Sunday, 21 June 2020

Anza kujitawala kwanza ........



Habari za wakati huu rafiki yangu, ni jumapili nyingine inayotupa tafsiri kwamba wiki nyingine imeondoka, amini kwenye wiki hii wapo wengi ambao wamepitia changamoto kubwa kuliko unazopitia na hawajakata tamaa na wameendelea kusonga mbele je kwanini wewe ujiambie haiwezekani?Hebu Leo badilisha mbinu na jiandae kupeleka mashambulizi upya kwenye changamoto unazopitia, ukimshirikisha mungu na kuweka bidii hakutakuwa na wa kukuzuia........

Leo tunaendelea kubaki na falsafa, na Leo tutaangalia nukuu kutoka kwa mwanafalsafa ZENO anayetuambia "Man conquers the world by conquering himself" Hapa tunapata funzo kubwa kwamba huwezi kuitawala dunia kama umeshindwa kujitawala mwenyewe.

Huwa tunapenda kuwa viongozi bora tuweze kuongoza wengine, lakini huwezi kuongoza yoyote kama huwezi kujiongoza mwenyewe, kama unashindwa kujisimamia kwenye yale uliyopanga kuyakamilisha na Kila siku unajiambia nitaanza kesho je utaweza kumuongoza nani? Lazima wewe uanze kuwa mfano kisha dunia nzima itakufahamu na hata baada ya maisha ya hapa duniani bado utabaki kwenye mawazo ya watu.

Marekani wanafahamu karne ya 18 ilikuwa karne ya Marcus,karne ya 19 ilikuwa karne ya Jefferson na karne ya 20 ilikuwa karne ya Martin Luther king,hawa watu pamoja na kwamba walikuwa marekani lakini dunia nzima inatambuwa uwepo wao na vizazi  vingi vitapita na wataendelea kukumbukwa. Watu hawa waliweza kujisimamia na wakajiongoza na kisha watu wakaweka imani kwao na kuweza kuwafuata na kukubaliana nao.

Hivyo acha kuwaza mambo makubwa ya kutawala chochote kama huwezi kutawala fikra, hisia zako na hofu inakutawala,anza na wewe mwenyewe,anza na familia yako, anza ni jamii inayokuzunguka, taifa lako kisha Alama zako zitabaki na kusikika duniani.Asante sana na uwe na siku njema.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251




No comments:

Post a Comment