vutia machoni na havimuingizii pesa yoyote ile.
Mwandishi anafananisha kutengeneza mali zinazozalisha ili kustaafu ni Sawa na kupanda mti, mwanzo utaupa huduma zote na kuumwagilia na baadaye ukiwa mkubwa na mizizi yake kwenda chini hufikia Maji na kuto hitaji huduma kitoka kwako bali kukupatia kivuli au matunda.
Mwaka 1990 Mike alichukuwa urithi kutoka kwa baba yake (baba tajiri) na aliweza kuzisimamia vizuri na utajiri wao ukakua Mara dufu, huku mwaka 1994 Robert akiwa na miaka 47 na mke wake mwenye umri wa miaka 37 waliamua kustafu na kuendelea kula utajiri wao, na hapa Robert anatupatia dhana ya kustafu kwamba siyo kuacha kufanya kazi moja kwa moja bali kutokuifanya au kufanya hakuzuii fedha kuongezeka, hapa unakuwa umefikia hatua fedha inakufanyia wewe kazi kwa uwekezaji uliofanya huko nyuma.
Lazima Mimi na wewe tuanze kufikiri ni lini tutahitaji kuwa tumefikia hatua ya kustafu na fedha zikitufanyia kazi, kwani nguvu ulizo nazo sasa hazitakuwa Sawa na nguvu utakazo kuwa nazo miaka 10 au 20 ijayo hivyo maandalizi ya kufika huko anza kuyafanya sasa.
Asante sana rafiki nina imani unakwenda kufanyia kazi haya uliyojifunza Leo, uwe na siku njema.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944/0712161251
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment