Monday, 21 September 2020
Maswali ya kujiuliza unapotaka kukopa Kwa ajili ya kuanza biashara.
Hangera Sana rafiki yangu Kwa kuendelea kujifunza kupitia kurasa zangu za Ustawi wa fire, Leo tutakwenda kuangalia mambo ya msingi unayopaswa kuangalia kabla hujachukua mkopo ili kuanzisha biashara.......
Kwanza kabida unakumbuka tulijifunza kutoka kwenye kitabu cha Elimu ya msingi kuhusu fedha kwamba kukopa ili kuanzisha biashara no mkopo Mbaya. Leo tutajifunza Kwa kina kutoka kitabu cha THE RICHEST MAN IN THE BABYLON kama mkopeshaji fedha babeli anavyotufundisha.
Kwanza kabisa Kwa yeyote anayetaka kukopa au kukopeshwa lazima ajiulize maswali kadha ya msingi. Na zaidi kabla hujamkopesha mtu hakikisha unafahamu yafuatayo.
A. Fedha unazokopa/anazokopa kwako ni za nini?
B. Kama ni Kwa ajili ya kufanya biashara je unao uzoefu au ujuzi na biashara hiyo?
C. Je unafahamu ni wapi utanunua Kwa bei ndogo zaidi unachotaka kuuza?
D. Je unafahamu ni wapi unapoweza kuuza Kwa bei nzuri na na kupata faida?
Rafiki Kwa wakopeshaji na wakopaji huwa na matamanio ya kupata wanachotaka, mkopeshaji ana tamaa ya kupata riba na mkopwaji huwa na tamaa ya kupata fedha ili kukamilisha alichopanga kufanyia fedha anazokopa Lakini mwisho wa siku wote hujikuta kwenye matatizo makubwa ya kifedha.
Taasisi za kifedha wako makini Sana kwenye hili na ndio maana hutoa mkopo pale dhamana ya mkopaji inapokua kubwa kuliko mkopo uliochukua, hivyo nenda kalifanyie kazi somo hili,usimkopeshe wala kukopa na kujikuta badala ya kumsaidia unayemkopesha unamuingiza kwenye matatizo makubwa zaidi na wewe pia kupoteza fedha zako, Pima hatari za mkopo unaochukua au kukopesha ili kuleta usalama wako wa kifedha.
Asante na nikutakie siku Norma, ili kujifunza zaidi fungua
https://kinyagakelvin.blogsport.com
Kinyagakelvin162@gmail.com
0712161251/0763766944
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment