Thursday, 24 September 2020
Fate leads the willing and drags along the reluctant - Seneca
Mungu watu ni mwema Sana kuweza kutufanya mimi na wewe kuifikia siku hii, siyo kitu rahisi kwani wapo wengi Sana walitamani na imeshindikana, Kwa kulitambua hilo basi tuanze siku yetu Kwa kufanya yale ya msingi na kuacha kuutumia Muda wetu Kwa mambo ya siyo na tija......
Leo tunaangalia kauli ya mwanafalsafa Seneca ambayo inatupa zoezi la kufanyia kazi kila siku Kwa wiki nzima.
Rafiki yangu pale unapoanza kushindana ndipo mwanzo wako wa kushindwa unapoanza kwani chochote unachoshindana nacho unakipa nguvu dhidi yako. Hata kama una nguvu kiasi gani lazima ukubaliane na matokeo kwamba huwezi lazimisha na kuwazuia watu namna wanavyokufikiria.
Wapo watu wengi wanaoteseka na historia za maisha yao, hutamani kubadilisha hali zilizojitokeza kwenye maisha yao, historia ya elimu yako siyo muhimu Kwa Sasa, hali yako mbaya ya kimahusiano iliyokutesa huko Nyuma usiipe nafasi leo.
Pale utakapoanza kuyakubali madhaifu yako na kuruhusu maisha yako yaendelee, huku ukiangalia ni wapi unataka kufika na kujitaidi kutimiza yanayokupeleka huko ndio unaanza kukua, kubali Kuna vingi hujui na Anza kujifunza Mara moja, wape watu nafasi ya kuishi wanavyotaka na wewe ishi maisha yako huku ukifahamu Kuna vingi huwezi vibadili na haviwezi kua vile unavyotaka wewe, kukataliwa, kusemwa na wengine,kukejeriwa na kudharaurauliwa ni vitu ambavyo havitakiwi kukuumiza kichwa, wewe jipe sababu ya kuendelea na maisha yako na kubali mengine yako nje ya uwezo wako vipokee na vikubali.
Makala hii imeandikwa na mimi rafiki yako Mwl Kelvin Kinyaga, unaweza nipata zaidi Kwa mawasiliano binafsi hapa chini.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogsport.com
0712161251 /0763766944
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment