Sunday, 27 September 2020
Jipe majibu sahihi ya maswali haya
Hongera Sana rafiki yangu Kwa kuweza kupata bahati ya kuifikia siku hii, bilashaka uko tayari kwenda kupambana na mikiki mikiki ya siku, karibu tuendelee kujifunza kupitia maswali.......
Kabla hatujaangalia maswali ya kujiuliza nikuambie kitu kimoja, maswali ni njia bora Sana ya kujifanyia tathimini kwani yanakuonyesha uko wapi na unataka kufika wapi.
Karibu uweze kutenga Muda wako na kujipa majibu sahihi.
1.Je unaipenda kazi yako? kama sivyo ni kwanini?
rafiki ni wengi Sana wanafanya kazi wasizo zipenda lakini ukiwauliza sababu za kutopenda wengi watasema haziwalipi vizuri, je na wewe sababu ni hiyo?Je umepanga kuondoka lini kwenye kazi hiyo usiyoipenda? Au utaendelea na utumwa huo maisha yako yote?
2.Vipi ukijiangalia kadri unavyokua uwezo wako wa kujiamini unaongezeka au unapungua?
Fahamu hili na lifanyie kazi mapema.
3.Je unajifunza kutokana na makosa yako au unarudia makosa yaleyale kila siku?
4.Ni nani shujaa wako na unajifunza kwake na kila siku anakupa msukumo zaidi wa kuzifikia ndoto zako?
5.Una ndoto gani kubwa inayoeleweka? Kama ipo ni ipi hiyo? Na je ni mipango gani uliyo nayo kuifikia Naoto hiyo?
Rafiki kama utaweza kukaa chini na kujipa majibu ya maswali haya Kwa usahihi? Nina hakika Kuna sehemu unakwenda ila kama utaona unakosa majibu naomba tuwasiliane kwani nina amini utakua mwanzo mzuri.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogsport.com
0712161251 /0763766944
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment