Sunday, 12 July 2020
Haya ndio majibu mawili ambayo unaweza kuwapa watoto wako wanapokuuliza maswali magumu...
Habari za wakati huu rafiki yangu, hongera kwa kuweza kuifikia jumapili nyingine tunakilatunakila sababu ya kumshukuru mungu, asante kwa kuzungukwa na watu wazuri pia na wanao tupenda, familia,Wazazi/walezi, ndugu jamaa na marafiki ni Zawadi tunazopaswa kuendelea kumshukuru mungu......
Rafiki utakubaliana na Mimi kwamba watoto ni watu wenye kupenda kudadisi vitu sana, hupenda kuuliza maswali magumu ili wapatiwe majibu sahihi lakini kwa bahati mbaya huwa hatuwapi majibu sahihi isipokuwa kuwadanganya ili kuondokana na usumbufu wa maswali hayo na pale wakiwa wakubwa tunaanza kushangaa ni wapi wamejifunzia uongo, pengine huwa hufahamu ni jibu gani unapaswa kuwapa ndio maana unadanganya, unakumbuka uongo tulio ambiwa watoto wanapatikana hospitalini kwa kununuliwa? Hili ni baadhi ya jibu la uongo tunalopenda kuwapa watoto lakini yapo mengi sana ambayo tunawadanganya na kuwapotosha kabisa, katika kupitia kwangu vitabu haya hapa ni majibu mawili sahihi kwao badala ya kuwkuwadaganya.
1.Mwambie akiwa mkubwa atafahamu;Badala ya kumdanganya kwa kumwambia mambo yasiyo sahihi mwambie awe na subira akiwa mkubwa atafahamu, hilo linaweza lisimtosheleze lakini litakuwa jibu sahihi, wengi watasema atakwenda kuuliza kwa mwingine na kupata jibu, lakini bado wewe utakuwa hujamfundisha uongo isipokuwa umemwambia siyo muda wake sahihi kulifahamu hilo.
2.Mwambie atumie akili yake; Vipo vitu vingi ambavyo hata sisi wenyewe hatuvifahamu na watoto wanapotuuliza tunaanza kuwapa majibu mepesi yasiyo na tija kwao, wewe huna pesa unamfundisha Mtoto kuhusu fedha, ni bora kumwambia atumie akili yake na kuja na mbinu tofauti kuliko kumdanganya, soma kwa bidii utapata fedha, huo bado ni uongo, ni bora ukamwambia swali hilo akamuulize mtu mwenye fedha alifanyaje akazipata fedha? Au atumie akili yake kwani wewe huna elimu hiyo kuliko kumpoteza kama ulivyopotea wewe.
Hayo ni baadhi ya majibu sahihi ya kumpa Mtoto wako, kuwa mkweli na Mtoto wako kufahamu kwamba kutofahamu Kila kitu ni hatua ya kufahamu mambo mengi zaidi.
Asante na nikutakie siku njema rafiki yangu.
Kinyagakelvin162@gmail.com
https://kinyagakelvin.blogspot.com
0763766944/0712161251
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment