Wednesday, 3 June 2020

Maombi pasipo Imani ni kazi bure......


Habari za wakati huu ndugu yangu na rafiki yangu, baada ya salamu napenda kukuambia kwamba nina kupenda sana na ninakuombea Kila siku ufanikiwe lakini kama huna imani na mafanikio ninayokuombea maombi yangu kwako ni kazi bure.......

Rafiki tuendelee na chambuzi kutoka vitabuni, na Leo tuendelee kutoka kitabu chetu cha THINK AND GROW RICH,wiki iliyopita tulionao nguvu ya shauku kwenye mafanikio na mambo mengi ambayo yamefanyika hapa duniani ni kwasababu ya shauku kubwa ambazo zilikuwepo ndani Mwa watu, Henry Ford alipata shauku kubwa ya kuona watu wanaacha kutumia farasi kama njia kuu ya kusafiria na kugundua gari,Wright brothers walipata shauku ya kutengeneza kitu kitakachoruka kama njia ya usafiri na kugundua ndege, Thomas Edison alitamani tuwe na kitu kinachotoa Mwanga kutokana na Umeme na kugundua taa za umeme pamoja na majaribio zaidi ya elfu kumi yaliyoshindwa lakini hakukata tamaa, hivyo SHAUKU kubwa ni hatua ya kwanza kuelekea kwenye mafanikio.

Leo tutaangalia hatua ya pili ambayo ni IMANI na namna inavyotengenezwa,Kwanza kabisa tuangalie Imani ni nini? Imani ni hali ya mawazo/akili ambayo inawezwa kutengenezwa au kuingizwa kwa mawazo yanayojirudia kwenye akili ya ndani ya binadamu(Subconscious mind) na kupitia  eneo hili ndio tunaweza kutengeneza utajiri mkubwa.

Eneo hili la akili ya ndani(Sub conscious mind) linaapokea kile kitu ambacho kinarudiwa sana na kukiona ndio sahihi, hata kama kitu hicho siyo sahihi kwakuwa umejiambia au kufanya kwa kurudia rudia basi sehemu hii inachukulia kitu hicho ni muhimu, hapa ndio maana mtu akitengeneza tabia hasa mbaya inakuwa ngumu kuivunja, tabia ya kukopa, wizi,uzinzi na tabia zingine kadha wa kadha,unapoanza kutengeneza tabia hizo kwa Mara ya kwanza kuna hali ya wasiwasi lakini unapozirudia Mara kwa Mara sehemu hii ya akili inachukulia ni kitu sahihi na kufanya uendelee kutekeleza.

Sasa unaweza kutumia eneo hili kutengeneza utajiri, unazikumbuka zile hatua sita za kufuata ili kufikia utajiri? Sasa kwa kuzisoma Kila siku unajitengenezea imani kwamba jambo lile ulilokusudia linawezekana, Kama una amini Kila jambo linalokutokea ni mkosi basi hali za namna hiyo zitaendelea kukutokea na kama una amini wewe ni mtu mwenye bahati nzuri, basi hali za uzuri zitaendelea kujitokeza dhidi yako.

Imani ni kitu ambacho kinalipa wazo lako maisha, ndio kinga pekee ya kushindwa.Imani inapochanganywa na maombi inafanya kitu kikubwa sana.

Rafiki nenda kaishi imani na tengeneza Imani chanya kwa kurudia vile ambavyo ni sahihi kwa kujiambia Kila siku nini unahitaji kwenye maisha yako, hakika hakutakuwa na chochote cha kukuzuia.

Kinyagakelvin162@gmail.com

Kupata masomo yaliyopita bonyeza kiungo hiki chini;

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/071216151

No comments:

Post a Comment