Sunday, 5 April 2020

Umri siyo kipimo cha ukubwa bali uwezo wa kufurahia matatizo na changamoto zako......



Rafiki yangu karibu tumalizie wiki pamoja,napenda tufunge juma pamoja ili tunapoanza wiki lingine tuwe na nguvu mpya za kukabiliana na magumu yaliyo mbele yetu.Kama unaweza kusoma hapa sina shaka ni miongoni Mwa watu wenye bahati sana....

Rafiki yangu miaka mitatu iliyopita kabla sijaanza kuishi maisha yangu nilikuwa miongoni Mwa watu ambao ni wengi lakini wanao ishi maisha ya maigizo, maisha ya majirani na maisha yasiyo eleweka, tabia ya mtu wa maisha haya ni mtu anayelalamika kwa jambo lolote lile, nilikuwa natamani maisha ya waigizaji wenzangu, maisha ya kutamani kuwa mbali na changamoto,maisha ya kutaka vitu vitokee bila jasho kwa kujiambia ukishasoma basi mengine yote ni akili yangu tu.

Mwanafalsafa Seneca aliwahi kusema hivi;

"
NO MAN IS MORE UNHAPPY THAN HE WHO NEVER FACE ADVERSITY.FOR HE IS NOT PERMITTED TO PROVE HIMSELF"

Kauli hii inatukumbusha umuhimu wa kuona changamoto na matatizo kama daraja la kutuvusha kutoka chini kwenda juu na kadri unavyopata matatizo na changamoto ndogo ndivyo unavyokosa furaha na ndivyo unavyojizuia kufika mafanikio ya juu. Na ndio maana unapoanza kufanyia mafunzo ya fedha unaona changamoto zinaongezeka, unalipwa fedha kidogo na unatakiwa uipunguze uiwekeze na usikope hivi ni vitu ambavyo siyo rahisi kama hujuwi umuhimu wa changamoto kwenye mafanikio.

Rafiki kauli ya kuondoka nayo Leo ni hii inayosema hivi;
       "Kama sina changamoto,sina maisha na nimuigizaji wa maisha"

Ni Mimi Mwl.Kelvin Kinyaga, mwandishi na muhamasishaji wa maarifa sahihi kupitia blog yangu ya http//kinyagakelvin.blogsports.com
0763766944
Asante na siku njema.

No comments:

Post a Comment