Wednesday, 10 June 2020

Hivi ndivyo unavyoweza kujifungua na vifungo ulivyojifungia kwenye maisha yako na kuwa huru tena.........



Rafiki wale wanao amini kwenye ushirikina na uchawi huwa wanayo imani kwamba kuna binadamu anaweza kufunga au kuchukua nyota zao, hivyo hutembea kwa waganga wa kienyeji ili waweze kuludishiwa nyota zao. Haya yote yanatokana na uelewa mdogo wa namna gani unaweza jifunga au kujiweka huru na kifungo kupitia imani ulizonazo mwenyewe.........

Wiki zilizo pita tuliweza kuona namna shauku na imani zilivyo na nguvu kuamua hatima za maisha yetu na mwandishi wa kitabu cha THINK AND GROW RICH anatuambia, pale tunapokosa imani tunakua na hali ya kutojiamini na kutojiamini kuna tujengea  hofu na hofu ndio kitu kinachotuangusha sana.Leo tutaangalia hatua tano za kutujengea kujiamini.

Kabla hatuja angalia hatua hizo tano tunapaswa kuelewa kwamba jamii inao mchango mkubwa sana wa kutujengea hali za kutojiamini, hebu jiulize kwenye familia yako Mtoto anakemewa Mara ngapi kwa siku pale anapojaribu kufanya vitu tofauti tofauti? Je kufokewa huko kunakwenda sambamba na pongezi? Shuleni je? Makazini nako? Sasa twende tuone namna ya kujijengea hali ya kujiamini kwenye maisha yetu.

Mwandishi anaita FIVE SELF CONFIDENCE FORMULA.
1.Jiambie "Ninafahamu ninao uwezo na nafsi yangu itaweza kuvumilia na nitaendelea kuchukua hatua mpaka nitakapo pata ninachotaka.

2.Mawazo ninayotengeneza yatakua kweli,na Kila siku nitaweka picha ya kile ninachotaka kwenye mawazo yangu mpaka kitimie.

3.Kujiamini kutaniwezesha kufikia kile ninachohitaji na Kila siku nitajijengea kujiamini.

4.Kwa kua nimeshajiwekea lengo na dhumuni sitoacha kujaribu Kila namna mpaka nilifikie.

5.Ukweli na haki ni msingi kwenye utajiri Wangu, hivyo kama biashara ninayofanya haiwafaidishi wengine sito ifanya, wivu, chuki, majungu na ubinafsi havitakua na nafasi kwenye maisha yangu na nitawapenda binadamu wote kwani mawazo hasi dhidi ya wengine havita niletea mafanikio.

Baada ya kuandika hatua hizo tano mwandishi anasema weka sahihi na Kila siku rudia kusoma hatua hizo na hali ya kujiamini itajengeka na hapo utakua umejitoa kwenye hofu na kutoogopa changamoto yoyote.

Your are "the master of your fate, the captain of your soul" because we have the power to control our thoughts.

Hakuna yeyote anayeweza kutawala uwezo wako wa kufikiri hivyo kwa kutambua hilo unaweza kua vyovyote vile unavyotaka, tambua hilo na litumie rafiki yangu.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment