Tuesday, 16 June 2020

Sehemu ya kipato changu ni mali yangu (III)......



Rafiki yangu hongera kwa afya na siku hii nzuri,hakika mungu wetu ni Mkuu sana tuna Kila sababu ya kumtukuza.........

Leo tunaendelea na sehemu ya tatu ya SEHEMU YA KIPATO CHANGU NI MALI YANGU na bila wasiwasi sasa umefahamu huruhusiwi kugawa fedha zako kwa Kila mtu na kujisahau wewe mwenyewe na nikuambie kitu kimoja kuhusu fedha, KAMA HUWEZI KUISHI CHINI YA KIPATO CHAKO hata ukipewa fedha kiasi gani utazitawanya na kurudi maisha yako ya awali, anza sasa kujijengea nidhamu ya kutumia chini ya kipato chako kwanza,haijalishi kipato chako ni kidogo kiasi gani tumia chini ya hicho unachopokea.

Tuendelee na simulizi ya Arkadi anayesimulia utajiri wake kutokana na ushauri aliopata kutoka kwa mtu mwenye hekima Algamish,kilipita kipindi cha takribani miaka miwili na tajiri Algamish alirudi na kukutana na Arkad na kumuuliza umeshaupata utajiri? Arkadi akamjibu hapana bado ila Nina vyanzo Vingi vya mapato ambavyo vinaendelea kumzalishia. Algamish akamwambia vizuri sana je bado unapokea ushauri wa muuza matofali? Arkad akasema labda kuhusu matofali na siyo vitu vingine.

Baada ya mazungumzo hayo Algamish akamwambia Arkad nimeshakuwa mzee sasa na kwakuwa umeshajifunza namna fedha inavyotengenezwa, Jinsi ya kuzitunza fedha na kivipi fedha inaweza kukufanyia kazi, yeye ni mzee na Mtoto wake anawaza namna ya kutumia fedha na utajiri wa baba yake. Hivyo akamuomba Arkad akawe msimamizi wa vyanzo vyake vya mapato. Arkad alikubali na alisimamia vizuri sana Mali zile na wote wakapata faida.Alikua anawapa simulizi hii wakamwambia Arkadi una bahati sana,Arkadi akawajibu mnasema nina bahati mmesahau nilivyoanza na kupoteza fedha zangu na kuvumilia kuanza tena? Wakamwambia je na sisi tukifuata ushauri huu tutakuwa na utajiri kama wako? Akawajibu mkiweka nguvu na jitihada lazima mtafanikiwa na fedha zinapatikana kwa njia za ajabu sana.

Rafiki hapa kuna funzo tunalipata, fedha inaanza kutengenezwa kwa kuishi chini ya kipato unachopata, fedha unazopata utaweza kuzitunza kama utapokea ushauri kwa watu wenye uzoefu wa kitu unachotaka kufanya, na kama utaiwekeza sehemu unayoifahamu itakufanyia wewe kazi badala ya wewe kuendelea kuitumikia kwa maisha yako yote.

Hayo ndio machache kuhusu fedha kwa kuanzia, wiki ijayo siku kama hii ya jumanne tutaendelea na sehemu nyingine kwa kuanza kuangalia ni namna gani tunaweza kutunisha mifuko iliyo sinyaa, zipo njia saba ambazo tunazipata toka kwenye kitabu cha THE RICHEST MAN IN THE BABYLON naomba usikose hata somo moja na endelea kupitia masomo yaliyopita kwa kubonyeza;

https://kinyagakelvin.blogspot.com

Kinyagakelvin162@gmail.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment