Friday, 20 March 2020
Unapokosa majibu ya maswali uliyo nayo ndipo unapohitaji mtu huyu.......
Habari za muda huu rafiki yangu, bilashaka umesoma na kutekeleza yote yaliyo kwenye makala ya Amani makirita inayosomeka WAKATI DUNIA INAFUNGWA WEWE FUNGUA VITABU........ Kama hujasoma usiendelee kusoma hapa nitafute nikutumie usome kwanza kisha utakuja kumalizia.
Rafiki yangu sisi binadamu ni viumbe wa kuhoji, viumbe wa kutaka kujuwa sababu kwanini jambo fulani limetokea na hapa penye kwanini zako ndipo penye mafanikio au kushindwa kwako, unaweza pata sababu sahihi au usipate sababu sahihi na wakati mwingine ukabaki njia panda usijuwe nini cha kufanya.
Upo usemi mmoja unasema hivi "WANAOLETA MABADILIKO SIYO WENGI BALI WACHACHE WENYE MSIMAMO" huku usemi mwingine wa kingereza unasema hivi "Every generation needs someone hero to answer their questions" misemo yote hii INA maanisha mabadiliko ya kweli hayaletwi kwa kuangalia kile anachofanya Kila mtu Bali kwa kuangalia mashujaa ambao ni wachache wanafanya nini, rafiki unayo maswali mengi sana. Na majibu mengi sana yasiyo sahihi na umeanza kukata tamaa, hapa ndipo unapotakiwa kupata mtu sahihi wa kujibu maswali yako yote kwa usahihi, umekuwa hufahamu kwanini ni masikini?kwanini hupati kazi na umesoma una elimu kubwa? Kila ukianza biashara inakufa? Basi Mimi nitakukutanisha na mtu sahihi ila anza kufanyia kazi kauli hii.
EVERYTHING THAT IS HAPPENING AT THIS MOMENT IS A RESULT OF CHOICES YOU'VE MADE IN THE PAST-DEEPAK CHOPRA.
maamuzi yako ya siku za nyuma ndio sababu ya yale unayopitia Leo, Je yalikuwa sahihi? Basi yanaweza boreshwa na kuwa bora zaidi na shujaa wa kujibu maswali yako na yakafanya Leo uamue sahihi ujishukuru kesho ninamfahamu hivyo Fanya mawasiliano nami nitakuonyesha shujaa wa kizazi chetu na utanishukuru siku moja.
Uwe na siku njema, siku ya kumfahamu shujaa wa kizazi chako ili alete mabadiliko chanya kwenye maisha yako.
Makala hii imeandaliwa na Mwl.Kelvin Kinyaga.
Mpenzi na mtu anayeamini kwenye vitabu na uandishi.
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment