Sunday, 14 June 2020

Tatizo lako unapenda kujifunza wakati wa machafuko........



Wiki nyingine imekatika, kipi umefanya cha maana kwenye wiki hili? Kipi cha tofauti na wiki zilizopita? Kama ni chakula hata wanyama wa mwituni wamekula na kushiba, jiulize ni lipi la maana umefanya ambalo wanyama wengine hawawezi kufanya? Umeingiza shilingi ngapi? Umetumia shilingi ngapi?kipi umepanga kufanya wiki hili linaloaanza?

Wakati napitia kitabu cha Steve chandler cha 100 ways to motivate your self,Hamasa namba 5 ilisomeka hivi "LEARN TO SWEAT IN PEACE" hapa pakanivutia kusoma zaidi ndani nikakutana na sentensi inayosomeka "As they say in the Navy seals,the more you sweat in peacetime, the less you bleed in war"

Hebu ona mfano huo, hebu vuta picha wewe ni mwanajeshi na siku ambazo hakuna vita wala tatizo lolote hufanyi mazoezi yoyote ya kivita, unasubiria mpaka wakati wa vita ndio uanze kujifunza je utakwenda kushinda vita hiyo? Kama ni mjenzi utasubiria wakati mvua inanyesha ndio uanze kujenga? Kama ni mwanafunzi utasubiria mpaka wakati wa mitihani ndio usome, kama ni mgonjwa utasubiria mpaka umezidiwa kabisa ndio uende hospitalini, Je hakuna namna ya kushindwa kwa hayo yote, kwani huwezi subiria wakati wa vita ndio ujifunze mbinu za kivita na ukashinda. Sasa jiulize kwanini wewe unapenda kuendelea kuendesha maisha yako kwa mfumo huo?

Unasubiria hela ya kustafia ndio uanze biashara?
Huo ni wakati wa machafuko na lazima utashindwa kwenye hiyo biashara na wakati huo ukipoteza ni umepoteza moja kwa moja, wangapi umewaona wameanza biashara za usafirishaji, duka na baada ya muda mfupi kufariki? Usisubirie wakati wa machafuko kuingia vitani anza sasa ili upate uzoefu.

Unasubiria ufukuzwe kazi ndio uanze biashara?
Kila siku nakupa masomo ya namna ya namna unavyotegemea chanzo kimoja cha kipato ilivyo hatari, hebu fikiria bwawa linalotegemea Maji kutoka kwenye chanzo kimoja si lazima likauke? Bahari haikauki kwasababu inapokea Maji kutoka kwenye vyanzo Vingi vya mito ndio maana inaitwa bahari, kumbuka kuna siku kazi hiyo unayoilalamikia kwamba inakulipa kidogo itakua haipo tena, hicho kiduka kimoja au biashara yako moja uliyo nayo kuna siku itakumbwa na dhoruba na isiwepo kabisa, je hapo ndio utaanza kuchukua hatua?

Unaendelea kukaa kwa Wazazi, ndugu na jamaa hutaki kuanza na biashara ndogo kwasababu mama au baba wapo wanaendelea kukulisha,je unafahamu ni lini watu hao hawatakuwepo? Elimu yako nenda kaionyeshe kwa kujitegemea huo mchezo unaocheza ni hatari sana amka rafiki.

Yapo mengi sana ambayo binadamu tunasubiria mpaka wa machafuko ndio tuanze, ila ujumbe wa Leo unasema kadri unavyotoa jasho Leo wakati mambo yako shwari ndivyo wakati wa vita utakapofika utakavyo mwaga damu kidogo, lakini kama sasa unafurahia biashara moja uliyo nayo, kazi uliyo nayo, ndugu uliye naye basi tambuwa kuna siku vitu na watu hao hawatakuwepo na unaweza jifunza kwa wengine bila kusubiria wakati huo ufike.

Sitoacha ku kukumbusha rafiki yangu wakati mzuri wa kujifunza ni wakati huu usisubirie wakati wa mitihani hapo utakuwa umejiandaa kushindwa.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment