Friday, 17 April 2020

Tofauti ya kupenda na kuhitaji ndio itaamua ufike wapi......



Rafiki siyo Mara ya kwanza kukuambia siku hii umepewa kama Zawadi, Leo unaweza kuanza kunielewa nini nilikuwa ninamaanisha, hizo idadi za vifo unavyovisikia nisehemu ndogo sana, labda nikuulize kitu kimoja, tangu gonjwa hili la corona limeingia nchini vifo vingapi vimetangazwa? Je wangesema watangaze idadi ya wote waliokufa si utakubaliana na Mimi idadi hiyo ni ndogo sana, unafahamu kuna watu zaidi ya 20 wamekufa kwa Mara moja kwenye ajari? Pengine nao walikuwa wanawaza corona lakini hawajaondoka kwa corona, yote nayaandika lengo lisiwe kukutisha Bali kukufanya uishi kusudi na kuacha kujidanganya na kesho, kesho ni mbali kuliko siku zote, nenda kakamilishe yote uliyojipangia.

Rafiki na mwanamafanikio mwenzangu, sisi binadamu ni viumbe wa kupenda,Kila mmoja wetu vipo anavyovipenda,pengine ni kuangalia TV,pengine ni starehe,pengine ni kusoma vitabu, Pengine ni kuangalia mpira na vingine vingi, lakini wapo watu wanapenda vitu wanavyovihitaji pia,mfano mtu anapenda kufanya biashara na anahitaji biashara ili kuweza kufikia ndoto zake, hivyo mtu huyu kuyafikia mafanikio inakuwa rahisi sana kwani anapenda kile anachokihitaji,sasa tuchukulie mtu ambaye anaghairi kufanya kazi ili akatizame mpira, Je kupenda kwake kutizama mpira kuna mpa mahitaji yake?fedha na chakula anapata kwa kutizama mpira?

Hivyo nini unapaswa kufanya?
Usifanye kitu chochote kwasababu unakipenda bali jiulize ninakihitaji? Na siku zote anza na vile unavyohitaji kama kwa wakati mmoja hujuwi nini cha kufanya.

Jitaidi kujihusisha na vile unavyovihitaji na uvipende hivyo kwanza, nahitaji mafanikio na napenda kusoma vitabu na kujifunza na kubadilika, hapo hakuna wa kunizuia kufanikiwa.

Rafiki kwa Leo ni hayo machache,andika yote unayopenda na jiulize kama ndio unayohitaji halafu utaona ni nini unaweza kufanya.

Fungua kiungo https://Kinyagakelvin.blogspot.com na utajifunza zaidi, kuna masomo mengi yatakayo kuongoza kwenye safari yako ya mafanikio.

Imeandikwa na Mwl.Kelvin Kinyaga
Kinyagakelvin162@gmail.com
0763766944

No comments:

Post a Comment