Sunday, 27 September 2020
Unajifunza nini kwenye kisa hiki kifupi?
Habari za wakati huu rafiki, una maadui wengi Sana na adui yako mkuu ni yule unayemuona ukijitazama kwenye kioo, adui wengine ni mazoea na kutojifunza, hebu jiulize wiki hili la 39 tangu mwaka umeanza linakwisha umefanya nini? Je umejifunza nini?.......
Leo nataka tujifunze kitu kimoja ambacho kilinipa ujasili kwenye mambo mengine mengi Sana na yamenisaidia Sana.
Nimetoka nyumbani naelekea bank na nina uhitaji wa haraka na fedha ninazohitaji kutoa Kwa njia ya ATM kufika nakuta foleni ni ndefu na Kati ya ATM tatu ni moja tu ndio inafanya kazi bahati mbaya ilikua ni siku ya jumapili na bank zimefungwa siwezi tolea ndani na bahati mbaya habari ya mawakala haikuwepo Kwa wakati huo, wakati najiuliza nifanyaje nikajiuliza nani kasema hizo ATM mbili hazifanyi kazi? Nikagundua ni askari anayelinda hapo alikua akiwaelekeza watu kwamba hizo ATM mbili hazifanyi kazi Lakini Kwa wakati huo hayupo eneo la ATM bali yuko pembeni anaongea na mtu, Kwa sababu nilikua na haraka nilimuomba aliyekua nyuma yangu ngoja nikaangalie pengine mtandao umerudi na kama sivyo ningerudi kwenye foleni yangu, nilipofika nilikuta mtandao uko Safi na bahati nzuri na Ile ATM nyingine mambo yalikua hivyo hivyo,nikatoa fedha na kila mtu akashangazwa kwamba tumetumia ATM moja Kwa shida wakati ATM zote zilikua zinafanya kazi, rafiki pengine kwako tukio hili lisiwe na maana lakini kwangu lilinipa sheria.
KWANGU MWENYEWE
1.Nikiwa na shauku ya jambo lolote siangalii changamoto zilizopo mbele yangu bali kile ninachohitaji Kwa mbinu na gharama yoyote.
2.Asili itakuruhusu kukupatia unachotaka kama kweli kutoka moyoni unakihitaji.
3.Sikia lakini usiamini kirahisi thibitisha kile unachokisikia.
4.Acha kufuata wingi tumia njia zako.
ASKARI
Usiwaongoze watu kwenye jambo ambalo wewe mwenyewe hulifahamu ki undani na hujalisimamia ipasavyo.
Kama Kuna la Ziada umejifunza kwenye kisa hiki naomba unishirikishe Kwa njia yoyote Kati ya hizi hapa chini.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogsport.com
0712161251 /0763766944
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment