Saturday, 15 February 2020

Muda huu usigawe kwa wengine hata kama wanaununua kwa mabilion ya shilingi......

Rafiki hongera kwa kuendelea kuwa nami kupitia page yangu, bilashaka unaishi kusudi la maisha yako ndio maana huachi kujifunza, washindi wote wanafahamu siri ya ushindi ni kujifunza na kuweka kwenye matendo, karibu tuwe sote.......

Rafiki Kila mmoja wetu ni mshiriki wa kuuza au kununua kwa namna moja au nyingine na wote tunategemeana kwa namna moja au nyingine,wa kuuza anamtegemea wa kununua na wa kununua anamtegemea wa kuuza na hayo ndio yanaleta ladha ya maisha, pamoja na kutegemeana huku bado kuna upande una nufaika zaidi ya upande mwingine hasa kwenye kuuza au kununua muda.

Je wewe unauza au una nunua muda?
Pengine unaweza ukaanza kujiuliza ni duka gani linalouza muda? Na Je na nunua au nauzaje? Rafiki kwanza tukubaliane kwamba mungu ametugawia muda kwa usawa bila kumpunja yeyote, wote tuna masaa 24.Sasa swali unalotakiwa kujiuliza ni hayo masaa 24 unayatumia kwa ajiri yako au wengine? Kama ni kwa ajiri ya wengine ni masaa mangapi unatoa kwa ajiri ya wengine na mangapi unatoa kwa ajiri yako? kuuza Masaa yote kwa mtu ni tatizo na kutumia masaa yote kwa ajiri yako mwenyewe ni tatizo lazima ujifunze kuuza na kununua muda wako.Je ni wangapi wameuza muda wao kwa Bakresah,hivyo muda mwingi hufanya kazi na kutumia ujuzi wao kwa manufaa ya bakresah? Hili siyo ninalotaka kukuambia rafiki au nataka kukukataza usiuze muda wako, pengine umeuza kwa serikali endelea kuuza kwani mwanzo lazima uuze halafu baadaye utaanza kununua lakini yapo masaa ambayo hutakiwi kuuza Je unataka kuyafahamu masaa hayo? Na ni kwa namna gani yatakufikisha kilele? Karibu.....

Muda huu usiuze kwa yeyote.
Rafiki haijarishi unakouza muda wako unalipwa shilingi ngapi lakini bila kutumia muda kwa ajiri yako mwenyewe hutayafikia mafanikio ya juu. Muda huo ni saa moja mpaka mawili baada ya kuamka na saa moja mpaka mawili baada ya kutoka kwenye shughuli zako za kipato kikuu,masaa ya asubuhi yatumie kuipangilia siku yako na namna utaiendea siku hiyo na yapi utayafanya kwa viwango vya juu kwa utoafauti na ulivyofanya Jana,maana usitarajie kupata matokeo tofauti kwa kufanya kitu kilekile na kwa namna ile ile. Masaa mawili na zaidi yatumie kwa ajiri yako, kwanza tathimin siku yako uliyoimaliza imemalizikaje? Yapi umefanya sahihi na yapi umekosea? yapi umekamilisha na yapi hujakamilisha na jipe sababu sahihi za kutokamilisha, nasema sababu sahihi kwani nafahamu mwili utakavyokupa sababu za kizembe zitakazo kubakiza ulipo bila kupiga hatua yoyote na hapa mwanafalsafa EPICTETUS ana tuambia;

"Allow not sleep to close your are aried eyes, until you have reckoned up each day time deed:"where did I go wrong? What did I do?and what duty's left undone?From first to last review your acts and then reprove yourself for wretched (or cowardly) but rejoice in those done well" Discourses 3.10.2.2-3.

Hayo yote yanatupa umuhimu wa kutoimaliza siku yako bila kujifanyia tathimini mwenyewe, wengi uuza muda wao kwa masaa mengi kwa hela kidogo na masaa baada ya kuwafanyia kazi walio nunua muda hutumia masaa yaliyobaki kustarehe na pesa ambazo wakati mwingine siyo zao, wamekopa na kuendelea kuwa na mfumo huo siku zote, hivyo rafiki usikubali kuingia kwenye mtego, pangilia mchezo wako wa kuuza na kununua muda lakini tenga masaa kwa ajiri yako.

Asante sana rafiki na uwe na siku njema.
Ni Mimi Mwl.Kelvin Kinyaga
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944.

2 comments:

  1. Nisahihi kabisa mr.kelvin kwa kutukumbsha kujua Thaman ya muda kwenye maisha yetu ya kila siku maana muda ndio kitu pekee ambacho kila mtu amepewa bila upendeleo hapa dunian awe tajir au maakin.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Asante sana rafiki, endelea kutembelea ukurasa huu Kila jumamosi, kuna mafunzo mengi mazuri kwa ajili yako.

      Delete