Saturday, 20 June 2020
Udhaifu wa kuepukana nao.......
Rafiki yangu habari za wakati huu, bilashaka unaendelea vizuri,nikupongeze kwa kuendelea kujifunza kupitia ukurasa Wangu wa Ustawi wa fikra, hakikisha ufurahii tu kupata masomo haya hakikisha unachukua hatua za kubadilika, nimeona faida za kusoma vitabu nikajiambia sitokuwa Sawa nikipiga hatua peke yangu nikaamua kushiriki na wewe hivyo fanyia kazi mafundisho haya...........
Leo tutaangalia somo kutoka kwa wana falsafa wa kistoa, imeanza kuwa utamaduni kwangu Kila jumamosi kupitia mafunzo haya na hakika kama unahitaji utulivu hii ndio falsafa bora sana ya kutupatia utulivu mkubwa sana,falsafa hii haitaki kujielezea kwa watu kwamba wewe ni mstoa, wala kuandika masomo ya kistoa bali kwenda kuishi kwa vitendo yale utakayojifunza.
Leo kutoka kwenye falsafa hii tutajifunza jambo ambalo wengi tuna udhaifu nalo mkubwa sana, Kila mtu hapendi kuitwa dhaifu, tunapenda kuonekana ni jasiri,pamoja na matamanio hayo kuna mambo mengi tunayafanya tukiamini yanatufanya tuonekane jasiri kumbe ndio tunazidi kuwa dhaifu.
Hatuko tayari kuambiwa wazi wazi makosa yetu, hapa wana falsafa hii wanasema huu ni udhaifu mkubwa sana kwetu binadamu tulio wengi, tunapoambiwa makosa yetu lazima tutaanza kuangalia namna ya kujitetea na wakati mwingine kuwa tayari kuingia kwenye ugomvi na yeyote ambaye atatuonyesha makosa yetu wazi wazi.
Unaweza kuona wewe huna udhaifu huu lakini jiulize ni lini na nani alikukosoa na kukuonyesha makosa yako? Kama hakuna anayekukosoa je ni kwamba Kila unachofanya ni sahihi? Kama siyo sahihi basi inawezekana watu wamekuacha au umezungukwa na watu wasio sahihi, watu wa chini sana na ndio maana hawako tayari kukueleza ukweli pale unapokosea.
Mstoa Marcus Aurelius yeye alikuwa anatenga muda wa wa kuwashukuru watu walio mkosoa waziwazi na hilo lilimfanya awe jasiri zaidi na kuwa imara zaidi, hivyo rafiki kama unakasirika na huna mtu wa kujaribu kubeba ujasiri wa kukueleza makosa yako basi tambuwa una udhaifu mkubwa sana na hilo ndilo linalokufanya usipige hatua kwenye maisha yako, kwani watu wanaona makosa yako wazi wazi na hawapo tayari kukukosoa kwasababu wanafahamu hutokubaliana nao na wewe unaendelea kuamini akili yako iko sahihi kumbe wakati mwingine akili yako inakudanganya na kukufanya kuendelea kurudia makosa.
Asante sana rafiki yangu,nakupenda sana na sitoacha kushare upendo Wangu kwa kukuletea kile ninachojifunza,fanyia kazi haya na Nina hakika hutabaki kama ulivyo Leo.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944/0712161251
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment