Thursday, 2 July 2020

Unahitaji maandalizi.


Habari rafiki yangu, nikupongeze kwa siku nyingine ambayo ile bahati ya kuweza kuiona imetujia tena na hatufahamu bahati hii ni ya muda gani kutoka sasa, cha muhimu ni kujali muda na kutokubaliana upite bila kuishi kusudi ulilonalo.

Leo kwa ufupi kabisa nakukumbusha na nafahamu unafahamu hutoweza kushinda hata kama ndio hitaji lako bila ya maandalizi. Kocha mmoja aliyeitwa Bobby knight alipenda sana kuwaambia wachezaji wake "The will to win is not as important as the will to prepare to win".Kama unahitaji kushinda kweli basi tambuwa maandalizi ya kushinda ndio muhimu kuliko kitu chochote kwenye ushinda wako.

Rafiki kwa kuona umuhimu huo ndio maana napenda kukukaribisha ujiunge na kisima cha maarifa, kwani kuyasaka mafanikio ni kama kupigana vita na huwezi pigana vita peke yako unahitaji jeshi na jeshi unalopaswa kuungana nalo kwa mazoezi ya kushinda vita ya mafanikio ni Kisima cha maarifa.

Habari njema kwa wakazi wa moshi na Kilimanjaro ni kwamba kama ilivyo ratiba yetu kwa Kila Jumapili ya kwanza ya mwezi kwa wana kisima cha maarifa Tanzania tunakutana na kuweza kupeana mbinu za kushinda ikiwa na kupanga mipango yetu ya pamoja basi napenda kukuambia kwamba nina nafasi moja kwa Ajili ya wewe ambaye siyo mwana kisima cha maarifa na unaishi Kilimanjaro,karibu kwenye mkutano wetu utakaofanyika jumapili hii na utaweza kuona jinsi maandalizi ya kushinda yanavyohitaji kuwa na jeshi, nafasi ni moja pekee kama utahitaji tuwasiliane mapema.

Nikutakie siku njema na uwe wakati bora kwa maandalizi ya kufika kule unakotaka kufika.

Kinyagakelvin162@gmail.com

https://kinyagakelvin.blogspot.com

0763766944/0712161251

No comments:

Post a Comment