Monday, 8 June 2020

Hivi kazi nzuri ni ipi?....



Haijarishi unafanya kipi ilimradi kinakuingizia kipato una Kila sababu ya kumshukuru mungu kwa hilo, karibu rafiki yangu tujifunze pamoja......

Rafiki yangu zipo hadithi ambazo tumezizoea mashuleni, kwa familia zetu zikitutaka tusome kwabidii ili tuje kupata kazi nzuri yenye kutupatia maisha yenye furaha, Je ulishawahi kujiuliza kazi nzuri ni ipi?wakati ukitafakari jibu la swali hili hebu tuendelee na hadithi ya Mike na Robert.

Wiki iliyopita tuliona namna Robert alivyokasilishwa na namna baba yake Mike alivyowafanyisha kazi kwa malipo kidogo na ikafikia wakati Robert alihitaji kuacha kazi kwani alichokitegemea hakipati na analipwa ujira kidogo na hapo Baba tajiri ambaye ni baba wa Mike anampa somo la kwanza ambalo na wewe unapaswa kulifahamu ambalo matajiri wote wanaijuwa siri hiyo kwenye fedha.

MATAJIRI HAWAFANYII KAZI FEDHA.

Rafiki baba huyu tajiri aliwaambia Robert na Mike kwamba watu wengi hufanya kazi ili walipwe na siku zote hulaumu waajiri wao kwamba ni sababu ya maisha magumu kwani hawawalipi vizuri na kuwaza hivyo kunawanyima kuwapa fursa ya kuona makosa upande wao na wamekuwa wakizifanyia kazi fedha badala ya kuona ni namna gani fedha zinaweza kuwafanyia kazi wao.

Robert akamwambia kama ni hivyo basi sipo tayari kuendelea kulipwa kidogo ni bora niache kazi nikatafute kazi nyingine na baba yake Mike anamwambia na hivyo ndio wanavyofanya watu wengi pia huhangaika wakitafuta kazi nyingine kwa kudhani huku watatatua matatizo yao ya kifedha kumbe kadri wanavyolipwa zaidi ndivyo changamoto zinapngezeka, akampa mfano wa baba yake ambaye ni msomi wa PHD lakini bado ana matatizo kibao ya kifedha, akawapongeza kwa kutokubali kulipwa kidogo lakini kuondoka na kutafuta kazi nyingine siyo suruhu ya kumaliza matatizo yao.

Hapa rafiki tunapewa funzo kwamba watu wengi tunadharau kazi tulizonazo kwa kipimo cha malipo na kutamani kazi fulani za wengine na wakati mwingine kwa kuongeza elimu na jitiada mbali mbali tunafanikiwa kuzipata kazi hizo, pamoja na malipo mazuri bado changamoto za kifedha zinaendelea. Watu wengi hudhani kazi nzuri ni inayokulipa zaidi lakini matajiri wanafahamu kazi siyo tatizo tatizo ni elimu ya namna fedha inavyoweza kukufanyia kazi.

Baada kupewa somo hilo Robert na Mike walianza kuelewa lakini akauliza ni njia gani nitaitumia kutengeneza fedha zaidi? Rich dad akamwambia tumia kilichopo ndani ya kichwa chako, hicho ndio kitu pekee kitakachotatua matatizo yako ya kifedha.

Rafiki hapa tunapata funzo kwamba usilizike kulipwa kidogo maisha yako yote na wala usifikirie kwamba kazi inayokulipa kipato kikubwa itazimaliza changamoto zako za kifedha bali tumia ubongo wako kufikili namna fedha unayopata inaweza kukufanyia kazi wewe na hili litakuondolea matatizo yako yote ya kifedha. Asante sana rafiki na nikutakie siku njema.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944 /0712161251.

No comments:

Post a Comment