Wednesday, 17 June 2020
Thamani ya kitu hupimwa kwenye vitu hivi vitatu......
Habari za wakati huu rafiki, hongera kwa siku hii nzuri, siku ambayo unakwenda kufanya zaidi ya Jana, naomba tuungane pamoja tuweze kuona ni vitu gani vinafanya kitu kingine kiwe na thamani kubwa na kingine kiwe na thamani ndogo?kama ni mfanyakazi au mfanyabiashara hapa ndipo patafanya watu wakulipe zaidi......
Baada ya wiki iliyopita kuweza kuona aina za vipato na kutambuwa ni aina gani inaweza kukupa utajiri basi wiki hii tuangalie misingi mitatu inayoamua thamani ya kitu unachofanya. JE KWANINI WATU WAKULIPE ZAIDI?
1.Uhitaji wa kile unachokifanya.
Rafiki kama unafanya kitu ambacho Kila mtu anakihitaji kweli basi thamani ya kitu hicho inakuwa kubwa, unaweza kuona malimao yalivyopanda bei msimu huu wa korona ni kwasababu Kila mtu aliaminishwa kwamba yanaweza kupunguza madhara ya kusambaa mwilini kwa ugonjwa huo.Hivyo kama huduma unayotoa si watu wengi wanahitaji basi hapo thamani yake inakuwa ndogo pia.
2.Upatikanaji wa wanaoweza kukifanya.
Kama kile unachofanya wapo wengi waliopo tayari kukifanya kitu hicho basi thamani yake inakuwa ndogo, hapa ndipo watu huona vingine vikithaminiwa zaidi ya vingine, Leo wewe ukiwa na digrii ya elimu na mwingine akawa na digrii ya urubani huhitaji kufahamu nani atalipwa zaidi hivyo hapo si kwamba mwalimu hana umuhimu lakini ni wangapi wako tayari kusomea urubani na wangapi wapo tayari kusomea ualimu? Hivyo kama Kila mtu yupo tayari kufanya unachofanya basi tambuwa hapo thamani yake ni ya chini.
3.Namna unavyokifanya kitu hicho.
Hapa mwandishi ametolea mfano wa makazini mfano hospitalini, unakuta Kila mtu akienda hospitalini anasema anataka kutibiwa na daktari fulani, ina maana hapo daktari huyo anayafanya tofauti na wengine na siyo kitu kingine, hivyo kama kitu unakifanya kawaida basi tumbuwa thamani yake inakuwa ndogo.
Rafiki ifahamu misingi hii mitatu na itumie kutengeneza thamani zaidi itakayotengeneza kipato zaidi, jiambie kuanzia sasa nitafanya kitu chenye uhitaji kwa wengi, kitu ambacho wengine hawapo tayari kufanya na nitakifanya kwa viwango vya juu sana kiasi kwamba Kila mtu atavutiwa na kukiona kina thamani ya juu sana na kuwa tayari kulipa zaidi.
Hapo umeshaona ni wapi unakosea kwenye kazi, biashara na Kila kitu unachofanya na sasa anza kubadilika taratibu kwa kujiwekea thamani zaidi. Asante tuonane wiki ijayo siku kama hii tutaendelea kupata chambuzi kutoka kitabu cha ELIMU YA MSINGI KUHUSU FEDHA,kujipatia nakala yako naomba tuwasiliane ni kitabu ambacho hakipaswi kukosekana kwenye shelvu yako ya vitabu.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944/0712161251
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment