Tuesday, 2 June 2020

Sehemu ya kipato changu ni mali yangu.......



Rafiki hongera kwa siku hii nyingine, siku ambayo ni bahati sana kuiona na vyovyote unavyoichukulia siku hii lakini tambuwa upo wajibu wa kuifanya iwe bora zaidi kataa mazoea ishi kusudi la maisha yako.......

Rafiki yangu Leo tunaendelea na chambuzi kutoka kwenye kitabu cha THE RICHEST MAN IN THE BABYLON kitabu ambacho Kila siku ninavyoweka bidii kusoma vitabu vinavyohusiana na fedha waandishi hawaachi kuelezea umuhimu wa kitabu hicho kwenye maisha yao, ni kitabu ambacho kina nguvu sana kama utafanyia kazi kanuni za fedha utakazojifunza humo. Karibu tuendelee na uchambuzi......

Wiki iliyopita tuliona namna Arkad mtu tajiri kuwahi kuwepo kwenye mji wa Baberi akielezea ni kwa namna gani aliweza kutoka kwenye uandishi mpaka kuwa na utajiri mkubwa na namna alivyokutana na Algamish aliyemfundisha kanuni za fedha.

Algamish alipokwenda kuchukuwa kanuni yake aliyokuwa akiandikiwa na Arkad alikuta imekamilika ndipo akafurahi na kumwambia Arkad umetimiza ahadi yako sasa ni zamu yangu kutimiza ahadi yangu ya kukufundisha kanuni zitakazokufanya uwe na utajiri na alianza kwa kumwambia maneno haya chini ambayo nayanukuu kutoka kwa Algamish mwenyewe.

"I FOUND THE ROAD TO WEALTH WHEN I DECIDED THAT A PART OF ALL I EARNED WAS MINE TO KEEP."

Hii ndio kauli ya kwanza ambayo Algamish alimwambia Arkadi kama ushauri ambao mtu anapaswa kuanza nao pale anapotaka kuondokana na matatizo ya kifedha. Arkadi akauliza kwa mshangao Je ni hivyo tu ndio kutanifanya niwe tajiri?

Pengine hata wewe unaweza kushangaa, kwamba kwa kuamua kutenga pembeni sehemu ya kipato chako na kukifanya Mali yako kunakufanya uwe na utajiri?Je wewe unatenga sehemu ya kipato chako na kukifanya Mali yako?

Arkadi anamwambia Algamish kwamba lakini kwani kipato changu chote si ni Mali yangu? Pengine na wewe ungeuliza swali hilo kwani ndivyo unavyoamini,lakini ukweli siyo huo. Hebu jiulize swali moja,kipato chako kinakwenda wapi? Kama ni mwajiriwa kabla hujapata kipato chako kuna kodi, bima ya Afya,mifuko ya jamii na makato mengine yanakatwa moja kwa moja, halafu ukishachukuwa kiasi unachopata unaanza kulipa kodi ya nyumba, ada za watoto, hela ya chakula, bili za Umeme, king'amuzi na matumizi kadha wa kadha,kwahyo kipato unachopata unakitumia kwa kuwalipa wengine halafu wewe unajisahau kujilipa.

Rafiki yangu unachotakiwa kufahamu ni kwamba hakikisha kabla hujawalipa wengine jilipe wewe kwanza, chukuwa si chini ya asilimia kumi ya kipato chako kiwekeze ili kije kukufanyia kazi baadaye na kama unatumia hela yote unayoipata basi hapo utazifanyia kazi fedha maisha yako yote lakini kama unatenga sehemu ya kipato chako na kuziwekeza basi itafikia wakati fedha zitakufanyia wewe kazi. Na hapa mwandishi anatushauri tulifanye hili mapema tusisubiri mpaka tunapokaribia uzeeni au kustafu ndio tuanze utamaduni huu kwani kadri utakavyopanda mti mapema ndivyo utakavyoota mapema.

Swali la kujiuliza je kama mwaka ulio anza kazi ungetenga asilimia 10 ya kipato chako Kila unapopokea fedha Leo ungekuwa na Tsh ngapi? Sasa kama hukufanya hivyo hebu jiulize asilimia 10 ya kipato chako Leo ukiizidisha Mara miezi 12 ya mwaka mmoja, halafu kiasi utakachopata ukakizidisha Mara miaka 10 unapata kiasi gani? Hujachelewa unaweza kuanza sasa.

Wiki inayofuata tutaona hatua inayofuata baada ya kuweka utaratibu wa kutenga sehemu hiyo ya kipato chako na ni kwa vipi utakiweka na namna ya kukiwekeza ili kikufanyie kazi wewe, asante sana rafiki pengine umejifunza kitu na unakwenda kukifanyia kazi Mara moja huna haja ya kuchelewa.

Makala hizi nzuri zimeandikwa na Mimi Mwalimu na mwandishi ambaye ninatamani tuvuke pamoja na ndio maana nakushirikisha na wewe.

Kinyagakelvin162@gmail.com

Blog yangu;
https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment