Tuesday, 30 June 2020

Zifahamu aina za maarifa na namna ya kutumia ili kufikia ndoto zako.....


Habari za wakati huu rafiki, hongera kwa mwezi huu mpya kama tunavyopenda kuita na wakati huo huo tunaendelea kufanya mambo yale yale na kukaa kusubiria matokeo tofauti, kama kweli tunataka uwe mwezi mpya basi chaguwa mambo ambayo hayakuwa na tija kwako kwenye mwezi uliopita na achana nayo,kisha peleka nguvu zako kwenye yale muhimu na yatakayokusaidia kufikia ndoto zako kwa wepesi iwezekanavyo.

Rafiki kama ilivyo kawaida yetu siku hii ya jumatano kwenye Kila wiki tunajifunza kutoka kitabu cha Think and grow rich, kitabu ambacho mwandishi anatushauri tunaposoma tusijaribu kuacha hata jambo moja na kutolifanyia kazi, tujifunze na kwenda kufanyia kazi.

Leo tutaangalia umuhimu wa maarifa na aina za maarifa, rafiki yangu utakubaliana na mimi kwamba karne hii tuliyopo ni karne ya maarifa na taarifa sahihi, kama unakwenda kufanyia kazi maarifa au taarifa sahihi basi hakuna atakayekuzuia kufika unapotaka kufika, pamoja na umuhimu wa taarifa na maarifa bado watu wengi wanatumia muda mwingi kusikiliza au kutafuta taarifa zisizo na manufaa yoyote kwao, watu hupenda kusikia habari hasi, kutumia muda mwingi kubishania mambo mbali mbali yanayoendelea na yasiyo na tija yoyote kwao, Leo tutajifunza aina za maarifa na utafahamu ni maarifa gani utapaswa kuyatumia kupiga hatua.

Zipo aina mbili za maarifa, aina ya kwanza ni MAARIFA YA KAWAIDA ambayo hupatikana kwenye jamii na mashuleni, na maarifa haya yanaitwa ya kawaida kwasababu yana mambo mengi sana na wingi huo wa maarifa bado hauwezi msaidia mtu kwenye kumpatia hitaji lake, maarifa haya ni kama njia ambayo itakusaidia kuweza kupata mwanga wa kule unakotaka kufika.

Aina ya pili ni MAARIFA YA KITAALUMA, haya ni yale maarifa ambayo Kila mtu anatakiwa kuyapata, ni maarifa ambayo yanapatikana kwa mtu anayefahamu ni kwa vipi anayapata na kuyatumia na yakamsaidia kwenye kutatua changamoto zake ambazo zinamkwamisha kufikia ndoto zake. Mwandishi anasema ukiyapata maarifa haya na kuweka kazi lazima utapiga hatua kubwa sana.

Mwandishi anasema maana ya elimu ni yale maarifa ambayo mtu unayapata ili kuendeleza kile kilichopo ndani yako,hebu tuone maeneo ambayo elimu hii ya kitaaluma inapatikana.

1.Uzoefu wako mwenyewe kwa elimu uliyopata.

2.Uzoefu na elimu za watu wengine ambao upo nao.MASTER MIND GROUP hili ni kundi la watu ambao mna ujuzi tofauti tofauti na mnasaidiana kufikia ndoto zenu (Kisima cha maarifa ndio mfano sahihi wa master mind group)

3.Kwenye vyuo mbali mbali vinavyotoa taaluma mahususi kwa kozi fulani.

4.Usomaji wa vitabu

Haya ndio maeneo ambayo elimu ya kitaaluma inapatikana,hivyo kama unataka kupiga hatua kubwa kufikia ndoto zako basi pigana kupata elimu kutokana na maeneo hayo.

"Any man is educated who knows where to get knowledge when he needs it and how to organize that knowledge into definite plans of action"

Ukishafahamu wapi elimu unayohitaji ili kukusaidia kufikia ndoto zako, kisha kuitumia elimu hiyo kwa kuunganisha na vitendo,basi utapiga hatua kubwa sana, kisima cha maarifa tunaishi kanuni ya PATA MAARIFA SAHIHI+WEKA KAZI KUTOKANA NA MAARIFA ULIYOPATA=MAFANIKIO MAKUBWA, hii inatupa picha kwamba maarifa pekee hayaleti muujiza wowote, bali yanapounganishwa na vitendo kwa kuyafanyia kazi ndio kutatupatia mafanikio makubwa.

Kwenye kitabu hiki kipo kisa kimoja kimeelezwa kinachomuhusu tajiri wa kipindi cha vita vya dunia Henry Ford,mtu aliyekuwa tajiri wa dunia kwa kipindi hicho ambapo gazeti moja la Chicago marekani lilimwandika kama mtu asiye na elimu na kumdhalilisha, Henry aliamua kufunguwa mashitaka dhidi ya wamiliki wa gazeti na moja ya utetezi wake kuhusu kuwa na elimu ndogo,aliulizwa kuhusu idadi ya wanajeshi wa kimarekani waliokwenda kupigana vitani, akajibu hakumbuki idadi kamili ila ni wengi na pale anapoulizwa  maswali  ya kijinga kama hayo, akiwa na maswali ambayo kwa kuyajibu kuna mnufaisha yeye kufikia ndoto zake basi ana vijana wake alio waajiri watampatia majibu ya maswali hayo, hivyo haoni umuhimu wa kujifunza Kila kitu wakati havimsaidii kwenye kutimiza ndoto zake, ila ana uwezo wa kupata elimu yoyote anayohitaji.

Hili linatupa funzo kwamba elimu tulizojifunza darasani zina mambo mengi ambayo hayana umuhimu kwenye kutimiza ndoto zetu na kama umeshafahamu ni elimu gani itasaidia kufikia ndoto zako basi anza sasa kupigana mpaka uipate elimu hiyo.

Asante sana rafiki yangu nikutakie siku njema katika kuuanza mwezi huu mpya wa Julai.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0712161251/0763766944

No comments:

Post a Comment