Friday, 7 February 2020
Haya apa makosa kumi umekuwa unafanya na yamekuchelesha.
Rafiki yangu mshukuru mungu kwa kuweza kupata nafasi ya kusoma makala hii muhimu kwenye page hii ya USTAWI WA FIKRA itakayokwenda kubadilisha namna ya kufikiri kwako, Nina amini ukisoma na kufanyia kazi lazima maisha yako yabadilike na utapiga hatua za kukutoa hapo ulipo na kukufikisha hatua ya juu kimaendeleo,imani hii inatokana na ukweli kwamba hata Mimi yamenitoa sehemu moja kunipeleka sehemu nyingine bora zaidi.Karibu tuwe sote....
Rafiki kabla hatujakwenda kuangalia maeneo hayo kumi utakubaliana na Mimi kwamba namna ya kufikiri kwetu ndio kunaleta shida kwenye maisha yetu, hivyo kwa kujifunza na kubadilisha namna ya kufikiri na kuamini ndio kunaweza kutuimarisha kuwa bora zaidi, sasa karibu ujifunze makosa kumi ambayo umekuwa unafanya kwa kujuwa au kutofahamu na yamekuwa yakikuangusha sana.
1.Eneo la kwanza ni hufahamu kusudi la maisha yako.
Rafiki yangu safari yoyote inaanza kama anayesafiri anafahamu ni wapi anakoelekea. Sasa kama mtu hajuwi kusudi la maisha yake na kwamba nini anataka na nini hataki basi hawezi fika popote kwenye ulimwengu huu wenye Kila kitu, kama unataka kufanikiwa basi juwa nini kitafanya ufanikiwe na kifuate na siyo Kila siku unakimbizana na fursa, Leo umesikia ufugaji upo,kesho umesikia kilimo unaacha kufuga na kuanza kilimo, huko ni kutojuwa kusudi la maisha yako.
2.Eneo la pili ni kulalamikia wengine kuwa sababu ya kushindwa kwako.
Ni kawaida kabisa kumkuta mtu akisema ni kwasababu sikupelekwa shule nzuri na Wazazi ndio maana maisha yangu yamekuwa ya shida,sababu Mimi ni yatima,Kwasababu serikali imegoma kuongeza mshahara, kama unatabia ya kulalamikia wengine basi tambuwa hutokosa na ndio utazidi kutofanikiwa, werevu wote uanza kuona tatizo ni wao hivyo hurekebisha kasoro zao na kupiga hatua.
3.Kuamini kwamba huwezi kufanya biashara kwani huna mtaji na biashara ndogo hazitakufikisha popote hivyo siku zote una amini utaanza biashara kwa kukopa au kwakuwa na hela nyingi ni kujichelewesha na hata ukipata hizo fedha nyingi biashara itakushinda na utakata tamaa ya kufanya biashara, anza na kidogo kisha kikuze ni njia nzuri ya kujifunza.
4.Kosa la nne ni kuona fahari kuwasaidia ndugu zako kifedha badala ya kuwapa elimu ya namna ya kupata fedha na wakajitegemea,kuna wangapi walikuwa msaada kwa ndugu zao na walipoanguka ki uchumi na familia zao zikaanguka? Kama ni Wazazi kijijini wape miradi ya kuku wafuge kuliko kuruhusu wakutegemee Kila siku watakunyanyua pale utakapoanguka. Hawahitaji msaada wa fedha wanahitaji mawazo ya kuwafanya wapate fedha na wajitegemee.
5.Kosa la tano unalofanya ni kukosa elimu ya fedha.
Rafiki hata kama umesomea uchumi, umesoma sana nikuambia kitu kimoja bado huna muelewa mpana wa mambo ya fedha, eneo la uwekezaji,akiba, mikopo mizuri na mibaya na fursa unazoweza kuziona bado hujaambiwa kwa elimu ya darasani kama unahitaji vitabu vizuri vitakavyo kuelimisha namna ya kukua kifedha.
6.Kuishi maisha bila bajeti.
Eneo hili linawatesa wengi sana, watu wananunua vitu kwa tamaa, hawapangi bajeti, hivyo ujikuta Kila siku kwenye madeni kwasababu hununua vitu wasivyovihitaji kwa pesa ambazo hawana.
7.Eneo la saba ambalo linakurudisha nyuma ni kuishi kwa kujifananisha na wengine.
Hapa rafiki panawatesa wengi, watu wamekuwa hawajipi maisha ya furaha kwasababu wanaishi viwango visivyo vyao,jirani kapeleka Mtoto shule nzuri ya gharama na Mimi nitakopa mwanangu aende shule nzuri, hivyo hujikuta kwenye msongo wa mawazo bila sababu.
8.Eneo lingine ambalo wengi linatutesa ni kufanya maamuzi kwa hisia;
Sisi binadamu tunapaswa kufanya maamuzi kwa kufikiri na siyo kwa hisia lakini Mara nyingi tunazipa hisia nafasi ya kutuamulia na hivyo kujikuta tukijutia maamuzi yetu,watu wanafahamu vyakula vinavyowaletea matatizo ya afya lakini wanaendelea kula kwa mazoea.
9.Eneo lingine ambalo tunakosea ni kuruhusu watu wanaotuzunguka wawe washauri wetu.
Ni kawaida kwetu binadamubinadamu kuamini watu wa karibu kutushauri kwa mambo ambayo hawana uzoefu nayo, mambo ya fedha muone aliyefanikiwa kifedha atakushauri, mambo ya afya muone alibobea kwenye afya na siyo kupokea ushauri kwasababu ni ndugu au Wazazi.Kama unataka ushauri wowote nitakuunganisha na mtu sahihi karibu.
10.Kuamini kupata elimu ya darasi kutaamuwa hatma ya maisha yako.
Kizazi cha sasa kinawaza sana kwenye kuajiriwa kuliko kujiajiri, hivyo wasomi hukaa wakiamini na kusubiri ajira ambazo hazipo na kuweka maisha yasubiri wakati fursa zipo kibao Swala ni kuamka na kuzichangamkia.
Rafiki hayo ni maeneo kumi ambayo umekwenda nayo yamekuangusha,weka kazi na nidhamu binafsi na muda yafanyie kazi hayatakuacha hapo ulipo.
Makala hii imeandikwa na Mimi Mwl.Kelvin Kinyaga.
Nataka tufike wote juu usiache kufuatilia page hii Kila jumamosi. Asante sana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment