Thursday, 11 June 2020

Usipime utajiri wako kwa kiasi cha kipato unachotengeneza pekee bali pamoja na njia unazotumia kutengeneza kipato........,.


Nakusalimia ndugu yangu, mfanyakazi unaye subiria kwa umakini kuona bajeti ya mwaka huu inakwendaje kubadilisha maisha yako, nakupa pole kwasababu hicho unachokitarajia ni zaidi ya utumwa kwenye maisha yako hebu pata muda na waza kwa kina huko nyuma umeongezewa mishahara mingapi je kipi ulifanyia? Je matatizo ya kifedha yalikwisha? Hebu jaribu kuwaza nje ya box uondokane na utumwa huo......

Rafiki yangu Leo tuangalie maana ya neno KIPATO na  aina za vipato pamoja na kipato kitakacho amua Uhuru wako kifedha, wiki iliyopita niligusia eneo la fedha na sheria zake, pamoja na kwamba najitahidi kugusia maeneo mengi lakini yapo maeneo mengi naruka kwani siwezi kukuchambulia Kila kitu, nakushauri tuwasiliane nikuambie ni namna gani unaweza jipatia kitabu hicho cha ELIMU YA MSINGI KUHUSU FEDHA.

KIPATO maana yake nini? Kipato ni ile fedha unayolipwa kutokana na kufanya au kuwezesha kitu fulani kufanyika.Inaweza kuwa ni kazi ambayo umefanya wewe au bidhaa na huduma ulizotoa kwa wengine ambazo wanazihitaji ili maisha yao kuwa bora. Hapa unaweza kuona kwamba namna ya ukubwa wa huduma au matatizo ya wengine unavyoweza kuyatatua ndivyo na wingi wa fedha ulivyo. Ndio maana masomo yaliyopita tuliona kwamba fedha ni matokeo ya thamani unayotoa kwa wengine. Kila mmoja wetu anaingiza kipato kwa namna yake mwenyewe, wapo walio ajiriwa na walio jiajiri wenyewe.

Wengi tunatamani kupokea kipato kikubwa lakini hatufahamu kwamba kwa kuendelea kufanya kitu kile kile tutaendelea kupokea kitu kile kile, kama unataka kupata kipato kikubwa zaidi basi ongeza wigo wa kutatua matatizo ya wengine siyo kung'ang'ana na kitu kile kile. Pamoja na utofauti wa majukumu yetu tunayobeba na kutuingizia kipato zipo aina kuu mbili tu za kipato,ambazo unapaswa kuzifahamu kwa kina na umuhimu wake kwenye maisha yako.

1.KIPATO CHA MOJA KWA MOJA(ACTIVE INCOME)
Kipato chochote ambacho unakipata kwa kutegemea uwepo wako moja kwa moja ndio ulipwe hicho ni kipato cha moja kwa moja. Kama umeajiriwa basi lazima uende kazini ndio ulipwe, Kama ni mfanyabiashara lazima uwepo eneo la biashara ndio uingize kipato, changamoto za kipato hiki ni kwamba kina ukomo kwasababu huwezi kuwa sehemu nyingi kwa wakati mmoja, kipato hiki kinahitaji masaa yako ambayo hayawezi kuzidi 24,hivyo hata kama unalipwa kiasi kikubwa namna gani bado huwezi kuwa na Uhuru kifedha na ndio maana wengi tunao ingiza kipato kupitia njia hii pale tunapofariki kama ni familia Mara moja inaanza kuhangaika kwani na kipato kinaondoka Mara moja.

2.KIPATO KISICHO CHA MOJA KWA MOJA (PASSIVE INCOME)
Hiki ni kipato ambacho kinaingia hata pasipo uwepo wako wa moja kwa moja kwenye shughuli inayokuingizia kipato. Ukiwa umelala kipato kinaingia, uwe matembezini na familia kipato kinaingia.Hapa kipato kinaingia kwasababu ya uwekezaji ulio fanya.uwekezaji kwenye hisa au riba unayopata kutokana na fedha ulizowekeza.

Rafiki nafikiri sasa umeweza kuona ni kipato gani unakihitaji kati ya vipato hivyo viwili, baada kujijengea usomaji wa vitabu kwa muda mrefu nilipata kupenda kujifunza falsafa ya ustoa na katika mafunzo hayo lipo swali ambalo huwa napenda kujiuliza FAMILIA YANGU ITAISHI VIPI KAMA NITAKUFA SASA HIVI?sasa kama kipato changu kitaendelea kuwa cha moja kwa moja nadhani unafahamu hali itakuwaje.

Hivyo rafiki pambana siku zote ufahamu namna ya kuwekeza na tena anza kuwekeza sasa hivi, kabla sijawa member wa KISIMA CHA MAARIFA niliamini uwekezaji ni kwa watu wenye vipato vya ubilionea lakini baada ya kujifunza nimeweza kuanza kuwekeza taratibu na kwa kipato hiki hiki unachokiona ni kidogo, kutaka kufahamu ni kwa vipi unaweza kuwekeza karibu sana KISIMA CHA MAARIFA sehemu itakayo badili maisha yako.Rafiki wewe ni wa thamani kwangu ndio maana unapokea makala hii, nakupenda daima na mungu akubariki.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment