Saturday, 27 June 2020

Namna pekee ya kukaa na watu wenye akili.......



Rafiki yangu kile unachoambatana nacho ndicho kitakachoamua hatima yako, Kama unaambatana na watu wajinga huwezi kuwa mbali na ujinga,na kama ukiambatana na watu wenye akili na uwezo mkubwa wa kufikiri basi na wewe utajifunza na kuwa na akili kubwa, siyo kitu rahisi sana kuhitaji kukutana na watu wenye mafanikio makubwa ili ujifunze kwao, Leo huwezi kusema kesho nahitaji nikutane na bakheresa na ukakutana naye akufundishe nini ufanye ili ufanikiwe kama yeye, hilo litakuwa gumu kwako, lakini ipo njia rahisi ya kukutana na watu kama hao na kuzungumza nao, Bilgate na matajiri wakubwa utakutana nao kwa njia hii ambayo nakwenda kukuambia hapa chini......

"Going straight to seat of intelligence"That's what books are"-Epictetus.

Kama unahitaji kufanikiwa kweli na kuwa na uwezo mkubwa kiakili,kama unataka kukaa seat moja na watu waliofanikiwa basi lazima ufuate upande wa vitabu, jijengee tabia hii ya kusoma vitabu na utakutana na wote waliofanikiwa na watakufundisha nini walifanya wakafikia mafanikio hayo na muda si mrefu utajifunza na kufanikiwa kama utatekeleza ulicho jifunza.

Rafiki labda nikupe shuhuda ndogo kwangu, kabla sijawa na utaratibu wa kusoma vitabu na kujiunga na kisima cha maarifa niliungana na wenzangu kwamba mshahara ni kidogo na hautoshi, hili ni kweli lakini njia pekee niliyoona kwa kipindi hicho ni kukaa kusubiria serikali waniongezee mshahara, kukaa na kuilalamikia serikali ikawa ndio kitu nilidhani ni sahihi, mwishoni Mwa mwaka wa 2017 nilianza kujifunza kupitia Amka Mtanzania ambapo nilijifunza bure na kuanza kuona hali ya kulalamika na kubeba jukumu la maisha yangu likabaki kwangu, mwaka 2018 mwanzoni niliweza kulipa ada na kuwa mwana kisima cha maarifa, hebu fikiria kutoka kutoweza kukutanisha mshahara na mshahara mpaka kufikia hatua ya kuwekeza karibu nusu ya mshahara Wangu sasa na mshahara huo haukuongezwa hata shilingi kumi tangu mwaka huo wa 2018 mpaka sasa lakini nimeacha kulalamika na nina imani kubwa ya kufikia ndoto zangu. Hii ndio nguvu ya vitabu kwenye maisha yetu.

Leo wakati napitia kurasa za Kila siku za ustoa nikakutana na kichwa cha habari kinachosomeka hivi "Why did the slave masters hide their money in books?" Hili likanifanya niendelee kusoma na ndipo nikakutana na kisa kimoja cha kocha wa mpira wa kikapu (basketball) aliyeitwa GEORGE RAVELING aliyeulizwa swali hilo la kwanini wamiliki wa watumwa (slave masters) wanapenda kuficha fedha zao kwenye vitabu?

George anamjibu bibi yake hafahamu ni kwanini ndipo bibi anampa sababu "because they knew slaves wouldn't open them" akimaanisha kwamba kwasababu watumwa hawapendi kufunguwa vitabu na kusoma.

Hivyo rafiki kama unataka kuondokana na utumwa wa fedha, utumwa wa ujinga, utumwa wa ajiri na manyanyaso kazini, utumwa wa fikra zako, utumwa wa hisia zako basi anza kujenga Tabia ya kusoma vitabu,hili litakupa Uhuru wa kutumikia wengine kwani u dhaifu na mtumwa kwasababu umekumbatia ujinga na hutaki kujifunza, kama utaruhusu siku yako ipite bila ya kusoma kurasa kadhaa za vitabu basi tambuwa unakumbatia ujinga na rafiki wa ujinga ni utumwa, hivyo kama unahitaji kufahamu utapataje vitabu vizuri vya kusoma basi wasiliana na Mimi na ukiweza kujiunga na kisima cha maarifa utapiga hatua kubwa sana kwani utazungukwa na watu sahihi. Nakupenda na nakutakia siku njema.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment