Thursday, 18 June 2020

Kama mahitaji muhimu kwetu ni rahisi na yapo tele kwanini tunateseka?.......


Rafiki mungu alipoumba ulimwengu huu kabla ya kutuumba sisi binadamu alihakikisha mahitaji yote muhimu na ya msingi tunayapata kirahisi kabisa, na hapa ndio maana tuna amini kwamba dunia haijapungukiwa na chochote, Kila kitu kipo tele na kinapatikana kwa wingi, pamoja na yote hayo na dunia kua na utele bado binadamu tunateseka je kwanini? Hebu tuone mahitaji ya binadamu ya msingi ni yapi na utakubaliana na Mimi kwamba dunia inao utele.....

1.Hewa
Kupumua ni hitaji la binadamu, na ili tuweze kupumua vizuri tunahitaji hewa safi,je mungu alipo umba ulimwengu hukuweka hewa ya kutosha? Bilashaka ni hapana hewa ipo ya kutosha lakini watu kwa kuharibu mazingira na kukata miti, kuchoma misitu na kukua kwa sayansi na tekinolojia pamoja na viwanda tumeharibu mazingira yetu na magonjwa mengi kuibuka, na takwimu zinaonyesha vifo vingi hutokana na uharibifu wa mazingira. Pamoja na hatari hizo bado tunayo nafasi ya kurekebisha hilo kwa kuendelea kuyatunza mazingira yetu.

2.Chakula
Rafiki kwa asili sote tunakumbuka kwamba hapo kale binadamu hakua na nyenzo bora kama sasa, tunaweza kuona alitembea na kuokoteza matunda, baadaye aligundua moto na uwindaji ukafanyika,akaanza kula nyama ambayo ilibanikwa kwenye moto, baadaye akagundua kilimo,nakumbuka kijijini kwetu matunda yalitapakaa Kila eneo, lakini kwasababu ya uharibifu wetu tumepoteza vitu vyetu vya asili, Leo ukienda kijijini miti ya matunda imeharibiwa, ardhi yetu ilikua nzuri na yenye rutuba lakini Leo ugunduzi unatuambia tutumie mbolea, pamoja na kwamba tumeharibu ardhi zetu kwa kemikali lakini uharibifu ni mkubwa na vyakula vinaenda vikipungua, watu tumeacha kufuga wote tunataka kununua,je tutashindwa kuteseka?

3.Maji
Asilimia kubwa kwenye dunia tunayoishi tumezungukwa na Maji, Maji yapo ya kutosha lakini kwasababu ya uharibifu wetu tumeharibu na kuchafua vyanzo hivyo vya Maji na hivyo karne ya sasa huwezi enda mtoni na kunywa Maji kisha ukabaki salama, hata hivyo kutokana na akili na utashi wa binadamu bado tunaweza kupata Maji safi na salama.

Hayo ndio tunayoambiwa kwamba ni mahitaji muhimu, swali la kujiuliza ni kipi hapo ambacho hakihitaji fedha? Ukiondoa Hewa vingine vyote vinahitaji fedha ili uweze kuvipata na hata hewa kwa uharibifu wetu umefanya tuvute hewa chafu na kupata maradhi ambayo yatafanya twende hospitali ambapo bila fedha hatuwezi tibiwa, hivyo fedha ni hitaji kubwa ambalo kwa karne ya sasa tunalihitaji baada ya hewa ni fedha? Je fedha zina upungufu?

Kama fedha imekua muhimu kwetu basi amini hakuna upungufu wa kitu hicho, Leo tumeacha kufuga, nyumba zetu zimepambwa maua badala ya kulimwa mboga, miti ya matunda ni ya kutafuta, hakuna anayetaka kujishughulisha na kilimo, fedha zetu tunazozitafuta kwa shida zinapotelea huku na inafika sehemu tunamlaumu mungu kwamba ametuacha hatuna kitu, hebu tujifanyie tathimini upya kuna mahali tunakosea na hatutaki kulikubali hilo.

Asante sana rafiki nikutakie kazi njema, kwani huyu ndie rafiki wetu wa kweli tusikubali kukaa tu, kama ni mfanya kazi tumie siku za mapumziko kujishughulisha na kama tutakuwa na chakula cha kutosha Nina hakika hata matumizi mengine ya ziada tutayapata kirahisi tumekuwa wavivu na tegemezi sana ndio maana tunateseka.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment