Sunday, 26 April 2020

Changamoto na matatizo yao siyo wanayokuambia, usikimbilie kutoa ushauri wako......



Rafiki yangu nakuita mwanamafanikio kwasababu Nina amini unalo kusudi ambalo unalifanyia kazi na Kila siku unapiga hatua kuliendea na ndio maana unasoma hapa, hivyo nikusihi usiishie hapa bali endelea kusoma mpaka mwisho na kuna kitu utaondoka nacho, karibu........

Rafiki yangu nina amini kwamba zipo changamoto nyingi unazipitia lakini Leo nataka tujadiliane kwa pamoja changamoto ya kuombwa kutoa ushauri, kuombwa msaada na watu wetu wa karibu ambao huna namna ya kuwakwepa kwa namna yeyote ile, na wakati mwingine umekuwa ukijaribu kuwasaidia lakini matatizo yao ni yale yale na inafika sehemu unahisi kuchoshwa nao, rafiki usichoshwe na hilo kwani rafiki yako nipo nitakuambia dawa ya tatizo hilo. Kabla hatujaenda kuangalia ki undani namna ya kutatua hili tuone shuhuda kutoka kwa rafiki yetu huyu.

"Nimechoshwa na tabia ya Mzazi wangu kuomba hela Mara kwa Mara na nikijaribu kumuanzishia biashara haidumu na anaendelea kuomba hela nashindwa nifanyaje ili nimsaidie"

Kama tunavyoona changamoto inayomkumba rafiki yetu, hapa ni Mzazi na huwezi sema unampotezea lazima umsaidie na shida ni vipi unamsaidia, kwanza kabisa kwa mtu huyu ni yeye mwenyewe alimtengenezea tabia Mzazi wake ya kumpa hela na chochote anachohitaji na inafika sehemu hawezi tena kumsaidia kwa kiwango cha kumridhisha Mzazi wake, hapa ni kwamba aliamini changamoto kwa Mzazi wake ni fedha kumbe si kweli, Msemo wa usimpe mtu samaki bali mfundishe namna ya kuvua samaki ndio unajidhihirisha hapa,kwa changamoto na matatizo yanayowakabiri wengi hasa watu wa karibu ufumbuzi wake siyo kuwatimizia wanachohitaji moja kwa moja kabla ya kupata suruhisho la kudumu.

Wiki hii nilikuwa napitia makala za ustoa ndio nikakutana na sababu nne zinazopelekea watu kupitia changamoto nyingi, pengine ulikuwa huzifahamu au unazifahamu na hukujuwa kama zina nguvu kubwa, zitumie kwako na kwa yeyote anayekuomba ushauri.

1.When we wake up
Rafiki kama hili ulikuwa unalichukulia pouwa basi unajidanganya,muda wa kuamka ni muhimu sana kwenye maisha yetu.

2.What we study and practice
Kujifunza na kusoma vitabu ni maisha, hivyo kama hakuna unapojifunza huna maisha.

3.Who we have in our lives as influences
Rafiki kama unamshauri mtu na hufahamu msukumo wake unatoka wapi ni kazi bure, unamshauri mtu afanye biashara na hana kusudi la kufanya hivyo unampotezea muda wake na wako pia.

4.Where we go and how we spend our time.
Muda ni Mali hivyo kama unampa mtu ushauri halafu yeye hafahamu thamani ya muda ni kazi bure.

Mambo haya manne ni muhimu sana na kabla hujamshauri mtu kitu chochote angalia mambo hayo manne na ona kama unaweza kuwapa ushauri na kuwatengenezea tabia mpya kwenye mambo hayo kisha changamoto zao zingine zitaondoka, na ukiona unajohusisha na mtu anayepuuza vitu hivi vinne basi jiandae kuumia.

Makala hii imeletwa nami rafiki yako, Mwl kelvin Kinyaga;
Msomaji na mwana kisima cha maarifa;

Unaweza nipata kwa No.0763766944;
Email adress Kinyagakelvin162@gmail.com
Blog yangu https://kinyagakelvin162.blogspot.com ukifunguwa kiungo hiki utapata makala na mafunzo mengi. Asante sana.

No comments:

Post a Comment