Monday, 15 June 2020

Tatizo ni kwamba huna na uifahamu elimu unayopaswa kuijua maisha yako yote ya hapa duniani.



Rafiki yangu nakukumbusha kwamba thamani unayolipwa ndio thamani yako halisi, huwezi kubali kwenda sokoni kununua embe moja kwa Tsh Milioni moja hata kama una fedha kiasi gani, ndivyo anayekulipa anavyoona thamani yako na kukulipa kile unachostahili, na wewe umelizika na kiasi hicho kwasababu hakuna anayekuhitaji ili akulipe zaidi, ungekua na thamani kubwa Kila mtu angekung'ang'ania na kutaka akulipe zaidi ili anufaike na wewe, sina la kukuambia kama unaona hustahili kulipwa unacholipwa jiulize ni nani anaweza kunilipa zaidi? Kwa thamani gani niliyo nayo?


Kama unasoma hapa nina hakika mtazamo wako unaanza kubadilika na kama unahitaji kupata ufafanuzi zaidi tuwasiliane kwani nimezungukwa na maarifa mengi sahihi na pia nimezungukwa na wana kisima cha maarifa zaidi ya mia mbili waliobobea kwenye Kila eneo, kuanzia udaktari, ufugaji, sheria, kilimo na Kila aina ya changamoto kama si Mimi basi nitakuunganisha nao na changamoto zako zitapungua hivyo usijiwekee mipaka kupata ushauri zaidi.

Leo tunaendelea na chambuzi ya kitabu cha RICH DAD, POOR DAD wiki iliyopita tuliweza kuona tofauti ya masikini na matajiri,MATAJIRI HAWAIFANYII KAZI FEDHA na hapo tuliweza kuona Robert na Mike wanapatiwa somo hilo na kuanza kulielewa. Sasa Leo tutaona ni namna gani fedha inaweza kukufanyia kazi wewe na mwandishi anasema elimu hii ndio elimu uliyopaswa kuifahamu na kuisoma maisha yako yote, lakini pamoja na utitili wa vyeti ulivyo navyo bado hujawahi kufundishwa ni kwa namna gani fedha itakufanyia kazi wewe badala ya wewe kuifanyia kazi fedha.

Mike na Robert somo lilipoanza kuwaingia Rich dad anawauliza mko tayari kuendelea na somo? Wakajibu ndio, akawaambia kama mko tayari basi mtaendelea kufanya kazi na safari hii siwalipi chochote, kwa mshangao Robert akabaki kuwaza kwamba amekuja kudai aongezewe mshahara badala yake halipwi kabisa!!? Nadhani hata wewe ungeshangaa. Rich dad akawaambia wachague kama wanataka kuwa kama wafanya kazi wengine atawaongeza mshahara mpaka kufikia dola za kimarekani 5 kwa saa ,kutoka kuwalipa senti kumi.Hapa Robert anasema kwa umri wake mdogo alikua anatamani sana kulipwa kiasi hicho lakini kwasababu somo la kutoifanyia kazi fedha lilikua limeingia alikaa kimya na kuto kubali ofa hiyo ili afundishwe ni namna gani fedha itakwenda kumfanyia kazi, basi baada ya kukataa ofa hiyo kubwa Rich dad akawaambia waendelee na kazi.

Robert na Mike waliendelea kufanya kazi bure bila ya kulipwa chochote, na Robert hakumwambia baba yake masikini (poor dad)kwamba anafanya kazi bila kulipwa kwa baba yake na Mike(Rich dad) na baada ya hizo wiki tatu kufanya kazi bila malipo Rich dad anarudi na kuwaambia waende matembezi pamoja, wakiwa matembezini anawauliza mambo yanakwendaje? Je kuna mambo mapya wamejifunza zaidi kwa hizo wiki tatu? Kwasababu kama mnataka kua na utajiri lazima mjifunze mambo mengi.

HISIA HIZI MBILI ZINAWEZA KUKUFANYA UWE MTUMWA WA FEDHA MAISHA YAKO YOTE, ZIFAHAMU NA ONDOKANA NA UTUMWA HUO.
Baada ya Rich dad kuona vijana wanavutiwa na somo la kutaka kufahamu namna fedha inavyowafanyia kazi Rich dad anawaambia nukuu hii ambayo nataka na wewe uifahamu.

"Most people have a price.And they have a price because of human emotions named fear and greed.First,the fear of being without money motivates us to work hard, and then once we get that paycheck,greed or disire starts us thinking about all the wonderful things money can buy."

Hapa rich dad anasema ukweli mtupu,hisia za hofu na tamaa ni hisia zinazofanya waajiriwa tuendelee kuwa watumwa,kwanza inaanza hofu ya kuto kua na fedha, hofu  hii inatusukuma kufanya kazi kwa bidii ili tulipwe na tukishalipwa fedha tunaingiwa tamaa ya kuzitumia fedha hizo. Hapa mwandishi anasema hili linatufanya tutengeneze kanuni ya AMKA, NENDA KAZINI, PATA MSHAHARA, LIPA MADENI.na kanuni hii inaendelea kwa maisha yetu yote, hivyo tunakuwa watumwa wa fedha kwa maisha yetu yote. Hisia hizi zinafanya kazi Kila fedha inapoongezeka tamaa ya kuzitumia inakuwepo na kukufanya uendelee na utaratibu huu. Na hapa mwandishi anaita utaratibu huu MBIO ZA PANYA kwani haziwezi kutufikisha popote pale kwenye kujikomboa ki uchumi.

Baada ya kumsikiliza baba tajiri Robert akauliza Je kuna njia nyingine? Baba tajiri akamjibu ndio ipo njia nyingine ambayo matajiri wanaitumia.Akawaambia wafanyakazi wengi wanapata hisia za hofu ya kutokuwa na fedha ila badala ya kuikabili kwa kufikiri wanakimbilia kutaka walipwe zaidi na hapo wanakuwa watumwa wa fedha kwa maisha yao yote.

Kwa Leo tuishie hapa rafiki, Kila jumatatu uchambuzi wa kitabu cha Rich dad, poor dad utakujia kupitia page hii ya Ustawi wa fikra, kama ulipoteza masomo yaliyopita bonyeza  https://kinyagakelvin.blogspot.com  na hapo utayapata yote, endelea tuwe sote kuna mengi sana utajifunza.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251


No comments:

Post a Comment