Thursday, 25 June 2020
There is no end to relationship-Krishnamunt......
Rafiki hongera kwa siku nyingine nzuri, furahi day kama wengi wanavyopenda kuiita, wengi hufurahi siku hii wakiamini ni siku ambayo wanaanza kufurahia mapumziko ya mwisho wa wiki lakini kwako wewe kama unajitoa kweli kufanikiwa siku za mwisho wa wiki ndio siku zitakazoamua hatima ya maisha yako, usikubali kukaa bila kuwa na kitu cha kujishughulisha nacho......
Rafiki leo tuzungumzie kauli ya Krishnamunt ya kwamba haitafikia hatua ukajiambia huhitaji mahusiano na wengine, hili ni zoezi endelevu kwa maisha yako yote kwani chochote kinaumbwa kwa namna kinavyohusiana.
Pamoja na umuhimu wa mahusiano na wengine kwenye maisha yetu,watu wengi tunasahau kwamba huwezi kuwa na mahusiano mazuri na wengine kama huna mahusiano mazuri na wewe mwenyewe, ndio maana tunaamini wanaofanikiwa wanafanikiwa kwasababu wanafurahia maisha, kama wewe mwenyewe hujikubali kwa kile unachofanya hakuna atakayekukubali, chochote unachotaka kukiunda basi tambuwa lazima uwe na mahusiano mazuri na wengine, hakuna mtu aliwahi kufanikiwa kwa kujiambia hahitaji kuhusiana na wengine, mfanyabiashara ili afanikiwe lazima awe na uhusiano mzuri na wateja wake, mfanyakazi ili awe mfanyakazi bora lazima awe na mahusiano mazuri na wafanyakazi wenzake pamoja na wanao pokea huduma kutoka kwake.
Usiruhusu hisia iongoze mahusiano yako na wengine bali ruhusu fikra zaidi dhidi ya hisia,wengi tunaruhusu hisia iongoze badala ya fikra kwenye mahusiano, na ndio maana kosa lile lile alilofanya mtu unayempenda linakuwa ni kosa dogo, lakini kosa hilo hilo akifanya mtu usiyempenda linakuwa kubwa na kukuzwa na wakati mwingine kutokusamehe. Kutatua changamoto yoyote iliyoko mbele yako jiulize maamuzi ninayotaka kufanya yanahusisha kufikiri au hisia?
Rafiki jiulize kama una mahusiano mazuri na wewe mwenyewe?kwani huwezi wapa watu kile usichokuwa nacho, kisha hakikisha una husiana na wengine vizuri kwa kuhakikisha huna chuki na yeyote kwani hakuna kitakachomuumiza yeyote kutoka ndani mwako halafu wewe kikakuacha salama, kama una hasira na yeyote lazima ikuumize wewe kwanza kabla hujamuumiza unayemchukia, huwezi mfanyia mtu ubaya harafu wewe ukabaki salama, siku zote tambuwa kazi yako kubwa ni kusamambaza upendo kwa wengine.
Kazi yangu ni kuhakikisha maisha yangu na yako yanakuwa bora zaidi Kila tunapopata siku moja ya Zawadi zaidi,tutaendelea kua pamoja rafiki nakupenda daima.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944/0712161251
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment