Monday, 29 June 2020

Tiba ya pili inayokwenda kutunisha mfuko wako ulio sinyaa....


Rafiki yangu habari ya siku hii nyingine, hongera kwa kuweza kuwa miongoni Mwa watu wenye bahati ya kuweza kuifikia siku hii, nina imani Zawadi hii huwezi kubali ikapotea bila kufahamu umefanya nini,Panga na hakikisha unakwenda kukamilisha yote uliyopanga kutekeleza kwenye siku hii..

Leo tunaendelea na uchambuzi wa kitabu chetu cha The richest man in the Babylon na kwa wiki kadhaa tumejifunza mambo mengi sana ambayo nina amini ueyafanyia kazi kabla masomo hayo hayajapoa, Leo tunakwenda kuangalia Tiba nyingine ambayo tunajifunza kutoka kwa Tajiri Arkadi baada ya kuona tiba ya kwanza ya KUANZA KUTUNISHA MFUKO WAKO KWA KUTUMIA SEHEMU TISA KATI YA KUMI NA MOJA KUIWEKEZA, baada ya kufundisha tiba hii ya kwanza mtu mmoja alimuuliza ninawezaje kutenga sehemu hiyo wakati kipato ninachokipokea ni kidogo na hakitoshi hata kwa matumizi muhimu?

Ndipo Arkadi akawajibu kwa kuwauliza swali, Je ni wangapi ambao jana walikuwa na mifuko iliyosinyaa? Karibu watu wote waliopo ukumbini walinyoosha mikono, basi akawaambia kwa kuwauliza inawezekanaje watu wote humu muwe na mifuko iliyo sinyaa wakati mnafanya kazi tofauti tofauti na mna vipato visivyo fanana?

Hapa tunapata funzo kwamba, waajiriwa huwa tunatabia ya kuongeza matumizi kadri  kipato kinavyoongezeka, ndio maana anayepokea million moja, laki tano na hata kipato kidogo cha laki moja bado inapokaribia na siku anayopokea tena kipato hicho huhakikisha kipato cha mwanzo kimekwisha, hili hata kwa mtu mmoja unaweza kukubaliana na hili, kuna miezi unapata fedha nyingi tofauti na kawaida lakini unazitumia zote na pengine kabla ya kupokea zingine utahakikisha zile za mwanzo umezimaliza, hii yote ni ile nguvu ya tamaa ya kutumia tuliyo nayo.

Baada ya kuwapa ufafanuzi huo Arkadi anawafundisha tiba ya pili ya kutunisha mifuko yako iliyo sinyaa ni DHIBITI MATUMIZI YAKO, haijalishi unapokea nini lazima ujidhibiti kwenye kutumia kipato hicho kwani hayo matumizi unayo yaona ni muhimu hukua kadri kipato chako kinachoongezeka. Hivyo anza kudhibiti matumizi yako.

Mwandishi anafananisha tamaa ya kutumia kipato tunachopokea na magugu yasiyo pandwa shambani, kama hayatadhibitiwa yataendelea kukua na kuathiri mazao yaliyopo kwenye Shamba hilo, hivyo anza sasa kutengeneza bajeti yako kwa Tisa ya kumi na hiyo moja inayobaki hakikisha unaiweka kwa ajiri ya kukikuza kipato chako. Fahamu matumizi muhimu kweli na yapi siyo muhimu na ondokana nayo Mara moja.

Rafiki yangu asante na nikutakie utekelezaji mwema kwa haya unayojifunza hapa yatakufikisha sehemu fulani ya juu tofauti na ulipo sasa, nakupenda na nakutakia siku njema.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment