Friday, 5 June 2020

Hizi ndizo zawadi za thamani unazopaswa kuzitumia ipasavyo na kuzitunza.........



Rafiki yangu ulishawahi kuwaza kwamba kuna siku unaweza pata ajari na ukavunjika mikono yote miwili,umeshawahi kuwaza kwamba kuna siku unaweza kuamka ukajikuta ni kipofu? Je vipi kama kuna kansa inaendelea kukutafuna taratibu lakini hujaitambuwa bado? Rafiki lengo langu siyo kukutisha kwani vitu hivi vinaweza mkuta yeyote, swali unalopaswa kulifikiria ni je mikono niliyopewa bure, macho na afya kwa ujumla navitumiaje?......

Leo rafiki nitakuambia Zawadi nne zenye thamani kubwa ambazo unapaswa kuzitambuwa na kuzitumia ipasavyo, Zawadi hizi zimeandikwa kwenye kitabu cha Robert kiyosaki cha BE RICH AND HAPPY na ukishazifahamu nenda kuziishi na kuzitumia ipasavyo.

1.Afya(Health);
Hii ni Zawadi kubwa unayopaswa kuitunza kweli kweli, afya ya roho, mwili na akili ni hitaji muhimu sana kwa maisha, hakikisha mwili wako unaufanyisha mazoezi kwani Maji yaliyotulia ni mfu na mwili usio na mazoezi ni mwili wenye magonjwa,hakikisha roho yako imeshiba kweli kweli amini kuna mungu na tenda yale yanayo mpendeza, mwili wako ndio nyumba ya akili na roho hivyo utunze sana, usiruhusu uchafu kuingia mwilini mwako na unakula vyakula na lishe bora, mwili wako unapaswa kupumzishwa, yote unayoyaangaikia sasa ni kazi bure kama Afya yako itatetereka, kuna watu hata ukiwapelekea mamilion ya fedha kwao ni kazi bure kwani afya zao zimetetereka hawajuwi wafanye nini.

2.Mahusiano
Unaweza ona  mahusiano yako na wengine ni kitu cha kawaida, ndoa yako kama umeoa au kuolewa, Wazazi, ndugu jamaa na marafiki zako wa kweli ni watu ambavyo ni wa thamani sana, kuna wengi walifika mbali sana lakini walipojaribu kupuuza watu wao wa karibu walipata mahangaiko makubwa sana, hivyo kuwa mwema kwao na usipuuze neno mahusiano ni Zawadi ya muhimu sana.

3.Kuheshimu watu wenye mafanikio
Hapa mwandishi anasema hivi

"I have found that what I hate in others I become and what I love in others I become"

Hakuna mtu asiyehitaji mafanikio na huwezi kupata mafanikio kwa kuwachukia waliofanikiwa, ninaweza kukuambia hili kwa namna pana sana lakini amini matajiri wanapenda sana watu waliofanikiwa na na kama unaona matajiri ni watu wabaya basi ninakuambia utakuwa masikini maisha yako yote kwani kile unachokichukia ndio ulichonacho, kama unamchukia mtu ina maana chuki ipo ndani mwako, basi kuanzia sasa tambuwa waliofanikiwa ni Zawadi kubwa sana kwako, huna gari lakini unasafiri, siyo daktari lakini ukiumwa unatibiwa, huna kiwanda cha nguo lakini unavaa nguo, hivyo heshimu waliofanikiwa na ona ni watu wanakufanya wewe uwe hivyo ulivyo na pambana ili uwe upande wa waliofanikiwa.

4.Kila siku yako moja ni Zawadi kubwa sana kwako.
Tatizo letu sisi binadamu kubwa ni mazoea, kwakuwa leo umeamka salama unajihakikishia kwamba na kesho utaamka salama lakini hilo siyo sahihi kabisa, Kila kunapokucha ona ni bahati ya pekee sana na itumie kwa kufanya yaliyo sahihi pekee, hivi unafahamu 80% ya mambo unayofanya hayana mchango wowote kwenye mafanikio yako? Ni asilimia 20% pekee ndio vitu vya maana, muda unaoangalia TV, kusema wengine na ushabiki usio na maana ni vitu visivyo na maana kabisa kwako.

Hizo ndizo Zawadi za kipekee kwenye maisha yako yote, zitunze sana kwani Kila siku yako moja mbele inapunguza siku zako za wewe kuwa hapa duniani, sambaza upendo kwa Kila mtu Kila siku, asante sana na nikutakie siku njema rafiki.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment