Friday, 12 June 2020
Kabla hujalaumu kwa lolote jiulize maswali haya mawili........
Nafahamu swala la bajeti linaendelea hapo ulipo,sielewi mnajadili nini lakini hiyo ni bajeti ya nchi,vipi yako?je ipo tayari? Pamoja na yote mtakayojadili kumbukeni bajeti ya nchi ina gawanyika sehemu mbili matumizi ya kawaida na matumizi ya maendeleo je wewe yako ina matumizi ya kawaida pekee au na bajeti ya maendeleo umeweka? Hayo ndio yatakua na umuhimu kwako mengine yote hapo ni kelele tu .........
Rafiki yangu sisi binadamu ni viumbe ambao ni wepesi sana kulalamika, vipo vitu vingi ambavyo tunaona tuna haki kulalamika, kabla sijafahamu hasara za kulalamika sikuwahi kufahamu ni kwa namna gani najichelewesha kwa kulalamika, kuna siku nilimuuliza rafiki yangu anitajie faida za kulalamika na aliponitajia ndipo nikagundua kuna sehemu kuna shida kwenye kulalamika kwetu,kwenye kitabu cha Be rich and happy mwandishi ametupa sababu mbili zinazofanya tulalamike na sababu hizi zimefanya niwe najiuliza maswali mawili kabla sijalaumu kwa kitu chochote, naomba na wewe ujifunze na kujiuliza maswali haya.
1.Ujinga Wangu uko wapi kwenye hili ninalolalamikia?
Mwandishi anasema sababu moja wapo inayofanya watu walalamike ni ujinga walio nao wa kushindwa kufahamu ufumbuzi sahihi wa matatizo yao, unalalamikia bosi wako, wateja wako kwenye biashara, serikali, ndugu na hata Wazazi kwasababu ya ujinga wako, mtu mmoja amewahi kusema mke wangu amebadilika sana na sielewi kwa nini?angejiuliza swali la ujinga Wake uko wapi asingelalamika kwetu,kwanza angefahamu ujinga wake ni kujaribu kulalamika kwetu kuhusu mke wake, mbili angefahamu kwamba watu hawabadiliki ila wanatoa makucha yao baada ya kujaribu kuficha kwa muda mrefu, tatu wakati anaoa alifanya maamuzi peke yake je anavyoshirikisha wengine huo si ujinga? Hivyo jiambie siku zote Mimi ni mjinga ndio maana na lalamika na si vinginevyo.
2.Nina danganya nini kwenye hili ninalotaka kulalamikia?
Sababu zote unazojipa kwamba ni za msingi na ni haki yako kulalamika basi tambua kwamba zote ni za uongo na sababu za kweli zitakazofanya uchukue hatua sahihi hutaki kuzisema kwasababu zina kugusa mwenyewe, unalalamika kwamba serikali haijakupa nafasi ya kazi na umesoma?basi huo ni uongo kwasababu zipo sababu zingine za kwamba hutaki kuonekana wa chini na kujishughulisha na chochote cha kukuingizia kipato, unalalamika kipato ni kidogo na bosi wako ndio tatizo kwani hakulipi vizuri, huo wote ni uongo na ukweli unaukwepa kwasababu unakuhusu wewe kwani umezoea kuishi kwa mazoea na hutaki kubadilika.
Hebu jiulize wale wa piga picha walio tupiga picha na kusubiria zikasafishwe mwanzo walisema nini sababu ya biashara zao kua mbaya? Ulishawahi jiuliza simu za motolora, Nokia, Philips na zingine nyingi zilizotoka kama matoleo ya mwanzo wangeendelea kukomaa na aina ile ya simu vipi wasingesema biashara ni mbaya kwa kisingizio cha uchumi?Hebu acha kuwaza mawazo yaleyale kwa kutegemea matokeo tofauti, usilaumu biashara zimekua ngumu kwasababu yoyote ile bali jiulize mwenyewe UJINGA WANGU UKO WAPI?NI LIPI NATAKA KUJIDANGANYA MWENYEWE? baada ya kujipa maswali hayo utagundua ujinga wako wote na uongo unaotaka kuaminisha wengine na kupata majibu sahihi ya kusonga mbele. Acha kulalamika chukua hatua.Ukichaa ni matokeo ya kujaribu kukwepa majukumu yako, tuendelee kuwa pamoja,nakupenda daima.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944/0712161251
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment