Saturday, 6 June 2020
Kazi yako ni kuwaongoza na kuwaelekeza na siyo kujaribu kuwatatulia matatizo yao yote yanayowakabiri.......
Hongera sana rafiki yangu, kama unajaribu kupunguza mateso kwa wengine ni kazi nzuri sana unafanya na endelea, watu wanateseka kwa kukosa upendo basi wasambazie upendo, watu wamekata tamaa ya kuendelea mbele wakumbushe jukumu lao, usimseme yoyote vibaya kama yeye hayupo hapo nenda kamfate mweleze atakuelewa kama amekosea na kurekebisha, je bado una kinyongo na mtu? Chuki haiwezi kukusaidia nenda kamwonyeshe upendo Leo anayekuchukia........
Leo tutaangalia sehemu ya malezi kwa watoto wetu, Kila Mzazi hapendi kuona Mtoto/watoto wake wakiteseka, hapendi waje kuhangaika na maisha ya baadaye,tunatamani kuona maisha yao yanakuwa mazuri.
Bahati mbaya sana pamoja na matamanio hayo hatuwaandai watoto wetu kuwa bora, kwani tunajaribu kuwaonyesha kwamba Kila kitu ni rahisi, Kila wanachotueleza tunapambana kuwapatia lakini je huo ni uhalisia wa maisha?Je maisha yatatupa Kila tunachohitaji?
Thomas Edison ni mfanyabiashara mwenye mafanikio makubwa sana na yeye ni miongoni Mwa mzazi ambaye alitamani sana watoto wake wawe na maisha mazuri lakini njia alizozitumia na ambazo wengi tunazitumia kulea na kuwaandaa watoto wetu hawawezi kuwa vile tunavyotaka na hilo lilimfanya mke wake amwandikie ujumbe ambao nitauweka hapa chini, ujumbe huo ulisomeka hivi;
“You’ve made a success of your life,” she wrote, “built up tremendous industries successfully so you have nothing more to prove to the world that you are capable—All know it—Can’t you be happy in just letting the boys struggle along, with you to guide them… Forget a little bit that you are Charle’s manager and be a father—a big father!”
Sasa hili ndilo linatukumba Wazazi tulio wengi, hatuwezi wapa nafasi watoto wetu wakajisimamia, muda wote tunahitaji watutegemee sisi kwa Kila kitu, kama tunataka wakue,wajifunze na wawe na maisha mazuri basi waache wapambane wenyewe na kazi yako kubwa ni kuwaongoza tu, siyo Kila anachohitaji unampatia labda utaishi nae maisha yako yote.
Kazi yako ni kuwa baba na siyo boss kwa watoto wako, kama familia inakuchukulia wewe ndio boss wao basi fahamu kwamba kuna siku utalia machozi na hakutakuwa na wakukufuta machozi.
Asante na siku njema rafiki yangu.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944/0712161251
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment