Tuesday, 23 June 2020

Hizi hapa hatua tatu za kufuata ili kukamilisha mpango na malengo yako ya kifedha........


Leo kabla hujaendelea kusoma hapa jiulize ni lipi katika niliyojifunza kwenye Ustawi wa fikra nililifanyia kazi? Kisha ukanishirikisha inbox na kama hufanyi hivyo Kila siku unajiambia masomo mazuri nitaanza mipango kamili siku zijazo, hapo unajidanganya mwenyewe kitu ambacho hakitamuumiza yeyote isipokuwa wewe mwenyewe, siwezi kaa chini nikaandika kitu ambacho sina hakika kwamba kitakusaidia,nina hakika ukifanyia kazi masomo haya tutafika pamoja kule tunakotaka kufika......

Leo tunaendelea na uchambuzi wa kitabu chetu cha THINK AND GROW RICH,baada ya wiki iliyopita kuona namna akili yetu ilivyogawanyika na kufanya kazi,wiki hii tutaona hatua tatu za kufuata ili lengo lako ulilojiwekea liweze kutimia, watu wanafanya kazi na kulipwa au biashara lakini miaka yote mipango yao kifedha hahifikiwi kwasababu wanaishi kutamani pasipo na mpango madhubuti wa kuyafikia yale unayotamani na ndio maana wengi wanaingia kwenye mtego wa madeni kwa kufikiri hiyo ndio njia pekee ya kukamilisha mipango yao. Hapa chini nakuandikia hatua tatu unazopaswa kuzifuata ili mpango ulio nao uweze kukamilika.

HATUA YA KWANZA
Taja kiasi cha fedha unachohitaji,taja tarehe ya mwisho ya wewe kupata kiasi hicho na bidhaa au huduma unayotakiwa kutoa ili kupata kiasi hicho. Wakati unasema hivyo na kuweka mpango huo jione tayari unamiliki kiasi hicho.Hapa chini nakuwekea mfano wa hatua hii.

Mpaka kufikia June 1,mwaka 2021 nitakuwa nimepata Tsh 1095000 ambazo zitatokana na biashara ya Visheti.Nitahakikisha natoa huduma nzuri kwa wateja ili niweze kupata zaidi ya Tsh 3000 kwa siku kama faida. Nina amini nitakuwa nazimiliki fedha hizi. Imani yangu ina niambia tayari nimeshazipata fedha hizi, kwani tayari ninao mpango ninao ufuata na nina uhakika wa kupata fedha hizo muda huo utakapofika. Kama unavyanzo Vingi vya mapato basi Kila chanzo unakiwekea mpango wake na baadaye unaweka mpango wa majumuisho.Hili linategemeana na uwezo wa chanzo chako cha mapato kama ni cha siku, mwezi, miezi sita au mwaka.

HATUA YA PILI
Rudia Maelezo hayo asubuhi na jioni mpaka ile sehemu ya ubongo wa ndani (subconscious mind)iweze kuona kama ndio kitu kinachotokea kwenye maisha yako.

HATUA YA TATU
Weka nakala ya Maelezo yako haya sehemu ambayo unaweza kuyaona asubuhi na usiku na isome kabla ya kulala na pale unapoamka, Kila siku mpaka tarehe uliyojiwekea inapofika bila kuacha hata siku moja.

Mwanzo akili yako itaanza kupingana na hatua hizi na utaanza kuhisi kuzipuuzia lakini ukiweka ung'ang'anizi wa kuto kubali kurudi nyuma nina hakika wa zaidi ya asilimia tisini unakwenda kutimiza lengo lako ulilo jiwekea, lakini kama unajiambia unahitaji kiasi fulani cha fedha bila ya kufuata hatua hizo basi utakuwa unaishi kutamani na huwezi kutimiza malengo yako.

Unaweza ona Kila mwanzo Mwa mwaka watu wakifurahia mwaka mpya na kuweka mipango mizuri ila kabla ya kufika mwezi march zaidi ya asilimia 80 wanakuwa wamesharudi kwenye maisha yale yale ya Kila siku.

Rafiki yangu nenda kaweke mipango yako kifedha kwa namna hii na kama utafanya hivyo utaona nguvu itakayokusukuma na utapiga hatua Kila siku, haitakuwa rahisi lakini ukijiwekea ung'ang'anizi sina shaka utapata matokeo mazuri sana.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment