Monday, 19 October 2020

Yesu Kristof lango la ufalme wa mungu hapa duniani.

Rafiki yangu Habari za wakati huu, bilashaka ni mara nyingine zawadi ya pumzi inakaa ndani mwetu, huwezi amini ni maelfu ya watu Jana walikuwepo lakini leo ni wafu, tumshukuru mungu na tukaitumie zawadi hii Kwa kulitukuza Jina lake. Rafiki yangu swala la Imani linaweza kutugawa lakini utakubaliana na mimi kwamba hilo siyo kusudi la mungu, leo nikiwa ninakwenda kuzungumzia yesu kristo kama lango Kwa wakristo, bilashaka na ndugu zetu waislam mtume Muhammad ndiye lango, Kwa wakristo hatuwezi fika mbinguni Kwa kupuuza Jina Yesu Kristo, vivyo hivyo Kwa wenzetu waislam hawawezi kupuuza Jina Muhammad Kwa safari ya kutafuta mbingu ya mwenyezi mungu, hivyo tunatumia Milango tofauti lakini safari yetu ni moja. Kwa upande wetu wakristo Tunafahamu kwamba palikuwepo Adamu wa kwanza aliyemuasi mungu na hivyo Kwa sababu yeye alikuwa uzao wa kwanza, basi lilikua lango kwetu sisi wanadamu wote na ndio maana tunazaliwa na dhambi ya asili ambayo inaondolewa Kwa njia ya ubatizo kupitia Adamu wa pili ambaye ndie yesu kristo Masia mkombozi wa ulimwengu. "Mimi ndimi mlango;mtu akiingia Kwa mimi, ataokoka;ataingia na kutoka, naye atapata malisho. You 10:9." hapa yesu anatumia mfano huu kutuonyesha kwamba yeye njia ya wokovu Kwa watu wote wanaotamani kuingia kwenye ufalme wa mungu. "Yesu akamwambia, mimi ndimi njia, na kweli, na uzima;mtu haji Kwa Baba, ila Kwa njia ya mimi ". Yoh 14:6" Yesu mwenyewe anakiri kuwa yeye ndiye njia ya kweli na uzima. Dhambi ilitutenga na mungu lakini Kwa kumwamini yesu tunaingizwa tena kwenye ufalme wa mungu. " Yohana 3:16,"Kwa maana jinsi hii mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanae pekee ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele." Kwa kunukuu vifungu hivi vya biblia hakuna namna tunaweza kuona nguvu ya yesu kristo inatutoa kwenye mateso na shida na mahangaiko na kutukomboa, siyo dhambini tu bali kwenye kila hitaji letu pale tunapomuhitaji. Wapo wengi wanaoteseka Kwa kutafuta njia zisizo faha, Kwa waganga wa kienyeji kutafuta wabaya wao, Kwa mizimu ya mababu na hivyo kuteseka Kwa maisha yao yote, mfuate yesu kristo yeye atakuonyesha mambo makubwa ya ajabu usiyo yajua. Nikutakie siku Njema na mungu akubariki. Kinyagakelvin162@gmail.com https://kinyagakelvin.blogspot.com 0712161251 /0763766944

No comments:

Post a Comment