Sunday, 7 June 2020

Una mchango wako kwenye mambo kwenda vibaya.....



Habari za jumapili rafiki, ni kawaida yangu Kila mwisho Mwa wiki kujiuliza maswali kadhaa,wiki imekwisha nimejifunza nini? Nimefanya jambo gani litakalofanya nitimize ndoto zangu? Yapi nimefanya sahihi na yapi sitakiwi kuyarudia kufanya? Kama kuna changamoto ni namna gani naweza zikabili? Nakuomba na wewe upate muda huo ni muhimu sana.....

Rafiki huwa tunashindwa kwenye mambo mengi kwa kuamini kwamba wengine wametusababishia lakini hilo siyo sahihi na tafiti zinaonyesha mambo yanavyokwenda vibaya Kila mtu anao mchango wake, na ndio maana tunaambiwa mambo yakienda vibaya nenda kwenye kioo chako na yule unayemuona ndiye anapaswa kulalamikiwa.

Kocha wa mpira wa miguu Paul Bryant alikuwa akipenda kusema hivi "Jambo likiharibika jiambie ni Mimi nimelifanya, likienda vizuri kidogo sema ni sisi tumelifanya na likienda vizuri sana sema ni nyie mmefanya"

Hii ni kauli ya hekima sana, kauli inayokuondolea hali ya kulaumu wengine na kuona kasoro zako kirahisi na kwakufanya hivyo utapiga hatua kubwa sana rafiki yangu, nenda kaishi kauli hii siku zote na hakika utakuwa imara sana.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment