Sunday, 29 March 2020
Tatizo lako siyo tatizo, bali hujuwi tatizo ni nini?....
Rafiki yangu habari za wakati huu, Nina hakika kwa wiki nzima umetatua mambo mengi na umesababisha mengi yanayo Fanya dunia yetu kuwa sehemu bora sana ya kuishi, na hii ndio maana ya wewe kuishi, na je unaogopa Corona,kifo au kutokuishi? Maana wapi wanaogopa corona kwa kuhofia kifo kumbe walishakufa siku nyingi wanasubiri kuzikwa tu, kama umekata tamaa na changamoto unazopitia basi umeshakufa subiri siku uzikwe tukusahau,tunachopaswa kuogopa ni kutokuishi pekee na siyo kitu kingine chochote. Karibu tuwe wote......
Rafiki yangu utakubaliana na Mimi kabisa kwamba kama hujuwi tatizo ni nini huwezi litatua tatizo hilo, sababu tatizo litakuwa ni kubwa kuzidi wewe, hapo ndipo Kila siku utajipa sababu nyingi zisizo sahihi na kuona mambo hayawezekani, Leo nataka nikuambie matatizo yako yote yanaanzia kwenye sehemu inayoitwa MAARIFA SAHIHI,siku utakapopata maarifa sahihi kuhusu Fedha ndio utafahamu tatizo halikuwa fedha Bali tatizo ni maarifa yanayohusu fedha,siku utakapopata maarifa sahihi kuhusu mafanikio ndio utajuwa tatizo siyo utajiri,siku utakapo pata maarifa kuhusu biashara ndio utafahamu tatizo siyo ugumu wa biashara ila hukuwa na maarifa ya namna ya kufanya biashara, Je tatizo ni madeni yamekuandama? Tatizo siyo kipato unachopata ila tatizo ni maarifa ya namna ya kutumia kipato chako ili kufikia Uhuru wa kipato, Je rafiki yangu wewe tatizo lako ni nini? Una maarifa sahihi kuhusu tatizo hilo? Amini hakuna jambo lisilo kuwa na ufumbuzi hivyo ukiona unapitia changamoto yoyote ile basi fahamu kuna sehemu hapako Sawa na kama unataka kuondokana na tatizo hilo tuwasiliane nitakuonganisha na mbobezi wa eneo linalokutatiza kwani kupitia Club yetu ya KISIMA CHA MAARIFA kuna tiba ya Kila ugonjwa unaokusumbuwa, biashara,fedha,mahusiano,sheria na mengine mengi, asante na uwe na siku njema rafiki.
Nenda kajiulize Leo nini tatizo? Je una maarifa sahihi kwenye hilo tatizo?kisha chukuwa hatua sasa huna haja ya kuendelea kulalamika.
Ni Mimi Mwl.Kelvin Kinyaga mtu ambaye Nina amini katika maarifa sahihi kunikombowa, karibu tuwe sote.
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment