Sunday, 21 June 2020

Hivi ndivyo ujinga wa fedha unavyoathiri jamii....



Rafiki yangu hongera kwa kuwezi kuianza wiki hii nyingine, ni matumaini yangu hutokwenda kujipa sababu yoyote bali kutekeleza yale yote yaliyo kwenye mipango yako kama unavyoweza kukamilisha ratiba yako ya chakula na mipango yako ikapate kutimia.....

Kwanza kabisa nikushukuru kwa kuendelea kufuatilia mfululizo wa makala zangu kutoka katika kurasa zangu za Ustawi wa fikra, Nina hakika mabadiliko yoyote yanaanzia na fikra zetu.Hivyo sina shaka na nguvu ya maarifa kwenye mafanikio.

Kama ilivyokawaida yetu kwenye siku ya jumatatu tunachambuwa kitabu cha Rich dad,poor dad na mpaka kufikia Leo tumeshajifunza mambo mengi na hupaswi kusubiria chochote nenda kayaweke kwenye vitendo.Leo tutajifunza ni kwa namna gani utaweza kuzitawala fedha zako na siyo zenyewe kukutawala.

Leo mwandishi anatutaka kwanza tuweze kufahamu kwamba fedha haimalizi matatizo bali inayazidisha na kuyaongeza, mwanzo unapokuwa huna fedha unakuwa na matatizo kidogo, pengine ni makazi duni,mlo kamili hupati na shida ndogo ndogo, lakini kadri fedha zinapoongezeka na changamoto zake zinaongezeka na ndio maana wengi hurudi kwenye maisha yao ya mazoea, kwani wanapoanza kufanyia kazi fedha na kuziongeza na changamoto zinaongezeka na hii hutokana na watu kupenda kupata raha na furaha zaidi na vitu hivi huchangia matumizi kuongezeka.

NGUVU YA KUTAWALA FEDHA NA SIYO KUIGOPA
Wiki iliyopita tuliona namna hisia mbili zinavyotuendesha kwenye fedha, hisia za hofu ya kutokuwa na fedha na tamaa ya kuzitumia zimekuwa kikwazo kwetu kufanikiwa, sasa mwandishi anasema ukiweza kutawala hisia hizi mbili basi utakuwa pia umeweza kutawala fedha zako kwani fedha zinakuendesha kwasababu umeshindwa kutawala hisia zako.

Mwandishi anasema ujinga wa kutotaka kujifunza ndio sababu inayowafanya watu kuendelea kuteseka na fedha, watu wengi wakishahitimu masomo na hapo ndio inakuwa mwisho wa kujifunza na hapo ndipo wanapokubali kuendelea kuishi na ujinga wao, anasema watu hupenda kununua vitu vya kujionyesha na siyo kwasababu wana vihitaji na ni muhimu kwao kwa wakati huo,hayo yote ni matokeo ya ujinga wa kuto hitaji kujifunza.

Chukulia mfano Daktari anaongeza gharama za matibabu ili aweze kuongeza kipato chake, mwanasheria naye hivyo hivyo anataka kulipwa zaidi, mwalimu naye hivyo hivyo na mwisho wa siku mfanyabiashara naye anaongeza bei ya bidhaa na baada ya hapo serikali nayo inaongeza kodi na hivyo ndivyo ujinga wa fedha unavyo athiri jamii. Na pale tofauti ya wenye nacho na wasio nacho inapoongezeka na kuwa kubwa ndipo anguko la hilo taifa linapotokea.

Baada ya baba tajiri kuwaeleza Robert na Mike haya yote Robert akamuuliza kwa hiyo gharama hazitakiwi kuongezeka? Baba tajiri anawajibu kwa jamii inayoongozwa na serikali bei hazitakiwi kupanda bali kushuka.Akawaambia waendelee kufanya kazi bure huku vichwa vyao vikiendelea kufikiri ni kwa vipi wataondokana na mtego huo wa panya.

Robert na Mike Kila siku waliendelea kuwaza swali la wao kufanya kazi bila kulipwa, siku moja jumamosi wakiwa kazini walimuona yule anayewasimamia akichukuwa vitabu na kutaka kuondoka navyo ndipo wakamuuliza unavipeleka wapi? Akawajibu kuna sehemu anavirudisha ili kupewa vingine, basi walikwenda hiyo sehemu ya vitabu na kuuliza kama wanaweza kupatiwa vitabu vile na wakajibiwa inawezekana ila kwa sharti la kutoviuza.

Basi walivichukuwa vitabu vile na kwenda kuviweka nyumbani kwa kina Mike na walitumia sehemu ile kama maktaba na mkutubi akiwa ni msaidizi wa kazi wa kina Mike na watoto walikuja kusoma vitabu vile huku wakilipia, maktaba hiyo ilifunguliwa masaa mawili kwa siku na waliweza kupata dola 9 kwa wiki na walimlipa yule mkutubi dola 1,baadaye walianza kuwaza kufunguwa tawi lingine baada ya wateja kuongezeka, kwa bahati mbaya siku moja vurugu zilizuka pale maktaba na maktaba hiyo ikaamuliwa kufungwa.

Baba tajiri aliwapongeza kwa uthubutu wao na kuwaambia wasikate tamaa.

Rafiki yangu kwa Leo tuishie hapa tukutane tena wiki ijayo kuweza kuona kwa kina mafunzo yaliyo kwenye kitabu hiki, Asante na uwe na siku njema.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment